Lowassa ataka mfumo wa elimu ufumuliwe

Matatizo ktk elimu ya Tanzania ni ya muda mreru sana. kama leo hii wanafunzi wengi wanakaa chini, hakuna vitabu vya kutosha, hakuna maabara, zana nyingine za kufunrishia kwa walimu hakuna. mishahara midogo kwa walimu na pia kuchelewa kulipwa madai yao mbalimbali nk Je hali hii haikuwepo kipindi Lowasa Waziri Mkuu? Hali ilikuwa hivihivi, je hakuiona? Kwa nini leo? au ndio anataka kujitengezea mazingira mazuri yq 2015 na aonekane mwema na mwenye uchungu na nchi hii? Je anadhani kwa mfano akirudi kuwa kiongozi wa nchi hii ndio atayaona tena haya? Me nasema, v2 alivyosema sio vibaya ila alipaswa kuyatekeleza alipokuwa kwenye nafasi ya kufanya hivyo, kwa hivi sasa itakuwa ni unafiki na kutafuta tu umaarufu ambao kwa sasa ni mgumu kwa vile watu tumeshamshtukia. Ajipange upya kivingine
 
Kiongozi yeyote ambaye amewahi kuiba hata shilingi moja ya UMMA, hatakiwi kufumbua mdomo wake kuwatetea wananchi. Haiwezekani unapokuwa gizani unauma, ukiwa kwenye mwanga unatetea. Huo ni unafiki
 
Reactions: Ame
Alipoulizwa kuhusu walimu na vitendea kazi, Lowassa alisisitiza shule lazima zijengwe. Kukaa benchi kama kunamfanya mtu awe na akili basi kila kiongozi angekaa benchi kama mwaka na kurudi kazini.

Ujumbe wa Lowassa ni kuwa yeye ndiye alisimamia ujenzi wa shule za kata! kampeni
 

Ndugu Ben naomba mkipita huko vijijini mchukue majina na namba za wanaopenda mabadiliko kwa ajili ya kuwasiliana nao mara kwa mara pindi mtakapokuwa mmeshapita kwa ajili ya kuhamasisha mabadiliko. huu ni wakati wa mabadiliko hatuwezi kukubali kuwa na mfumo wa waziri yule yule toka 1990 mpaka leo yeye ni kubadilisha wizara tu
 

Noted Mkuu.
 

Noted Mkuu!
 
Lowassa ni mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya bunge inahusika na usalama & mambo ya nje. Ningetaka kujua, ni kwanini huyu mwenyekiti (Lowassa) haoengii kuhusu hali ya usalama wa raia na mali zao? Ni kwanini Lowassa hajaita waandishi wa habari, kama anavyofanya kwenye hii issue ya elimu, na kutoa maoni yake juu ya mauaji wa raia wasio na hatia?

Watanzania wanaoishi mipakanani wanavamiwa kila kukicha na watu wanaodhaniwa kutoka nchi jirani, maharamia wamezagaa kila kona, na wengine wamefia Dodoma, ni lini Lowassa ataongea? Silaha za moto ni nyingi mno huku mtaani na zinatumika kwenye ujambazi, mwenyekiti wa kamati ya ulinzi anasemaje?

Lowassa ni ameshiriki sana kuanzisha shule za kata, na matokeo ya hizo shule yanaonekana sasa. Je, watanzania waendelee kuamini huyu mtu ana jipya la maana kwenye elimu?
 

Kwa kweli uliyoyasema yanahitaji kutiliwa maanani. Labda cha kuongezea hapa ni kwamba yawezekana wanapoexperience practical (real life) ya kitu ndipo wanaona madhara yake kwamba ni makubwa.

Pia yawezekana ndo wanakuwa na uelewa mzuri wa maswala hayo kwani binadamu hujifunza daima.
 
