LUHANJO Kutoa Press Release Leo?


maamuzi yamefanyika RAIS WETU MPENDWA AKIWA HAYUPO OFISINI
 
maamuzi yamefanyika RAIS WETU MPENDWA AKIWA HAYUPO OFISINI

Jaribu kuwa na fikra pana, ni maamuzi gani yafanyike bila rais kufahamu? kama ni hivyo angemsimamisha Luhanjo basi kwa kufanya maamuzi bila yeye kuwepo ofisini.
Walikuwa wanajua wanachokifanya Luhanjo na Kikwete wake.
 
Mkuu ni nani aliowachagua hao watendaji wasiofaa na ni nani anaweza kuwafukuza...

Au kufaa kwa kiongozi kunapimwa vipi
umeuliza vema. Bw. Luhanjo amefanya kazi na rais wetu mda mrefu kazi kabla ya kuwa Katibu mkuu. Rais alipomchagua alijua anchagua mchapa kazi. Lakini sasa Rais yatosha kwa mtu huyu. Mengi ameharibu nasi tulikuwa kimya. Ilani yetu ni hii kwa rais wetu tunapolalamika sisi watendewaji basi na uyaweke malalamiko yetu kwenye notibuku yako ambayo hata Katibu wako Mtawa hayaoni. Kisha tuma vijana wa kazi wakuletee ukweli. Make good use of them. Usinyamaze kama Late Nyerere alivyolinyamazia suala lako la kule Monduli.
 
........FUKUZA hawa wazee ofisini kwako ikiwemo ngereja na Ludovic....

Kweli wanatakiwa kufukuzwa lakini Umemsahua na Malima. teh teh teh teh au una ajenda nyingine ?
 
Meno ya Luhanjo na mlio wa saa ya ukutani hayana tofauti kimaudhi. Ludovic Utoh kajiharibia jeshima yake kwa kumtetea Jairo. Ngereja kumpokea kwa kishindo Jairo wizara ya maji ni ishara ya kuchekelea maovu. wote watimuliwe kazi.
 
Rais lazima ajuwe nani anafanya nini pale ikulu.na pia si mda wa kucheza huyo LUHANJO ndiye aliyetajwa kuibeba maliasili na utaliii basi dhaili kuna kitu kinaendelea na bora atolewe yeye na watafata makatibu wengine wapuuzi na wazembe..
 
..........INATOSHA LUHANJO na wengine.makatibu wanakusanya kupeleka kwa luhanjo ili kukamilisha utamaduni wao wa kuchangia LUHANJO FUNDATION,na pasipo fanya hivyo unakwenda na maji."NITAWALINDA MIMI NIKO NA MKUU WA NCHI"
 
Hapo kwenye Red...sikubaliani na wewe.......mimi nimepoteza imani nae....hana kauli kabisa,yupo kimya mno.hao wasaidizi amewateuwa yeye mwenyewe kisha anashindwa hata kuwa wajibisha pale wanapokosea.......ama anawaonea haibu?Ushikaji kwenye kazi ni sumu-yeye(mkuru) halitambui hili?
''KUSEMA KWELI KWA HILI MMETUVUNJA MOYO VIBAYA MNO''
 
Jairo hakukosea aliposema wabunge wa chama cha wenye magamba ni sawa na ze-comedy na hao ni ndio wanaounda serikali ambayo ni sawa na ze-comedy serikali ambayo ina rais ambae ni sawa na ze-comedy aibuu!!!!!!!!watu wa ccm najua mnakipenda sana chama chenu ila wakati ukuta hamuwezi kushindana nao,kama vile kila nafsi itaonja mauti sembuse chama????????.Kweli watanzania wengi bado wako kwenye usingizi totoloo,na hata hapa jf wapo watu wenye mawazo mgando sana,hivi nyumbani kwako mambo yanapoenda mrama nyumba inakushinda unamlaumu nani??watoto wako??rafiki zako???jirani zako???? Jeykey usitufanye wote wajinga baki na ujinga wako kama ng'ombe aliyekwama matopeni,kwa uelewa wako Luhanjo hakuwa na mawasiliano na JK???HIYO YA WAPI WEWE??LALA ENDELEA KUNG'ATWA NA MBU,huyo ndiyo rais kigeugeu kumtudisha Jairo alikuwa anatesti zali tu alipogundua wabunge wamekuja juu karudisha majeshi nyuma,vuta subira.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…