Sipingani na nia yake ya kutaka kuingia Ikulu kwani ni haki yake ya kikatiba, lakini najiuliza tu kwa muda wote alipokuwa mbunge wa Monduli, kwa nafasi zote alizotumikia serikalini kuna cha pekee ambacho wananchi wa Monduli wanaweza kujivunia nayo? Umaskini anaotaka kuumaliza Tanzania atakapokuwa Rais, amejitahidi kiasi gani kuumaliza kwa wapiga kura wake wa Monduli?
Maswali yanaweza kuwa mengi, ila inafaa kusoma katikati ya mistari. Kama kwa miaka yote aliyokuwa Mbunge wa Monduli hakuonesha jitihada za kumaliza umaskini wa wapiga kura wake wa Monduli, ndiyo tujiaminishe kuwa kwa miaka kumi atakayokuwa Rais atafuta umaskini wa Tanzania?
Baadhi ya viashiria ya umaskini wa hali ya juu wa jimbo la Monduli ni tatizo la maji. Sijasikia jitihada zake kumaliza tatizo hilo, wala kulipatia ufumbuzi wa kudumu. Alikuwa hata waziri wa maji, lakini pita leo barabara ya Arusha -Karatu, utaona akina mama na punda wakisaka maji kwa umbali mrefu.
Nguvu kubwa ya hela inayotumika isingehitajika ikiwa kuna kitu cha wazi alichofanya huko jimboni kwake.
Kama kuna anayefahamu hatua kwa hatua jinsi alivyowatoa wapiga kura wake kutoka dimbwi la umaskini anaweza kulisemea, vinginevyo ni hadithi ile ile ya kuigeuza Kigoma kuwa Dubai, ambazo hadi leo ni ndoto za alinacha.
Maswali yanaweza kuwa mengi, ila inafaa kusoma katikati ya mistari. Kama kwa miaka yote aliyokuwa Mbunge wa Monduli hakuonesha jitihada za kumaliza umaskini wa wapiga kura wake wa Monduli, ndiyo tujiaminishe kuwa kwa miaka kumi atakayokuwa Rais atafuta umaskini wa Tanzania?
Baadhi ya viashiria ya umaskini wa hali ya juu wa jimbo la Monduli ni tatizo la maji. Sijasikia jitihada zake kumaliza tatizo hilo, wala kulipatia ufumbuzi wa kudumu. Alikuwa hata waziri wa maji, lakini pita leo barabara ya Arusha -Karatu, utaona akina mama na punda wakisaka maji kwa umbali mrefu.
Nguvu kubwa ya hela inayotumika isingehitajika ikiwa kuna kitu cha wazi alichofanya huko jimboni kwake.
Kama kuna anayefahamu hatua kwa hatua jinsi alivyowatoa wapiga kura wake kutoka dimbwi la umaskini anaweza kulisemea, vinginevyo ni hadithi ile ile ya kuigeuza Kigoma kuwa Dubai, ambazo hadi leo ni ndoto za alinacha.