Lowassa bana, Haya ngoja tusubiri

Lowassa bana, Haya ngoja tusubiri

Barbarosa

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2015
Posts
22,584
Reaction score
27,837
Alitoswa '95 hakukubali akafikiri mbaya wake ni Mwalimu Nyerere, ikaja 2005 pia akapigwa chini kiujanja bado akajipa moyo kwamba 2015 ni lazima awe Mgombea wa CCM piga ua, 2015 ikafika CCM wakarudia tena historia wakapiga chini mbaya yaani sasa baada ya hayo matukio yote matatu ya kupigwa chini bado amenuia na anaamini kabisa kwamba atakuwa Rais wa JMTZ.

Hapo mwishoni mwaka huu tena cha kuchekesha zaidi kwa kukitoa Chama Dola Madarakani na safari hii amerudia vitisho vyake kama alivyokuwa CCM kwamba wataandamana na kumtoa Rais wa JMTZ kwa nguvu Ikulu, hayo ni maneno ya Lowassa.

Na ukiangalia katika vitisho ambavyo amekuwa akitoa hakuna hata kimoja alichokifanikisha.

Naisubiri kwa hamu Novemba ifike, sasa sijui atakuja na lipi tena.
 
Subiria akiwa anaenda kuapishwa ndio utajua atakuja na lipi la maana.
 
Lowassa hajielewi, ikulu ataingia kwa kualikwa na rais tuuuu si vinginevyo, na ataisoma namba
 
Siku Lowassa akiapishwa mtaficha wapi nyuso zenu. Mbona Watanzania wameshaamua kuiondoa CCM.
 
Magufuli for change=money haaa haaaaa! Movemento for change hii ndo halisi.
 
Nasikia JK alipambana vikali kumpa uwaziri mkuu lowasa lakini watu na busara zao walijua lowasa uwaziri mkuu hauwez.

Haya, ndani ya muda mfup tu jamaa huyooo, njeeee
 
Yule jamaa anatakiwa avalishwe nepi sa hiv. Mana saa yoyote anaweza akaachia mambo. Duh bonge la aibu.
 
Alitoswa '95 hakukubali akafikiri mbaya wake ni Mwalimu Nyerere, ikaja 2005 pia akapigwa chini kiujanja bado akajipa moyo kwamba 2015 ni lazima awe Mgombea wa CCM piga ua, 2015 ikafika CCM wakarudia tena historia wakapiga chini mbaya yaani sasa baada ya hayo matukio yote matatu ya kupigwa chini bado amenuia na anaamini kabisa kwamba atakuwa Rais wa JMTZ.

Hapo mwishoni mwaka huu tena cha kuchekesha zaidi kwa kukitoa Chama Dola Madarakani na safari hii amerudia vitisho vyake kama alivyokuwa CCM kwamba wataandamana na kumtoa Rais wa JMTZ kwa nguvu Ikulu, hayo ni maneno ya Lowassa.

Na ukiangalia katika vitisho ambavyo amekuwa akitoa hakuna hata kimoja alichokifanikisha.

Naisubiri kwa hamu Novemba ifike, sasa sijui atakuja na lipi tena.

Usitoe mada bila utafiti. ENL aligombea 2005 kweli?
 
Lowasa hawezi kuwa rais wa TZ ila movement yake imeasaidia kupata wabunge wengi wa upinzani ingawa watakuwa hawana meno tena baada ya uchaguzi huu
 
Back
Top Bottom