Lowassa kuchunguza Ufisadi Meremeta!


In red...this voice and corruption in this republic. I will be back
 
Ndo yaleyale kuwa mchawi mpe mwanao akulelee, natuone sasa huu msemo kama unauhalisia wowote katika jamii kupitia skendo hii
 
................Kesi ya nyani unampelekea ngedere.
 

Kwa hiyo unataka kusema hata mtu akifanya ufisadi kwa miaka ishirini aliyokuwepo wizara mbalimbali, halafu akaja kufanya kazi moja vizuri, tena kukiwa na malengo ya kuukwaa urais, basi watanzania tunatakiwa tujisahaulishe ufisadi wake na kuanza kumbeba na kumtukuza... au sijakuelewa unachotaka kusema?

Eti EL ni mhanga wa kamati teule ya Mwakyembe. Inamaana Mwalimu alikua mtu wa majungu alipomtuhumu? unajifanya hujui tuhuma zake za kujimilikisha maelfu ya hectare za ranchi ya taifa akiwa Maji na Maendeleo ya Mifugo, Wizara ya ardhi unajua aliacha nini? The guy is a real estate
magnate kwa kuhodhi prime areas kwa majina ya wanafamilia.

Nigga please give us a break with your EL polishing!...
 
Mhh, hii ndo Tz, jamani mbona wanatufania usanii hivi.
 
Jamani hata sijui nini kitatokea hapo maana mtuhumiwa wa ufisadi anaongoza kamati kuchunguza ufisadi!
 

Kapewa fupa la kujisafishia ampe mwengine? hiyo ni ndoto
 
Re: Lowassa kuchunguza Ufisadi Meremeta!
jamani,Huyu Lowassa anafikiri Watanzania wana Akili ndogo kama zake??? ni bora akaachia hata huo ubunge wake, sisi tumemvumilia sana,KAMA ANA UELEWA ASJIINGIZE KWENYE KITU CHOCHOTE, AJIUZULU KAMA ROSTAM. HATA AKIENA NIGERI, SASA NI MUNGU MWENYEWE AMEINGILIA KATI, SIO JOSHUA -NIGERIA, PLEASE! NI RAHIS SANA WATANZANIA KUMSOMA, KULIKO YEYE ANAVYOFIKIRI HATUSOMA!
 
I read in Wikipedia about this guy, he was the first ever minister to resign over a fraud allegation! And now he is the one appointed to investigate alleged corruption matters in a company called Meremeta? This is soooo confusing, my mind is already spinning writing about it 🙁
I think in this move and the one revealed in the Wkilks today about Kikwete Tidbit, this current government has lost ALL credibility!
 
Hii nchi inaelekea kufa kifo cha mende kila kukicha kamati za uchunguzi zinaundwa na hakuna ata moja inayofanikiwa uchunguzi wake ukaleta manufaa zaidi ni wanakula posho na kupoteza muda badala ya kujadili jinsi ya kubolesha maisha ya watanzania,natamani nizaliwe upya nchi nyingine lakini sio tz lakini ipo siku yao wasisahau kuwa what goes around comes around.
 
Alwatan, every coin has two sides, so does human beings, kila binadamu ana mazuri yake na mabaya yake, tumeyashayajua mabaya yote ya EL, je ni kwa sababu ya mabaya hayo, hivyo ndio awe condemned in totality hata akipata chance ya kufanya mazuri ndio asipewe?.

"Once bitten, twice shy", EL ameshapata kipigo, ameshaumwa na nyoka huyo, hivyo sasa hata akiona unyasi atashituka, yeyenye si ndie mchawi mkuu wa ufisadi?, basi tumpe mtoto wetu wa ufisadi wa Maremeta ili atulelee!.
 
Huyu ndio tunaambiwa ni gamba linlosubiriwa kuvuliwa hivi karibuni. Makundi ndani ya chama yanatengeneza sinema nzuri sana, kila mtu stirling. bongo bwana!!!!!!!
 
