Lowassa umeturoga?

Mssassou

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2015
Posts
1,537
Reaction score
597
Mbona unapendwa sana?Kila mahali ni Lowassa na UKAWA,Lowassa mganga wako ni mzungu?Mikutano yako yote watu wanajaa pomoni kwa nini?Hamtumii wasanii(fiesta) kuwavutia watu,mabango yako ni machache sana lakini uko kwenye mioyo ya watu kwa nini?Unafedheheshwa kila siku lakini watu bado wanaimani na wewe,uwe mwizi,fisadi au mgonjwa watanzania wanasema watakuchagua hivyohivyo.Lowassa ,mimi niko kijijini Kisewe wilaya ya Ulanga mkoa wa Morogoro jina lako limetawala sana kwa vijana na wazee.Lowassa umeturoga?Hata mimi navutiwa na wewe lakini sijui kwa nini kwako
 

Hajakuroga ila yupo kwa wakati muafaka ni wakati wa Mabadiliko na kocha wetu kamsajili Messi.
 
Kama kweli ameloga hiyo dawa mimi imeniingia kisawa sawa, siambiwi, sisikii wala sioni... Mahaba niueeee Lowassa huyu daa!
 
Huyu jamaa kiukweli ni noma sana ndani ya miezi miwili tu kule FB anakaribia washinda watu waliokuwa huko toka 2010..
Kiukwelj watu wanampenda sana Lowasa, japo wote hawatamuona ila kwa tuliomuona twasambaza upendo ili watu wampe kura hadi alie machozi ya furaha
 
hoja hapa ni KURA si tu kwa kujaza mikutano kukubalika ni KUPATA KURA nyingi haina maana kujaza mkutano NA usipate KURA.mkisomba WATU lazima mtajaza
 
suala hapo sio upendo kwa Lowasa kiukweli wananchi wengi wamegudua kwamba ccm ni tatizo kubwa kwa maendeleo ya nchi yetu hivyo wameamua kumchagua kiongozi aliye mbali na ccm hata kama asingekuwa Lowasa yeyote angelisimama upande wa UKAWA angependwa kama anavyopendwa Luwasa, kilichomsaidia Lowasa zaidi ni kwa sababu alikuwa na wapenzi ndani ya ccm hivyo wamemfuta, na hilo ndilo Mbowe aliliangalia zaidi
 
Kuna kabibi kalihojiwa na Sam Mahela kakasema ana nyota ya utawala naanza kuamini maneno ya yule bibi
 
hoja hapa ni KURA si tu kwa kujaza mikutano kukubalika ni KUPATA KURA nyingi haina maana kujaza mkutano NA usipate KURA.mkisomba WATU lazima mtajaza

Pole Mkuu, lazima uchukie lkn ndio hali halisi, aliyekuambia hawatapiga kura ni nani, na kwanini wakijaa UKAWA sio wapiga kura ila wakijaa CCM ndio wapiga kura, karibu pande za hapa Recreation UKONGA nikugonge na kabukuli ka supu mkuu, hali ni mbaya huko lumumba so sio mbaya tukakutana na kutoa stress.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…