Lowassa: Nitamtoa Babu Seya gerezani

Status
Not open for further replies.
Mh Edward Lowassa amesema hatua zinazochukuliwa na Rais magufuli ni utekelezaji wa ilani ya ukawa.Amesema yale aliyoyapigia kelele wakati wa kampeni ndiyo yanayotekelezwa na Rais Magufuli."lakini nawataka wakiri basi kuwa wanatekeleza sera za lowassa na ukawa".amesema.Aidha Ameipongeza serikali ya Magufuli kwa kumwachia huru sheikh Ponda na kuelezea matumaini yake kesi ya babu seya nayo itaangaliwa upya.

Mytake: ukizingatia 2006 kipindi Babu Seya anahukumiwa, Lowassa alikuwa waziri mkuu. Katika kipindi cha kampeni mpaka sasa (leo, Arusha) amekuwa akisisitiza kuhusu hii kesi kuangaliwa upya, WHY?

Kwangu mimi, nabaki na maswali mengi sana!.. Na kuna mengi ya kuyatafutia majibu....
 
Lowasaaa mabadiliko mabadiliko Lowasaaa nlikuw nmeanza kusahau naona mtoa mada kanikumbusha, co mbaya tunaisubir 2020 tukuweke madarakan mzee, we endelea kukaa bech uku ukipasha pasha misuli nchi yko hii?
 

Wewe na mtu wako wote ni machizi, kuhusu sheikh ponda hukumu yake ilikuwa imeshatayarishwa kabla ya hata magufuli hajaapishwa ila ilikuwa inaahirishwa kwa dharura tofauti hata wakati mwingine ilikuwa hakimu ana majukumu mengine n.k lakini issue ya babu seya ni tofauti kwani yeye alishahukumiwa siku nyingi na bahati mbaya kesi kama yake ya kubaka tena vitoto haina msamaha, lakini pia acha kupotosha kuwa alihukumiwa 2006 ukweli alihukumiwa 2004
 
Hii ni mpya. Kiongozi wa mafisadi kudai eti yeye ana sera za kupinga ufisadi. Hapo alipo anatoa machozi kwa sababu mafisadi wenzake waliobaki CCM wanashughulikiwa na kwa vile ni mtandao na wanagawana matunda ya ufisadi hata yeye Lowassa ni mwathirika wa hatua za Magufuli. Ikiwa mara tu aliponunua CHADEMA hatua ya kwanza ilikuwa kwa CHADEMA kuondoa ufisadi kwenye ilani na tena kutoitamka hata kidogo kwenye kampeni iweje leo aseme Magufuli anatekeleza sera za chama chake? Au anafikiri Watanzania tumeshasahau mambo aliyokuwa anazungumzia wakati wa kampeni? Anajiganganya kama alivyodhani watanzania wamesahau alivyowafisadi kwenye Richmond mpaka kuitwa gamba na CCM kumbe hawajasahau na wakamdhihirishia kuwa bado wanakumbuka walipomnyima kura 25/10.

 

Kwa maana hiyo alipogombea akiwa CCM alikuwa na nia ya kutekeleza ilani ya CDM?

Hivi mpaka leo hajasoma vifungu vya ilani ya CCM anavyotekeleza JPM? Au anadhani ipo kwenye website ya CCM kama alivyoinadi ya CDM wakati wa kampeni.

Watanzania hawatajali ni ilani ipi inatekelezwa kwa sababu matatizo yao ya msingi yapo wazi. Kubwa ni nani mwenye uwezo wa kuyatatua bila porojo.
 
yaelekea anajua ukweli hapo wa iyo kesi
 
Lowasaaa mabadiliko mabadiliko Lowasaaa nlikuw nmeanza kusahau naona mtoa mada kanikumbusha, co mbaya tunaisubir 2020 tukuweke madarakan mzee, we endelea kukaa bech uku ukipasha pasha misuli nchi yko hii?

Tehe Tehe Tehe.
 

History repeat itself.
 
Kulikuwa na kitu mjomba .
 
Mungu pekee anajua
 
Ndugu wanajamvi.
Wengi wetu tulimsikia kwenye kampeni za kugombea uraisi mwaka 2015 Mh. Edward Lowasa kwamba angemtoa babu seya na wanawe.
Lakini watu Wengi walimsema vibaya kwamba anatetea waovu.
Asante Mungu yametimia kwani wametolewa kwa kipindi kifupi.
Heko Lowasa.
 
Ila kwakuwa katoa Magu ina faida
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…