Myelife
Senior Member
- Dec 31, 2011
- 164
- 107
Ndugu watanzania wenzangu,
Kuna habari nyingi sana kuhusu Mh Ed Lowasa, tangu mwaka mmoja na nusu uliopita kawa gumzo sana hapa Tanzania, hii ni kwakuwa ni mwasasiasa mkomavu/ mkongwe na pia mvumilivu sana.
Kuhusu ufisadi sina ushahidi wowote juu ya hili kwa hiyo namwachia yeye na Mola wake, mimi kama binadam ningepata ushahidi ningeweza kusema jambo, au kama mitambo ya Dowans ingetaifishwa pia ningeweza kuwa na maswali hasi juu yake, na ndiyo maana namwachia Mungu.
Suala la matumizi ya fedha na utajiri wake, tunamhukumu bure kwani A. Chenge angeanza kuhukumiwa kabla ya ED Lowassa ningeona kuna mazingira salama katika mchezo lakini pia ni nani anaependa umasikini?
Mimi nina mtizamo wa kiliberali, napenda kuwakumbusha pande zote mbili za CCM JK na CCM Lowassa kuwa, CCM wanapaswa kujua sasa vita hawapambani na Lowassa kama mtu bali wanapamba na Lowassa kama Taasisi hatarishi katika karata yao, hii nina maana kama itatokea ED Lowassa akaihama nchi leo taasisi hii itaendelea kubaki nchini na kuwa kama kansa itakayoendelea kuwatafuna CCM, hivyo wanapaswa kuiheshimu na kubadili mbinu ya vita.
TeamLowassa nao wanapaswa kujua kuwa wao sasa ni kama taasisi wanapaswa kujipanga kwa spidi ya kijeshi, waache kutoa matamko kila mara, na pia wao ndiyo wanauwezo wa kuamua kwa sasa chama kipi wakipe ushindi, kama wanataka kuvuka mstari wakati ni sasa, maana wakichelewa watachelewesha ushindi katika chama chochote, ila kama hawajaamua kuvuka mstari wajue wanaweza kuondoka katika siasa kwa kipindi fulani kwani teamLowassa ni ngumu kunusa au kulamba hata udiwani kwani watakuwa na kashfa ya kukiyumbisha chama.
Hivyo nawashauri kama hawavuki mstari kwenda chama kingine hata form ya udiwani wasichukue. ila kama wanataka kuendelea kuwepo katika siasa wafanye mara moja. pia teamLowassa hii isiwe na unafiki uliopitiliza wa kusema maneno mabaya kuhusu CCM hali ya kuwa wanaendelea kuzimiliki kadi za CCM.
Tungependa kuona watu wafanye wanachosema na siyo kuendelea kuongea wakiwa katika kivuli cha wapenda mabadiliko hali ya kuwa hawana meno yoyote katika chama.
katika taasisi hii kuna mkakati mmoja utakuwa unapikwa lakini ni lazima wajue muda si rafiki tena.
Pia wasiogope kwenda vyama mmbadala na pia vyama mmbadala wasisite kumpokea yeyote, kwani kabla ya kiongozi yeyote kumkatalia Lowassa uanachama anapaswa kujiuliza, je yeye hajawahi kuhama chama au ameshawapokea wanachama wangapi kutoka vyama vingine na ndiyo atoe maamuzi.
wamarekani wana msemo wao, "America has no permanent enemy but permanent interest" katika siasa husema hakuna adui wala rafiki wa kudumu katika siasa.
Karibuni wanajamvi.
Kuna habari nyingi sana kuhusu Mh Ed Lowasa, tangu mwaka mmoja na nusu uliopita kawa gumzo sana hapa Tanzania, hii ni kwakuwa ni mwasasiasa mkomavu/ mkongwe na pia mvumilivu sana.
Kuhusu ufisadi sina ushahidi wowote juu ya hili kwa hiyo namwachia yeye na Mola wake, mimi kama binadam ningepata ushahidi ningeweza kusema jambo, au kama mitambo ya Dowans ingetaifishwa pia ningeweza kuwa na maswali hasi juu yake, na ndiyo maana namwachia Mungu.
Suala la matumizi ya fedha na utajiri wake, tunamhukumu bure kwani A. Chenge angeanza kuhukumiwa kabla ya ED Lowassa ningeona kuna mazingira salama katika mchezo lakini pia ni nani anaependa umasikini?
Mimi nina mtizamo wa kiliberali, napenda kuwakumbusha pande zote mbili za CCM JK na CCM Lowassa kuwa, CCM wanapaswa kujua sasa vita hawapambani na Lowassa kama mtu bali wanapamba na Lowassa kama Taasisi hatarishi katika karata yao, hii nina maana kama itatokea ED Lowassa akaihama nchi leo taasisi hii itaendelea kubaki nchini na kuwa kama kansa itakayoendelea kuwatafuna CCM, hivyo wanapaswa kuiheshimu na kubadili mbinu ya vita.
TeamLowassa nao wanapaswa kujua kuwa wao sasa ni kama taasisi wanapaswa kujipanga kwa spidi ya kijeshi, waache kutoa matamko kila mara, na pia wao ndiyo wanauwezo wa kuamua kwa sasa chama kipi wakipe ushindi, kama wanataka kuvuka mstari wakati ni sasa, maana wakichelewa watachelewesha ushindi katika chama chochote, ila kama hawajaamua kuvuka mstari wajue wanaweza kuondoka katika siasa kwa kipindi fulani kwani teamLowassa ni ngumu kunusa au kulamba hata udiwani kwani watakuwa na kashfa ya kukiyumbisha chama.
Hivyo nawashauri kama hawavuki mstari kwenda chama kingine hata form ya udiwani wasichukue. ila kama wanataka kuendelea kuwepo katika siasa wafanye mara moja. pia teamLowassa hii isiwe na unafiki uliopitiliza wa kusema maneno mabaya kuhusu CCM hali ya kuwa wanaendelea kuzimiliki kadi za CCM.
Tungependa kuona watu wafanye wanachosema na siyo kuendelea kuongea wakiwa katika kivuli cha wapenda mabadiliko hali ya kuwa hawana meno yoyote katika chama.
katika taasisi hii kuna mkakati mmoja utakuwa unapikwa lakini ni lazima wajue muda si rafiki tena.
Pia wasiogope kwenda vyama mmbadala na pia vyama mmbadala wasisite kumpokea yeyote, kwani kabla ya kiongozi yeyote kumkatalia Lowassa uanachama anapaswa kujiuliza, je yeye hajawahi kuhama chama au ameshawapokea wanachama wangapi kutoka vyama vingine na ndiyo atoe maamuzi.
wamarekani wana msemo wao, "America has no permanent enemy but permanent interest" katika siasa husema hakuna adui wala rafiki wa kudumu katika siasa.
Karibuni wanajamvi.