Ofcourse akae Pembeni.Kuna mdau kasema kuna vitu unaweza kuona ukiwa pembeni.Yes Namuunga mkono na ndiyo maana tunataka kumshauri na ikibidi kumshinikiza akae pembeni.Hatuko tayari taifa zima kugeuzwa Mradi wa RICHMOND

Ben Richmond unajua ya nani? yeye kama mtanzania kwenye katiba ibara ya 8 ana haki ya kuongea kuhusu nchi au kushauri hivyo siasa isipitilize wakati mwingine." KUNYATA ANYATE KINYONGA AKINYATA KICHECHE ANA VIZIA KUKU"
 
Ben Richmond unajua ya nani? yeye kama mtanzania kwenye katiba ibara ya 8 ana haki ya kuongea kuhusu nchi au kushauri hivyo siasa isipitilize wakati mwingine." KUNYATA ANYATE KINYONGA AKINYATA KICHECHE ANA VIZIA KUKU"

Simba Mangu ..... Hatuihatji kujua Richmond ni ya nani kwa sasa.. tutajua ni ya nani, wapi na nini tukisha badilisha uwezo wa kufikiri na kuja na mawazo mapya.. swali hilo la Richmond jibu lake ni lahisi sana ....ni kwamba Richmond ifanyika au ilikuwepo wakati yeye akiwa waziri mkuu na ndio maana akajiuzuru.. well done.. kwa Losawa kusema kwamba tunahitaji tume huru ya elimu maana yake ni kusema kwamba serikali yao ya CCM imepungukiwa mawazo ya kutoa suluhisho la tatizo la elimu Tanzania... Ni kwa nini kama mbuge asije na hoja ya tume huru au mswaada mpya bungeni a u anataka kutengenza ulaji mwingine wa tume huru.... serikali ina ma-expert kibao na sijui hao ma-ex[ert wa elimi ni hiviyo au nini.... kwa nini basi wasiwajaribu hata akina Rajani wa Twaweza... labda watasaidia... kama kweli serikali haina mawazo mapya yafaa sasa katiba mpya ije na kipengele cha ku-recall the whole governement for gross incompetence na kuifanya sio tu elimu bali hata secta nyngine kama afya, mazingira na uchumi kudorora... hii ni Dereliction of basic duties of the government kwa wananchi wa Tanzania maana hatukuwachagua waje kutuambia tunahitaji tume huru...

Kuna mambo yanahitaji tume huru na sio kama haya ya elimu.. Elimu inatakiwa mawazo mpya na kuwa na new policy framework Pia .. kuwapa waalimu motisha wa maana na kuajili competent people....

Akili zile zile zilizosababisha matatizo yaleyale mengi ya watanzania haziwezi kuyaondoa matatizo hayo.. tunahitaji akili mpya ili zije kutoa ufumbuzi wa matatizo yaliyosababishwa na akili za zamani...

Ndio maana tunaona wana-copy na ku-pasty sera za akina Dovutwa (Wapinzani) kwa sana bila ku-acknowledge source.. yaani ni kuibia mtindo mmoja halafu wanataka watanzania tukubali kwamba kuibia inaruhusiwa katika mtihani wa matatizo....wakati siku zote tumeambia shuleni primary kuibia hairuhusiwi na ukigunduliwa unafutiwa matokeo.. kwa nini tusiwafutie matokeo basi na tufanye mtihani mpya ili tu-pass
 
Anachosema Lowassa ni kuwa sera za chama chake kuhusu elimu zimeshindwa. It is as simple as that. Na anataka Watanzania wawaangalie wao tena kuona kama wanaweza kutengeneza walichobomoa.


Anachofanya ni kudivert attention ya big issues. Pamoja na kuwa ni kweli elimu yetu ina tatizo, ufisadi ni tatizo kubwa zaidi kuliko hilo, ufisadi unatakiwa kushughulikiwa kwanza. Will be good if he will be talking about that.
 


Lakini watu wanakuwa na doubt pale ambapo mtu anatoa maoni akiwa na ambitions huku akiacha kutolea maoni yale ya nayo mhusu zaidi kwa sasa..Tumeona mambo ya ulinzi wa raia wa nchi hii chini ya matukio mabalimbali ya ki-polisi...Hapo huyo mtu hatoi maoni anakaa kimya; then inapokuja kwenye maoni ya kinadharia ndiyo utaona anakuja na mambo lukuki tena akiwa ameshapata kuwa na nafasi ya kuyatenda lakini hakuyatenda...

Huwezi kusema utafanya ama tunapaswa kufanya hiki wakati wewe katika nafasi yako hufanyi kile unachotakiwa kufanya kwa wakati huo unapotoa maoni ya mambo mengine ambayo yako mbali zaidi. Mchagua jembe si mkulima so to speak!
 

