Ni swali tu,
Kwanza tunafahamu kuwa Lowasa hana mapenzi ya dhati na chama chochote cha upinzani, na ni kwasababu hiyo upinzani ulikuwepo miaka zaidi ya ishirini lakini hajawahi hata kuufikiria. Aliipenda CCM ambayo leo anaitukana. Alikuwa FISADI, leo msafi.
Hana na hakuwahi kutaka kuleta ukombozi wa kweli wa mtanzania. Sera za CHADEMA na vyama vingine vya upinzani daima zilijipambanua ukombozi wa mtanzania. Kuiondoa CCM madarakani ilikuwa sera za vyama hivyo. Je, asingekatwa jina angeimba sera gani leo? Ni unafiki tu na kujiaibisha mtu mzima kama yeye. Juzi tu alikuwa kijani kwa nguvu zote, leo eti magwanda, atuaminishe eti ana nia thabiti ya kuiondoa CCM madarakani.
Nasikitika CHADEMA na vyama vingine vya upinzani vilijengwa kwa miaka 20, kwa taabu kubwa, lakini Lowasa pamoja na timu yake wataiua ndani ya mwaka moja. Hata kama Ikulu ataingia, jambo ambalo binafsi naona hadi muujiza uwepo.
Lowasa mapenzi yake ni Ikulu tu, ambayo anatumia nguvu zote iwezekanazo ili aipate. Lowasa hana nia thabiti ya kuiondoa CCM madarakani, hana mapenzi ya dhati kwa UKAWA. Kwake yeye UKAWA ni kama ngazi tu, nia yake ni Urais, na asipoupata?
Ila amefanikiwa kuzizika siasa za kweli za upinzani, walio na uchungu na Nchi hii.
Zimebaki siasa feki kama bidhaa za kichina.
Kwanza tunafahamu kuwa Lowasa hana mapenzi ya dhati na chama chochote cha upinzani, na ni kwasababu hiyo upinzani ulikuwepo miaka zaidi ya ishirini lakini hajawahi hata kuufikiria. Aliipenda CCM ambayo leo anaitukana. Alikuwa FISADI, leo msafi.
Hana na hakuwahi kutaka kuleta ukombozi wa kweli wa mtanzania. Sera za CHADEMA na vyama vingine vya upinzani daima zilijipambanua ukombozi wa mtanzania. Kuiondoa CCM madarakani ilikuwa sera za vyama hivyo. Je, asingekatwa jina angeimba sera gani leo? Ni unafiki tu na kujiaibisha mtu mzima kama yeye. Juzi tu alikuwa kijani kwa nguvu zote, leo eti magwanda, atuaminishe eti ana nia thabiti ya kuiondoa CCM madarakani.
Nasikitika CHADEMA na vyama vingine vya upinzani vilijengwa kwa miaka 20, kwa taabu kubwa, lakini Lowasa pamoja na timu yake wataiua ndani ya mwaka moja. Hata kama Ikulu ataingia, jambo ambalo binafsi naona hadi muujiza uwepo.
Lowasa mapenzi yake ni Ikulu tu, ambayo anatumia nguvu zote iwezekanazo ili aipate. Lowasa hana nia thabiti ya kuiondoa CCM madarakani, hana mapenzi ya dhati kwa UKAWA. Kwake yeye UKAWA ni kama ngazi tu, nia yake ni Urais, na asipoupata?
Ila amefanikiwa kuzizika siasa za kweli za upinzani, walio na uchungu na Nchi hii.
Zimebaki siasa feki kama bidhaa za kichina.