IamPrince George
JF-Expert Member
- Nov 22, 2014
- 412
- 168
LOWASSA NA AJENDA YA UMASKINI!
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.
Nitakuwa mnafiki na mchoyo wa fadhila kama sitokiri kuwa awamu zote za uongozi wa nchi yetu kuanzia Mwl Nyerere hadi Dr Kikwete kuwa wamefanya mengi, makubwa na mazuri katika kupambana na umaskini wa Tanzania.
Awamu zote ki ukweli zinahitaji sifa za kipekee katika jambo hili maana lazima tukubali kila zama na kitabu chake na waliotangulia wametimiza wajibu wao na sina budi kuwapongeza sana kwa niaba ya wote wapenda ukweli
Lakini haijawahi tokea tangu tupate uhuru mgombea wa chama chochote kuuzungumzia umaskini kama Lowassa anavyo uzungumzia
Lowassa kila anapopita anaweza kusahau kusalimia lakini haachi wala hasahau kuzungumzia umaskini wa Tanzania.
Wapo wagombee ambao wanapita kila mahala wakitoa kauli mbaya kwa wenzao lakini Lowassa kwake muda wa kuuzungumzia umaskini na nini atawafanyia watanzania akiwa jukwaani hautoshi.
Lowassa anatamani usiku na mchana azungumzie njia za kumaliza umaskini wa watanzania.
KAZI NZURI ALIZOZIFANYA MONDULI KAMA MBUNGE ZINA SADIFU HAYA ANAYO YAONGEA LEO.
Lowassa watanzania wamechoka na umaskini, na ajenda yako ya kuuchukia umaskini ina wagusa watanzania wa rika zote.
Mungu akubariki baba tupo tayari kwa mchaka mchaka.
Tumegundua kuwa chuki, fitina, wivu na majungu ndivyo vilivyotufikisha hapa tulipo na hatupo tayari tena kusikiliza wanao abudu mambo hayo.
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.
Nitakuwa mnafiki na mchoyo wa fadhila kama sitokiri kuwa awamu zote za uongozi wa nchi yetu kuanzia Mwl Nyerere hadi Dr Kikwete kuwa wamefanya mengi, makubwa na mazuri katika kupambana na umaskini wa Tanzania.
Awamu zote ki ukweli zinahitaji sifa za kipekee katika jambo hili maana lazima tukubali kila zama na kitabu chake na waliotangulia wametimiza wajibu wao na sina budi kuwapongeza sana kwa niaba ya wote wapenda ukweli
Lakini haijawahi tokea tangu tupate uhuru mgombea wa chama chochote kuuzungumzia umaskini kama Lowassa anavyo uzungumzia
Lowassa kila anapopita anaweza kusahau kusalimia lakini haachi wala hasahau kuzungumzia umaskini wa Tanzania.
Wapo wagombee ambao wanapita kila mahala wakitoa kauli mbaya kwa wenzao lakini Lowassa kwake muda wa kuuzungumzia umaskini na nini atawafanyia watanzania akiwa jukwaani hautoshi.
Lowassa anatamani usiku na mchana azungumzie njia za kumaliza umaskini wa watanzania.
KAZI NZURI ALIZOZIFANYA MONDULI KAMA MBUNGE ZINA SADIFU HAYA ANAYO YAONGEA LEO.
Lowassa watanzania wamechoka na umaskini, na ajenda yako ya kuuchukia umaskini ina wagusa watanzania wa rika zote.
Mungu akubariki baba tupo tayari kwa mchaka mchaka.
Tumegundua kuwa chuki, fitina, wivu na majungu ndivyo vilivyotufikisha hapa tulipo na hatupo tayari tena kusikiliza wanao abudu mambo hayo.