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading"]UPADATES:

Lowassa apingwa kuchunguza Meremeta

[/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"] Send to a friend
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: createdate"] Sunday.
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]

Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa

Fidelis Butahe
BAADA ya Bunge kuikabidhi Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama inayoongozwa na Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa, jukumu la kuchunguza ufisadi wa zaidi ya Sh205.9 bilioni unaodaiwa kufanywa kupitia Kampuni ya Meremeta, wasomi na wanasiasa nchini wamepinga uamuzi huo wakidai kuwa ukweli utapindishwa.Spika wa Bunge, Anne Makinda aliamua kuwa Kamati hiyo ya Bunge ifanye uchunguzi huo kwa kuwa ndiyo inayohusika na suala hilo la Meremeta.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Mwananchi Jumapili jana, wasomi na wanasiasa hao walidai kwamba, tatizo sio suala hilo kupelekwa katika kamati hiyo, bali ni mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye walisema hawaamini kama atafanya kazi hiyo vizuri.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Sengondo Mvungi alisema, "Inakuwaje mtu anatuhumiwa kwa mambo mbalimbali halafu kamati yake inapewa jukumu la kuchunguza suala hilo zito?"
Mvungi ambaye kitaaluma ni mwanasheria alisema kuwa, ni vyema kiongozi akiwa na tuhuma za kifisadi achunguzwe kwanza kabla ya kupewa majukumu.
"Hapa ndio utaona jinsi Serikali ya Tanzania inavyougua ugonjwa wa saratani ni lazima ife…, jambo hili katika taaluma ya sheria na katiba tunaliita kuwa ni ‘ishara ya dola inayokufa'," alisema Mvungi.
Aliongeza: "Siku hizi si ajabu kuona jaji anahongwa na Takukuru… Ni wazi kuwa Serikali inayumba".
Alisisitiza kwamba, ndani ya kamati hiyo atakayejiona hawezi kufanya kazi hiyo kwa kuwa ana maslahi binafsi na Meremeta aachie ngazi mapema ili kuondoa maswali kutoka kwa wananchi, kinyume chake uchunguzi wa kamati hiyo hautakuwa na faida yoyote.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema, "Jambo linaloibuliwa na kundi jingine na kuhitaji ufumbuzi si vyema likasimamiwa na kundi linalolalamikiwa".
Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni alisema kwa kiasi kikubwa sakata la Meremeta liliibuliwa na wabunge wa upinzani, lakini anashangaa kuona suala hilo linapi pelekwa katika kundi ambalo linaweza kuwa lilihusika.
"Simhukumu Lowassa kuwa ni fisadi…, lakini wakati Serikali inaingia mkataba na kampuni hii yeye alikuwa katika Baraza la Mawaziri, sasa suala hili kurejeshwa tena kwake ni sawa?" alihoji Mbowe.
Mbowe alisema kuwa huu ni wakati wa Bunge kutambua kuwa si lazima kila Kamati iongozwe na wabunge wa CCM na kusisitiza kuwa ni vyema ikaundwa Kamati itakayoongozwa na upinzani ili kuchunguza Meremeta.
Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, alisema si lazima ufisadi wa Meremeta ukachunguzwa na Kamati ya Bunge.
"Takukuru si wapo wanaweza kufanya kazi hii…, hili ni jambo nyeti ambalo linatakiwa kuchunguzwa na watu wenye taaluma kama Takukuru, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mkuu wa Jeshi la Polisi," alisema Mbatia.
Mbatia alidai kuwa ndani ya CCM hakuna wa kumfunga mwenzake kengele. Alidai kuwa chama hicho kimekithiri kwa ufisadi na kwamba walio salama ni wachache.
"Hakika uamuzi huu utazidi kuwachanganya Watanzania, inakuwaje mtu anatuhumiwa kwa mambo fulani halafu anachaguliwa kuwa Mwenyekiti Kamati ya Bunge, halafu kamati yake inapewa jukumu hili?" Alihoji Mbatia
Mwenyekiti wa Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, alidai kuwa kamati hiyo haiwezi kuja na majibu ya kuwaridhisha Watanzania.
"Ni usanii mtupu, hata vyombo vingine vya Serikali haviwezi kulichunguza jambo hili kwa kuwa kwa muda mrefu vimekuwa vibaraka wa mafisadi, labda vivunjwe na kuundwa upya," alidai Mtikila
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Dk Benson Bana, alisema ingawa uamuzi huo wa Bunge utazua maswali mengi kwa wananchi, sheria za Tanzania zinaeleza wazi kuwa mtuhumiwa sio mkosaji.
"Mbona Lowassa anakwenda kanisani na kuchangisha mamilioni ya fedha watu hawasemi lolote?" Alihoji Bana na kuongeza:
"Watanzania wasimhukumu mtu kwa hisia, sidhani kama hata hiyo kamati yake ina watu wasafi…, Lowassa kisheria na kisiasa yuko safi ila kihisia si safi, tunatakiwa kufanyia kazi hali halisi si hisia,".
Hata hivyo, alisema pamoja na Bunge kupeleka suala hilo kwa kamati inayoongozwa na Lowassa, Serikali pia inaweza kuunda tume yake ya kuchunguza ufisadi huo.
Mhadhiri mwingine wa chuo hicho, Bashiru Ally alisema kuwa unyeti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama unaweza kufanya majibu ya uchunguzi huo yakawa wazi au kuwa siri.
"Wanaweza kusema kuna mambo hawawezi kuyasema kwa ajili ya usalama wa nchi, ila binafsi nilidhani suala hili lingepelekwa Kamati ya Nishati na Madini au ile ya Mashirika ya Umma, sijui Spika wa Bunge katumia vigezo gani kulipeleka suala hili katika kamati hii," alihoji Bashiru.

