Lowassa: Wauaji wa Albino wanyongwe

Lowassa: Wauaji wa Albino wanyongwe

Cardinal06

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2015
Posts
963
Reaction score
327
Waziri Mkuu zamani, Edward Lowassa ameitaka jumuiya ya albino nchini kuisukuma Serikali ili Rais Jakaya Kikwete asaini utekelezaji wa hukumu ya kuwanyonga wauaji wa albino.

Kauli ya Lowassa imekuja wiki moja tu baada ya Rais Kikwete kusema hajapelekewa majina ya watu 16 waliohukumiwa kifo kutokana na mauaji ya albino kutokana na mlolongo mrefu wa kisheria uliopo kabla ya kumfikia.

Rais Kikwete alisema hayo wakati wa ibada maalumu ya kuwekwa wakfu Askofu Liberatus Sangu kuwa Mhashamu Askofu wa Jimbo Katoliki la Shinyanga.

Hata hivyo, jana Lowassa aliyekuwa mgeni rasmi katika kampeni ya matembezi kupinga mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) yaliyoandaliwa na Klabu za Mbio za Pole ya Temeke na kushirikisha vikundi mbalimbali vya Dar es Salaam, alisema: “Ninampongeza Rais Kikwete kutokana na jitihada zake za kukemea mauaji ya albino. Pia, nimesikia kuna watu sita wametakiwa kunyongwa lakini kwa maelezo ya Rais hukumu hizo hazijamfikia, hivyo nawaomba mfanye msukumo ili Rais asaini.”

Kutokana na kukithiri mauaji hayo, Lowassa aliiomba Serikali kuunda kamati maalumu itakayokuwa ikichunguza mauaji ya walemavu hao bila kutegemea kamati za mikoa ili kuongeza ufanisi wa kuilinda jamii hiyo.
 
lowasa+picha.jpg

Edward Lowassa

KWA UFUPI
Kauli ya Lowassa imekuja wiki moja tu baada ya Rais Kikwete kusema hajapelekewa majina ya watu 16 waliohukumiwa kifo kutokana na mauaji ya albino kutokana na mlolongo mrefu wa kisheria uliopo kabla ya kumfikia.

Dar es Salaam
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa ameitaka jumuiya ya albino nchini kuisukuma Serikali ili Rais Jakaya Kikwete asaini utekelezaji wa hukumu ya kuwanyonga wauaji wa albino.

Kauli ya Lowassa imekuja wiki moja tu baada ya Rais Kikwete kusema hajapelekewa majina ya watu 16 waliohukumiwa kifo kutokana na mauaji ya albino kutokana na mlolongo mrefu wa kisheria uliopo kabla ya kumfikia.

Rais Kikwete alisema hayo wakati wa ibada maalumu ya kuwekwa wakfu Askofu Liberatus Sangu kuwa Mhashamu Askofu wa Jimbo Katoliki la Shinyanga.

Hata hivyo, jana Lowassa aliyekuwa mgeni rasmi katika kampeni ya matembezi kupinga mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) yaliyoandaliwa na Klabu za Mbio za Pole ya Temeke na kushirikisha vikundi mbalimbali vya Dar es Salaam, alisema: "Ninampongeza Rais Kikwete kutokana na jitihada zake za kukemea mauaji ya albino. Pia, nimesikia kuna watu sita wametakiwa kunyongwa lakini kwa maelezo ya Rais hukumu hizo hazijamfikia, hivyo nawaomba mfanye msukumo ili Rais asaini."

Kutokana na kukithiri mauaji hayo, Lowassa aliiomba Serikali kuunda kamati maalumu itakayokuwa ikichunguza mauaji ya walemavu hao bila kutegemea kamati za mikoa ili kuongeza ufanisi wa kuilinda jamii hiyo.

Mwanasiasa huyo anayetajwa kutaka kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu ujao, aliuambia umati uliokusanyika katika viwanja vya TCC Chang'ombe kuwa suala la ulinzi wa albino si la Serikali pekee bali la wananchi wote.