Ninachoipenda JF ni watu kuwa na reference pindi mambo yanapotokea ndivyosivyo kama yanayojiri sasa kumbe wale walalamikao ndio walioasisi
 
Anayosema EL ni strategy ya kutaka kurudi kwa nguvu wakati wananchi tunafahamu kwamba alikuwa na nafasi kubwa sana ya kuhakikisha hayo yote yanatendeka pindi alipokuwa PM, anaposema sasa hivi ni kama janja ya nyani tu kwa kuwa anajua tumesahau
 
Tume ya nini?
Mwenye sera za Elimu za CUF,NCCR na CHADEMA aweke humu tuzione au azione najua anapita humu au vibaraka wake wanapita watampelekea maana lile la Elimu BURE kasha lichukua.
 
Anaota uras huyo, anajitafna tafna na kujing'ata meno tuone anahuruma nasisi. Mbona hakuizuia Richmond akaacha ijipenyeze bila

kuchukua hatua mpaka bunge likaingilia? Mwizi ni mwizi tu hata kama aseme yeye hahusiki lakini yeye si alikuwa kolongo la kupitia huo uchafu wa Richmond!!!!
 
Lowassa acha unafiki, amekuwa waziri miaka Ishirini mitatu ikiwa waziri mkuu, alifanya nini kwa wananchi asimame na aseme ili tujue nje ya hapo anataka simpathy vote. Atueleza kwanza yeye kama mtumshi wa umma aliwezaje kuapata Nyumba Mbili pale mahando, na zile za arusha mbezi beach, kampuni za Alpha brand school, cleaning and supper dealer wa Voda. Mr Lowassa we are not stupid as you think, and dont event try to tell us is your son we know the boy ............ AJisafishe kwa haya machache ndio aanze hii desparations zake kutafuta urais at any cost.
 


Mh Lowasa ameongea mambo ya kawaida sana ambayo hata hapa maskani huwa tunayaongea, halafu nastareheshwa na namna alivyoyatamka kana kwamba hajawahi kuwa MWONGOZAJI wa harakati za ukombozi wa Mtanzania.
Kwa kuongezea ni kuwa WAANDISHI KANJANJA, narudia, WAANDISHI KANJANJA wa hapa TANZANIA wanampamba sana huyu Mh Lowasa, laiti angekuwa ni keki basi ingekuwa na ngazi tano kama sio saba, lakini ikumbukwe kuwa hata kama keki itapambwa na kulembwa namna gani, mwisho wa siku lazima iliwe na vijiunga unga vyake vitaanguka sakafuni. Nashauri waandishi makini waachane na hawa viongozi zilipendwa, wafukue talanta ambazo yeye mwenyewe Lowasa anazitaja kuwa "Tanzania inao wasomi mahiri", hii inamaanisha Waandishi makini wawatafute hawa wasomi mahiri wanaosifiwa na Lowasa, kisha waandishi watuelimishe kuhusu umahiri wa wasomi hao, ili tuwafahamu na kisha tuwakabidhi nafasi za kisiasa na kiutendaji ili tuikwamue nchi yetu toka hapa ilipozamishwa KWA MAKUSUDI na ufisadi wa CCM ambao kwa kiasi kikubwa umewapofua macho MAKANJANJA kiasi kwamba fikra zao haziendi mbali na upeo wa shida ya tumbo almaarufu NJAA.
 
niliwahi kumsikia lowassa akiponda dhana nzima ya kilimo kwanza....sasa ameponda elimu
 

Jamani! jamani! Jamani!
Huyu edo inaelekea ni msahaulifu sana. Hakumbuki jinsi alivyokuwa anaipiga vita HakiElimu kwa kuikubusha serikali masuala haya ya ubovu wa elimu na misingi yake na akawashtaki kwa rais dhaifu JK! Leo anajitokeza kupiga debe yale ambayo aliwapinga Haki Elimu.

Fisadi edo alishindwa kuuona udhaifu huu akiwa madarakani lakini anauona akiwa nje maana yake ni kuwa hafai kuwa kiongozi kwa kuwa anapokuwa madarakani anakuwa kipofu na kukosa vission.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…