Lowassa na viberiti vya Chenge

Nguvu sio Pesa

JF-Expert Member
Dec 5, 2013
380
283
Basi UKAWA wakati ule wananchi wa Bariadi wakamuuliza Lowassa

."Je ni haki kuchukua viberiti vyake na kumpigia kura mgombea wa ccm.? "

Basi naye Lowassa akaomba wampatie pakiti moja ya kiberiti, akainua juu akawauliza "Je sura na chapa iliyopo juu ya pakiti moja ya kibiriti hiki ni ya nani? " Wakajibu, "Ni ya Chenge"

Lowassa akawambia, Mpeni Chenge vilivyo vyake Chenge, na ipeni UKAWA vilivyo vyake UKAWA.

Heri mtu yule atumainie umeme wa uhakika kuliko vibiriti vitakavyowasha kuni majuma mawili na kuisha kabla hata uchaguzi kufanyika. "

Wananchi wakaondoka huku lile neno likiwa limeenea mioyoni mwao, wakamsifu Mungu kwa kufungua akili na macho yao.
 

Attachments

  • 1442578825234.jpg
    1442578825234.jpg
    78 KB · Views: 141
Back
Top Bottom