[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Mkuu Pasco, awali ya yote tungependa uchunguzi utakaotoa jibu la tatizo la mere meta, na kama ulivyosema katika mstari wa mwisho '...... hit them hard' nadhani si vema akamuonea mtu ila ukweli mtupu., kwahiyo hatuhitaji mtu wa kulipa kisasi bali atakayetupa suluhisho.

Pili, Kuingia katika kamati ya ulinzi na usalama kulikuwa na maana kubwa moja, kujenga mazingira ya kujisafisha. Kumbuka kuwa EL ni mtu anayeijua serikali vizuri na anajua kujipanga na kupanga watu wake. Hilo ndilo lilomsukuma kugombea kamati muhimu na nyeti sana ya ulinzi, usalama na mambo ya nje ili; Kwanza azuie majeraha zaidi yanayoweza kutokea na kuondoa matumaini yake ya urais, na pili kuhakikisha kuwa ana uwezo wa kujisafisha, jambo tuliloliona ameanza nalo ingawa lilizimwa haraka na wabunge.

Tatu, ni kweli mimi na wengine hatuna imani na EL. Kukosa kwetu imani kunatokana na ukweli kuwa huyu ni mtuhumiwa na hakuna chombo chochote kilichowahi kumhukumu au kumsafisha. Ukweli ubaki kuwa kuwa utuhumiwa tu unaondoa sifa zake hata ile ya kuwa mwenyekiti wa kamati ya ulinzi, usalama na mambo ya nje. Ni mtu tunayemwangalia kwa wasi wasi sana hata katika dhamira njema.
Haya ndiyo matatizo yanayotokana na kutokubali tuhuma ili uhukumiwe kwa njia halali.

Makosa ya kisiasa ni pamoja na kukubali tuhuma hata kama si za kweli kwani tuhuma hizo zitabaki bila ufafanuzi. Kama angeenda mahakamani au akubali bungeni suala la Richmond lijadiliwe ili kumhukumu au kumsafisha asingejikuta katika mazingira hayo. Mwenzake Gire mahakama imesafisha na sasa ni 'mtu safi'.

Hatujamhukumu EL ila tunamtuhumu,na ni kutokana na tuhuma hizo alizoshindwa kuzithibitisha kuwa ni za uongo, na uongozi wa serikali kushindwa kutoa kauli thabiti juu ya ushiriki wake, tunaona ni makosa makubwa kumpa kazi ya kuchunguza tuhuma ikiwa yeye mwenyewe ni mtuhumiwa. Kanuni za asili haziruhusu jambo hilo.

Ni kweli kuwa si vema kuhukumu kesi mpya kwa makosa ya zamani, lakini kanuni za asili (natural justice) zinaeleza kuwa mtu mwenye kesi ya kubaka katoto ka miaka 2 akipatikana na kesi ya kubaka mwanamke wa miaka 32 uchunguzi wa kesi utahusisha historia yake katika mambo ya ubakaji. Kwa hakika katika kundi la watu 10 yeye atakuwa mtuhumiwa mkubwa sana 'person of interest'.

Ni kwa mantiki hiyo hatujamhukumu kwa kosa la Richmond aliloshindwa kujitetea, bali tunajiuliza kama ndiye aliyesimama na kutetea Richmond kuwa ni safi akiwa PM wapi uhalali wa kutueleza mere meta asiyoijua. Kwahi hili historia inamhukumu na ukweli unabaki pale pale EL HAFAI KUCHUNGUZA tuhuma za meremeta kwasababu moja kubwa, hana 'moral authority' .
 
<b>................Kesi ya nyani unampelekea ngedere.</b>
<br />
<br />
kwa jinsi alivyo na tamaa ya kuutaka urais anaweza kumlipua swahiba wake ili ajijengee cheap popularity
 
Alwatan, hivi hatuwezi kutofautiana bila kutukanana, kuitana majina ya ajabu, or calling names?.

Noted with thanks... BTW the word NIGGA here was not meant to be derrogatory.
 

kesi ya nyati unampelekea ng'ombe. anyway ngoja tuone how he will perform. maana pia kuna usemi mchawi mpe mwana alee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…