Lowassa, si usaidie na masikini

Lowassa, si usaidie na masikini

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,171
Reaction score
162,618
Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi la leo,mh.Lowassa amechangia shilingi milioni 50 katika harambee ya CCM huko Zanzibar .Mh.Lowassa alialikwa na chama katika harambee hiyo sambamba na baadhi ya wagombea uraisi wengine ambao nao walichangia kila mmoja shilingi miliono 10 Makongoro akiwemo huku Wassira akichangia milioni 5 na Mwandosya akichangia milioni 1.5.

Pinda na marafiki zake ndio walitia fora kwa kuchangia sh milioni 203.

Nachojiuliza hivi mbona sijawahi kumsikia mh.huyu akisaidi masikini wanaaomba milioni 2 au 3 ili kwenda India kwa matibabu?

Kama unaweza kutoa milioni 50 kuchangia chama ni kwanini basi usisaidie masikini hawa wanaomba misaada kwenye vyombo vya habari?

Milioni 50 ungeokoa maisha ya vichanga vinavyokufa kwa magonjwa ya moyo n.k.

Mh.ukiweza anzisha hata "foundation" walau utakumbukwa kwa hilo kuliko hela zako zikaishia kwenye mambo ya siasa tu.

Mh.hili ni ombi na ushauri ili kusaidia wanaoteseka au kufa na magonjwa kwa kushindwa kugharamia matibabu.

Huwa nasikitika sana kuona watanzania wanaomba misaada ya matibabu kupitia vyombo vya habari ili kuokoa maisha yao.

It pains a lot.

Ushauri huu unamuhusu hata Sabodo na matajiri wengine isipokuwa mzee Mengi tu ambae husaidia sana jamii.
 
Lowasa ni attention seaker tu
 
urais unasakwa by hooks and crooks
 
Yeye na masikini wapi na wapi , huko anakochangia ndiko anakowekeza then 50 milioni itengeneza bilioni 50 .
 
Ukitaka kujua kuwa huyu jamaa ni hana hutu nenda jimboni kwake ndio kuna ombaomba Arusha nzima na hana hata hutu angekwenda kusaidia hata wale wagonjwa wa Seriani.


swissme
 
Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi la leo,mh.Lowassa amechangia shilingi milioni 50 katika harambee ya CCM huko Zanzibar .Mh.Lowassa alialikwa na chama katika harambee hiyo sambamba na baadhi ya wagombea uraisi wengine ambao nao walichangia kila mmoja miliono 10 na Wassira milioni 1.5.

Nachojiuliza hivi mbona sijawahi kumsikia mh.huyu akisaidi masikini wanaaomba milioni 2 au 3 ili kwenda India kwa matibabu?

Kama unaweza kutoa milioni 50 kuchangia chama ni kwanini basi usisaidie masikini hawa wanaomba misaada kwenye vyombo vya habari?

Milioni 50 ungeokoa maisha ya vichanga vinavyokufa kwa magonjwa ya moyo n.k.

Mh.ukiweza anzisha hata "foundation" walau utakumbukwa kwa hilo kuliko hela zako zikaishia kwenye mambo ya siasa tu.

Mh.hili ni ombi na ushauri ili kusaidia wanaoteseka au kufa na magonjwa kwa kushindwa kugharamia matibabu.

Huwa nasikitika sana kuona watanzania wanaomba misaada ya matibabu kupitia vyombo vya habari ili kuokoa maisha yao.

It pains a lot.

Ushauri huu unamuhusu hata Sabodo na matajiri wengine isipokuwa mzee Mengi tu ambae husaidia sana jamii.

Alafu anaomba uraisi, akaufuate wa chama na sio wa nchi na watanzania
 
Ukitaka kujua kuwa huyu jamaa ni hana hutu nenda jimboni kwake ndio kuna ombaomba Arusha nzima na hana hata hutu angekwenda kusaidia hata wale wagonjwa wa Seriani.


swissme

Ur correct madam kwa kweli huyu lowasa hana "HUTU" ila kwa UTU anao.
 