Mapema Machi mwaka huu, Mahakama Kuu ya Tanzania iliwahukumu watu wanne kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na kosa la kumuua Zawadi Magindu (32) mwenye ulemavu wa ngozi, mkazi wa Kijiji cha Nyamaruru, Wilaya ya Geita.

Kifungo cha CCM
Awali wakati akitoa hotuba yake Lowassa alisema kutokana na kifungo alichowekewa na CCM hawezi kuzungumza mambo mengi kwa sababu yatamletea balaa.

"Kule CCM bado nina kifungo, nikisema mengi nitaleta balaa," alisema huku akishangiliwa na kundi la vijana waliokuwapo uwanjani hapo.

Lowassa yupo kifungoni na makada wengine watano ambao ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Januari Makamba, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Mbunge wa Sengerema William Ngeleja, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Stephen Wasira na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye.

Aliyekuwa mbunge wa Temeke (CCM), John Kibaso alisema Lowassa alikubali kuwa mgeni rasmi baada ya kumuomba aridhie ombi hilo kutokana na mambo yake ya kisiasa yanayomkabili.

"Awali mgeni rasmi ilibidi awe mbunge wa Ilala, Mussa Zungu lakini ikabidi tumuombe Lowassa aliyetuambia kuwa anaogopa CCM kwa kuwa haijaruhusu mambo hayo.

Hata hivyo, ndani ya wiki moja mzee wetu alikubali kushiriki nasi kama mlivyomuona," alisema Kibaso.

Katika maandamano hayo Lowassa aliviongoza vikundi mbalimbali vya mbio za pole katika matembezi ya haraka kutoka Uwanja wa Taifa hadi viwanja vya TCC Chang'ombe.

Pia aliongozana na Mbunge wa Temeke (CCM) Abbas Mtemvu, Mbunge wa Kinondoni (CCM), Idd Azzan na Zungu.

Mwenyekiti wa chama cha watu wenye albino Tanzania (TAS), Ernest Kimaya alisema ukataji wa viungo na kuuawa kwa watu wenye ualbino umetia doa nchi jambo ambalo linapaswa kukemewa na wadau mbalimbali.

Alisema mauaji hayo yameongezeka kwa kasi kuanzia mwaka 2006 ambapo hadi sasa watu wenye ulemavu huo wameuawa 75, waliojeruhiwa kwa kukatwa viungo ni 35 na makaburi 15 yalifukuliwa na kuchukuliwa viungo vya mwili.

CHANZO: Mwananchi(Jumatatu,Aprili 20 2015)
 
Kichwa cha habari na utumbo wa habari tofauti kabisa.
 
wabaya kweli sa iz wamehamia kwenye ajali mpk za stool za vioo
 
Hivi kwani anayemuua binadamu asio albino anafanywa nini? Na ni wapi albino anatofautishwa na asie albino mpaka hukumu ya mauaji yake ipiganiwe kuwa ni kunyongwa kana kwamba hapo awali haikua hivyo?
 
Wanajamvi

Juzi wakati Lowassa akiwa mgeni rasmi kwenye matembezi ya kupinga mauaji ya albino, alitoa kauli moja yenye ushupavu mkubwa sana. Ni kauli ya mamlaka, naweza kusema hivyo.

Nukuu isiyo rasmi "......wauaji wa albino wapelekwe kwa rais"

Kauli hii inaonyesha waziwazi kuwa ukiwa kiongozi mkuu wa taifa unapaswa kudili na matukio hatarishi kama haya mauaji ya albino perpendicularly bila kupepesa macho.

What if kama Lowassa ndo angekuwa rais wakati mauaji haya yanatokea, guess nini kingetokea kwa hao wauaji.

Big up sana Lowassa. Unazungumza kimamlaka something that our country lacked for long!

Watanzania wanakumbuka ulivyozungumza kimamlaka kuhusu mkataba wa DAWASA. Watanzania wanakumbuka ulivyozungumza kimamlaka kuhusu maji ya ziwa Victoria.
 
Kuhusu ushupavu na msimamo wa Lowassa haipingiki kwamba ni kiongozi. Leo hii CCM wanajitahidi kupingana na MTU anayeungwa mkono na makundi tote ya kijamii. CCM na kiongozi wake wake wakijua kuwa huko ni kupoteza dira.

