Lowassa ni Sokoine mpya

Lowassa ni Sokoine mpya

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,252
Reaction score
16,171
Nina imani sana na kabila la kimaasai kwa utendaji kazi wao na kuchukua maamuzi ya haraka na yenye manufaa. Labda hii inatokana na aina ya malezi, makuzi na mafundisho wanayopewa ndani ya jamii yao yanaozingatia uwajibikaji na utoaji taarifa sahihi kwa ngazi zao za juu kwenye familia. Mgawanyo wa kazi (division of labour) na kuheshimiana (respect) ni miongoni mwa mambo ambayo jamii nyingi zinapaswa kujifunza kutoka kwa wamasai. Hawana matani wala kuchekacheka kwenye mambo ya msingi, ni wakweli na wenye msimamo usioyumba. Hata mtoto mdogo anaweza kufanya kazi ya kuchunga na kuhesabu ndama na mbuzi kwa usahihi kabisa.

Kila mtu alikunwa na sifa na uongozi wa Sokoine (rip) alipokuwa mtumishi wa serikali na waziri Mkuu, alikuwa kiboko ya uhalifu na wahalifu nchini hadi akawa tishishio hata kwa watendaji wenzake kwa speed yake ya kufanya kazi na kuchukia uzembe na wizi. Hatumchagui mtu kutokana na kabila lake tu, lakini ni kweli pia yapo makabila mengine ambayo yana idadi kubwa ya watu wavivu, waongo, wazembe, wapenda porojo na wasiothamini kazi. Wanafundishwa kucheza ngoma usiku kucha, kuoa na kuolewa mapema na kucheza bao mchana kutwa.

Lowassa ana sifa za kuchapa kazi, kuchukuwa maamuzi haraka na kuchukia umaskini, hizi ni sifa halisi (typical) za kabila za kimasai, sio za kujifunza tu darasani. Mmasai amefundishwa kuwa na mali (ng'ombe) nyingi, hivyo sishangai kusikia Lowassa kuwa tajiri ana asili navyo.

Huwenda Lowassa akafanana kiutendaji na mmasai mwenzake hayati Edward Moringe Sokoine, tena wote ni ma-edward
 
mimi nitampigia kura kwa sb mbili moja ni sera yake ya elimu,pili kuchukia kwake umaskini.
 
Usimfananishe Sokoine na huyo fisadi. Wakati wa Sokoine wahujumu uchumi walikuwa wanatupa mali zao kwa mikon yao hawakuwa wanasubiri kukamatwa. Ulinganifu uliouleta hapa haupo kabisa dunia ya leo. Sijui umewaza nini mpaka umlinganishe Fisadi na Sokoine.
 
Usimfananishe Sokoine na huyo fisadi. Wakati wa Sokoine wahujumu uchumi walikuwa wanatupa mali zao kwa mikon yao hawakuwa wanasubiri kukamatwa. Ulinganifu uliouleta hapa haupo kabisa dunia ya leo. Sijui umewaza nini mpaka umlinganishe Fisadi na Sokoine.
Fisadi kwa namna gani? wivu wa kike huo. Lowassa hajaiba angeshakwenda jela kama Mramba. Kilichofanyika kwa richmond ni sawa na mzazi aliyejamba mbele za watu kisha kumsingizia mtoto wake mdogo aliyekaa pembeni yake kuwa ndiye aliyejamba ili kuficha aibu yake. Na mtoto mwenye adabu nzuri hawezi kubishana na mzazi wake pale kuwa sio yeye aliyejamba. Jukumu la mzazi kwenye tukio kama hilo ni kumuaibisha tu mtoto kuwa yeye ndiye mhusika wa harufu ile mbaya lakini hawezi kumfinya wala kumpiga kwakuwa anafahamu kuwa anamzingizia tu, ila mtoto anaweza kukumbana na adhabu kali kama atakosa adabu na kumwambia mzazi wake sio mimi ni wewe (mzazi) uliyejamba. Lowassa hakupelekwa mahakamani kwakuwa walijuwa kuwa lilikuwa kosa la kusingiziwa ili kuinusuru serikali kuanguka sawa na mtoto aliyesingiziwa kujamba na mzazi wake ambavyo hapigwi wala kufinywa baada kuaibishwa yeye badala ya mzazi.
 
Wamasai huwa niwatendaji wazuri ktk serikal, sokoine alikuwa mumasai naleo hii hatuta musahau, Edo anafaa kaz 2mpe kit
 
Moringe Sokine amekufa akiwa na 'mashati' matatu tu! na alikemea ufisadi waziwazi sio huyu aliyejimilikisha Ranchi za taifa!
 
Unaushaidi kama hunaushaidi funga mudomo au nenda mahakaman.
 