Monduli yenyewe kuna sehemu barabara tabu maji hamna shule ndio kabisa watoto wanakaa chini, shule zinajengwa na Ngos za wazungu lakini wanakuwa kimbele mbele cha kuweka mawe ya msingi na kufungua.

Matokeo yake vijana wengi wanakimbia umasaini wanakuja kuwa walinzi na wauza ugolo.
 
Monduli yenyewe kuna sehemu barabara tabu maji hamna shule ndio kabisa watoto wanakaa chini, shule zinajengwa na Ngos za wazungu lakini wanakuwa kimbele mbele cha kuweka mawe ya msingi na kufungua.

Matokeo yake vijana wengi wanakimbia umasaini wanakuja kuwa walinzi na wauza ugolo.

Katoa hela nyingi sana kulinganisha na wenzake na bado anaweza kutoswa tu.
 
Ukitaka kujua kuwa huyu jamaa ni hana hutu nenda jimboni kwake ndio kuna ombaomba Arusha nzima na hana hata hutu angekwenda kusaidia hata wale wagonjwa wa Seriani.


swissme

Wagonjwa wa Seliani ya Jimbo la Arusha mjini kwanini wasisaidiwe na Lema?Au na yeye njaa kali?
 
Hakika wewe unakilimbitwa nyuma na mbele! Kila siku Lowassa Lowassa... Tayari ameoa na anawatoto na wajukuu... Heading yako kwanini isiwe Pinda aliechanga fedha za ESCROW?...Hakuna mpuuzi humu JF kama wewe na akina Chooni ...
 
urais unasakwa by hooks and crooks
Tena kwa kutumia well-defined strategy.Lazima awahonge hao maccm ili wampititishe kuwa mgombea.Akimsaidia mtoto mgonjwa wa moyo huko Ilamaduhu, huyo mtoto atamsaidiaje Lowassa kuingia ikulu?
 
kachangia maskini wengi tuu wakiwemo wale wa UDOM, Mashekh wa Bagamoyo na wachungaji, wanafunzi wa vyuo vikuu vya Iringa na SAUT aliwachangia kwa sharti la kumshawishi agommbee uraisi
 
je hao waliotoa 200 na kitu je hawatakiwi kusaidia hao maskini? naona na wewe upo kwenye ugonjwa unaowasumbua watu kwa sasa, wa lowassa.
 
eee bhana mkuu umeandika jambo zito sana ambalo nina hakika hata lowasa mwenyewe hataki hata kulisikia , inasikitisha sana kuona wako vijana wanauza hata figo zao ili waweze kujikimu, lakini wenye uwezo ( wa halali au haramu ) wanaangalia tu , bali tetesi zinadokeza kwamba wanasiasa wenye mahesabu ya urais hawako tayari kusaidia mtu ambaye uhakika wake wa kufika octoba ( kiafya ) ni wa mashaka ! maana hakuna uhakika kama watakuwa hai hadi wakati huo ! nipe nikupe !
 
je hao waliotoa 200 na kitu je hawatakiwi kusaidia hao maskini? naona na wewe upo kwenye ugonjwa unaowasumbua watu kwa sasa, wa lowassa.
Jumlisha hela zote alizogawa lowasa tangu aanze hii huruma yake ya mashaka , hakika utashika kiuno !
 
Anayetoa misaada ya kijamii sio Mengi tu. Wapo matajiri wengi tu WaTZ wanatoa misaada ya kijamii lakini hawapendi majina yao yatangazwe.
 
Hakika wewe unakilimbitwa nyuma na mbele! Kila siku Lowassa Lowassa... Tayari ameoa na anawatoto na wajukuu... Heading yako kwanini isiwe Pinda aliechanga fedha za ESCROW?...Hakuna mpuuzi humu JF kama wewe na akina Chooni ...
Lugha za aina hii ndio zinawapa watawala justification ya kutuletea cyber law.

Anyway,signature yangu hapa chini inakuhusu sana.
 
Back
Top Bottom