Wakitaka chama kisife kifo cha asili wajitahidi sana kuwa waangalifu. Wale wanaojinasibu kuwa wanakubalika wapelekwe mbele ya vikao vya chama viamue vyenyewe. Atakaeshidwa Kama ni mkulima akalime, mvuvi akavue na huyo Kama atakuwa ni mfugaji akafuge mbuzi, ngombe na kondoo.
 
nyoooookooo, yaani wauaji wapelekwe kwa rais wakanywe juice kama waendavyo akina diamond na wasanii wengine sio? pumbafu kabisa, na hii ni kauli ya kishoga kabisa kutolewa na huyu fisadi anayetaka urahisi, bora hata kauli ya Pinda ya wanaoua albino nao wauawe, hiyo ndo kauli hasa.
 
Jk atakuwa amepata huu ujumbe ataufanyia kazi naomba zile EL akiwa anakimbia kwenye hayo matembezi@Team Lowassa
 
Msituchezee akili na huyoEdward wenu,akapumzike time out kwake
 
Hivi kwani anayemuua binadamu asio albino anafanywa nini? Na ni wapi albino anatofautishwa na asie albino mpaka hukumu ya mauaji yake ipiganiwe kuwa ni kunyongwa kana kwamba hapo awali haikua hivyo?

Wanyongwe tu bila kufuata taratibu za kisheria? utakuwa utawala gani huo? Je wapo watu wangapi magerezani wanaosubiri kunyongwa? kwanini hawa hukumu yao iharakishwe namna hiyo? mnataka kuficha nini? hao madereva wanaochinja watu mabarabarani kilasiku sio wauwaji? mbona wanunuzi wa hivyo viungo hamhangaiki nao? je kunyonga si ni kuua kulekule mtatofautianaje na hao wauaji. JK wasikupeleke mputa ukachuma dhambi bure, mwachie aje kuwanyonga yeye.
 
lowasa . mdomo umponza mtu . kutoa kibali cha kunyonga sio kitu laisi kama unavyofikilia .kwanza wanaokwenda jera sio wote wenye hatia .pil na amini hata ww mwenyewe unajuwa kwamba ukumu ya kunyonga imefutwa na umoja wa taifa . na mahanisha haki za binadamu hivyo basi kikwete naona bado mapema sana kutoa hukumu hiyo . pia ni kweli hinauma hukiona mwezio kakatwa mkono au mguu .ushauri wangu kwa lowasa usifanye kampeni kiaina mwambie best wafunge kifungo cha maisha na kazi ngumu na kila siku hasubuhi na jioni wawe wanachapwa viboko kumi kumi
 
Wanyongwe tu bila kufuata taratibu za kisheria? utakuwa utawala gani huo? Je wapo watu wangapi magerezani wanaosubiri kunyongwa? kwanini hawa hukumu yao iharakishwe namna hiyo? mnataka kuficha nini? hao madereva wanaochinja watu mabarabarani kilasiku sio wauwaji? mbona wanunuzi wa hivyo viungo hamhangaiki nao? je kunyonga si ni kuua kulekule mtatofautianaje na hao wauaji. JK wasikupeleke mputa ukachuma dhambi bure, mwachie aje kuwanyonga yeye.

Eddy, hii unanijibu mimi au ni majibu general kwa wanaotaka walioua albino wanyongwe? Sijakuelewa kwasababu hakuna mahali niliposema wanyongwe bila kufuata taratibu za kisheria, sijui kuna uhusiano gani kati ya wingi wa watu wanaohukumiwa kunyongwa gerezani na kuhukumu wauaji wengine kunyongwa? Sijasema kokote hawa hukumu yao iharakishwe, ajali za barabarani sijui unaziona zina uhusiano upi na uuaji wa makusudi wa mtu?
Sijui ni kwanini akili mwako unafikiri nikisema wauaji wa albino wanyongwe sijajumuisha na hao wanunuao?

Yani ni kama umerukia treni kwa mbele vile, sikuelewi. Hembu rudi tena pole pole.
 
Back
Top Bottom