Alishasema mkazigawane kama ni zake
Kama mtu akiipigia kura SSM akapimwe Kwa mkichwa
 
utendaji kazi wa Sokoine ulighalimu maisha yake,pia utendajikazi wa Lowassa ulighalimu uwaziri mkuu wake viongozi wa fisiem wanamuogopa ndiyo maana hawataki na wanajaribu kuzusha tu ili wamharibie
 
Mwaka huu hawana namuna lazima wapigwe mafisim hawa lo! lala salama sokoine ulituachia lowasa.
 
watanzania walilia sana alipotutoka sokoine jembe la ukweli dhidi ya wahujumu uchumi enzi za siasa za ujamaa. mtu aliyeamini ktk ujamaa bila chembe ya wasiwasi kumshinda hata muasisi wa sera hiyo julius nyerere. mzalendo wa kweli mwana mwaminifu, aliyeipenda taifa akafa kwa ajili ya upendo wake kwa taifa hili. je lowasa kwa jinsi anavyojitanabaisha anaweza kuwa suluhisho la mkwamo tulionao akawa kama sokoine? ni wazo tu ila nashawishika anaweza kwa kuwa wanaompinga ni wengi ni wale waliompoteza sokoine
 
mara kwa mara anasema maendeleo ya tanzania tutaenda kwa speed 120 anamaanisha kas itakayokuwa kwa maendeleo kama sokoine alikuwa akisema kinachofuata ni tendo nadhani lowasa ni mojawapo tumemwona kwa sekondar za kata
 
Fisadi kwa namna gani? wivu wa kike huo. Lowassa hajaiba angeshakwenda jela kama Mramba. Kilichofanyika kwa richmond ni sawa na mzazi aliyejamba mbele za watu kisha kumsingizia mtoto wake mdogo aliyekaa pembeni yake kuwa ndiye aliyejamba ili kuficha aibu yake. Na mtoto mwenye adabu nzuri hawezi kubishana na mzazi wake pale kuwa sio yeye aliyejamba. Jukumu la mzazi kwenye tukio kama hilo ni kumuaibisha tu mtoto kuwa yeye ndiye mhusika wa harufu ile mbaya lakini hawezi kumfinya wala kumpiga kwakuwa anafahamu kuwa anamzingizia tu, ila mtoto anaweza kukumbana na adhabu kali kama atakosa adabu na kumwambia mzazi wake sio mimi ni wewe (mzazi) uliyejamba. Lowassa hakupelekwa mahakamani kwakuwa walijuwa kuwa lilikuwa kosa la kusingiziwa ili kuinusuru serikali kuanguka sawa na mtoto aliyesingiziwa kujamba na mzazi wake ambavyo hapigwi wala kufinywa baada kuaibishwa yeye badala ya mzazi.

Hii ngonjera yako kawapelekee watoto wa chekechea, Mlituambia na kutuaninisha jamaa hafai, na tutamkata tu October 25.
 
Mtazamo sahihi lakini unaweza ambiwa unaingiza ukabila. Nitamchagua EL kwa sababu anamaanisha anachokisema na yupo cdm.
 
Nina imani sana na kabila la kimaasai kwa utendaji kazi wao na kuchukua maamuzi ya haraka na yenye manufaa. Labda hii inatokana na aina ya malezi, makuzi na mafundisho wanayopewa ndani ya jamii yao yanaozingatia uwajibikaji na utoaji taarifa sahihi kwa ngazi zao za juu kwenye familia. Mgawanyo wa kazi (division of labour) na kuheshimiana (respect) ni miongoni mwa mambo ambayo jamii nyingi zinapaswa kujifunza kutoka kwa wamasai. Hawana matani wala kuchekacheka kwenye mambo ya msingi, ni wakweli na wenye msimamo usioyumba. Hata mtoto mdogo anaweza kufanya kazi ya kuchunga na kuhesabu ndama na mbuzi kwa usahihi kabisa.

Kila mtu alikunwa na sifa na uongozi wa Sokoine (rip) alipokuwa mtumishi wa serikali na waziri Mkuu, alikuwa kiboko ya uhalifu na wahalifu nchini hadi akawa tishishio hata kwa watendaji wenzake kwa speed yake ya kufanya kazi na kuchukia uzembe na wizi. Hatumchagui mtu kutokana na kabila lake tu, lakini ni kweli pia yapo makabila mengine ambayo yana idadi kubwa ya watu wavivu, waongo, wazembe, wapenda porojo na wasiothamini kazi. Wanafundishwa kucheza ngoma usiku kucha, kuoa na kuolewa mapema na kucheza bao mchana kutwa.

Lowassa ana sifa za kuchapa kazi, kuchukuwa maamuzi haraka na kuchukia umaskini, hizi ni sifa halisi (typical) za kabila za kimasai, sio za kujifunza tu darasani. Mmasai amefundishwa kuwa na mali (ng'ombe) nyingi, hivyo sishangai kusikia Lowassa kuwa tajiri ana asili navyo.

Huwenda Lowassa akafanana kiutendaji na mmasai mwenzake hayati Edward Moringe Sokoine, tena wote ni ma-edward

Moringe Sokoine hakuwahi kujinyea hata siku moja!

 
Back
Top Bottom