rahma suleiman
Member
- Jan 16, 2014
- 28
- 10
kwa mara ya kwanza vijana wa ccm wamepata ujasiri na kusema ya moyoni juu ya vitendo vya rushwa iliyokithiri kwa baadhi ya viongozi ndani ya chama hicho. Ilikuwa kawaida kwa wengine tusio ndani ya chama hicho tukihoji rushwa za nje nje za kiongozi kwa viongozi wa dini, viongozi wa chama chake na wananchi wa kawaida kuonekana tunampaka matope maana sisi tu wapinzani tu lakini haya ya kina paul makonda yamefungua mapya. Wapo ambao bado wanafanya kila juhudi kumsafisha kiongozi huyu ama kwa kuwa ni wanufaika wa rushwa anazozitoa ama kwa kuahidiwa nafasi mbalimbali lakini naamn kwenye nafsi zao wanajua ukweli kwamba Lowasa ni fisadi na fedha anazitoa ni matokeo ya wizi mkubwa alioufanya akiwa kiongozi mkubwa wa serikali. ukitathmni jumla fedha zote alizotoa sasa ambazo si chini ya Bil 1 na ushee lazima upate ukakasi kuamin kwamba fedha hizo anazomwaga alizipata kihalali. Hii ni kwa sababu mishahara ya wabunge inafahamika na mishahara ya mawaziri inafahamika kwa hivyo hata kama asingetumia hata senti moja ya mishahara yake bado asingeweza kuwa na fedha za kumwaga kwa wingi na laana kama hivi sasa. KIle anachokidai safari ya matumaini ni machakato wa kihuni na wa kifisadi unaotegemea fedha ili kumwezesha kushinda nafasi ya urais. Lowasa hatambui kuwa nia ya dhati, utu wema na uzalendo ndio sifa kuu za kumfanya mtu kuwa kiongozi bora kwani kama utajiri na uwezo wa kuhonga ndio ingekuwa kupata urais basi matajr kama Bilget ndo wangekuwa marais. Ni mda sahih kwa CCm na vyama vingine kuziba milango kwa mafisadi wote kupata nafasi katika serikali na kuwaachia watu wasafi kugombea nafasi hzo. NAAMINI ANGUKO LA LOWASA ITAKUWA NI FUNDISHO KWA MAFISADI WOTE NA VIBARAKA WAO. 2015 BILA RUSHWA INAWEZEKANA.