Love bite - black chocolate

Kasie

Platinum Member
Joined
Dec 29, 2013
Posts
22,801
Reaction score
43,177
Habari za jioni,

Mng'ato wa mapenzi - kung'atwa kwa kupenda - mapenzi ya kung'atana - alama ya kuonesha kuwa umetoka kuchubwika n.k. n.k.

Japo ni mambo ya kizungu inatuhusu maana tumeiiga na sidhani kama asili yake ni huku afrika. Nachelea kusema si kila kitu kinafaa kuiga maana yaliyomkuta bidada mmoja wa mjengo flani hamu hana. Huyo dada tunafahamiana ile ya kusalimiana tuu na si zaidi ya hapo. Sasa tulikutana saluni week end hii na akawa anamsimulia huyo mdada mwenye saluni yaliyomsibu kama kawaida masikio hayana kufuli nikiwa nasubiri zamu yangu kunyolewa nikajikuta nasikiliza issue yote.

Bidada akawa anasimulia ijumaa jioni walitoka out na bwana ake hadi usiku mnene jamaa akamrudisha bidada kwake. Kama kawaida ya wapenzi jamaa akaingia kupiga viwili ili nae arudi kwake. Baada ya libeneke kuisha jamaa akamwambia nataka nikuachie love bite bidada akaelewa ni romantic kiss hehehee... weeh anasema nusu azimie. Maana jamaa alikuwa anamnyonya shingoni kwa pembeni kumbuka hapo pamepita mshipa mkubwa unaosambaza damu mwilini hivo bidada alilegea ila jamaa akawa anaongeza nguvu na kung'ata kabisa na meno yeeeeh si ndo bidada akaona mapigo ya moyo yanamtoka na roho inataka muacha huku anajiona.

Jamaa alimnyonya kwa dakika 25 bila kumuachia na hapo aliacha baada ya bidada kuonesha dalili anazimia kama vile kukoroma na kutapatapa.

Jamaa akamwambia kesho nakuja kurudia hadi love bite ionekane. Usiku ule hakumjibu kitu akafunga mlango wake akalala.

Kulipokucha bidada akazima simu maana alihisi jamaa angempigia na angerudi kumnyonya damu, sasa kilichonivunja mbavu kwenye habari hii ni kuwa bidada ni mweusi kama mpoki au lupita nyong'o. Sasa hebu jiulize hizi love bite kwa watu weusi kama Kasie hapa au mpoki si kutafuta kutoana damu kama si kuachiana kidonda maana alama haionekani. Au kidonda ndo love bite yenyewe......? Sasa mbona love yenyewe inasababisha maumivu? Maana kidonda lazima kiume au kung'atwa kunauma au mie sielewi.

Nlichokizoea mie love bite inaonekana kirahisi kwa watu weupe au wazungu wala mtu hutumii nguvu ni vaap love bite hiyoo shingo yote utasema mtu kuvaa cheni ya mbwa heheee

Haya ni mashokolo mageni kwa Kasie sijui ndo uzee.
Hapo hapo huyo mdada wa saluni akaunganisha nyie mapenzi hayana umri, akasema kuna mama mmoja ni mteja wake alienda saluni kwake amfanyie massage yaani huyo mama ni wa miaka 50 hadi 55 yaani alikuwa na love bite shingo yote. Huyo dada wa saluni akabaki anakodoa macho daah hadi bibi kama huyu bado anachubwika ki love bite.

Tukaishia kucheka, nikajikuta nawaza kwa sauti hivi siku Dr. Mengi anatoka kwenye luninga na love bite kibao shingoni si watu watacheka. ... of course atakuwa kaweka na Jackline ila daah mtandio na pull neck vitamhusu looh.

Ushawahi kupata love bite weye? Ulipigwa chata ya wapi? Shingoni? Mguuni? Mkononi? Pajani? .....???

Kasie bin popo.
 
Indeed mapenzi na manjonjo yake hayana umri.

Lakini nimeshangazwa na huyo jamaa alivyoamua kumkula shingo huyo bidada.

Uzoefu wangu na nijuavyo mimi Love Bite normally inatokea spontaneously in the process ya kugegedana....mkiwa kwenye dimbwi la kupeana maraha mnajikuta mmeishia kuwekana maalama kama hizo love bites n.k n.k
 
Hahahahaha kasinde umenichekesha htr hyo atakuwa dungdunga au vampire hah!!nakumbuka cku moja bae wngu akaniambia natka nikukic shingon mi nikajua just a kiss,akaanza taratibu nikawa nackilizia utamu lol mara kaanza kukaza mdomo mara meno yapo juu ya shingo weee!!!alikula kofi mpka 5 finger zikatokea mana nilihic anataka kunikausha damu!!!!
 
Huyo mwanafunzi bado,dkk 25 unaweka lovebite au unanyonya damu?,hata vampires hawatumii mda kunyonya damu khaaaa
Lovebite uwe mweupe uwe mweusi inaonekana mbona as long as jamaa awe mtaalamu,ila kama ndo upate vampire unalo, lazma akutegue mshipa wa damu
 

Pole
 


Pole sana best....ila huyo bae wako atakuwa mjukuu wa vampire huyo. Love bite kimsingi utakachosikia ni raha tuuuu baasi. Anahitaji orientation aisee. Mara nyingi mtu unakuja kushtuliwa na alama aidha wakati unajitazama kwenye kioo au mtu mwingine kukustua.

Huo mchezo hauhitaji hasira na kuanza kuumizana. Ha ha ha
 
Huyo jamaa atakuwa vampire/ zombie , love bite zaidi ya dakika 10
 

Asante mkuu kibaya ni kuwa hatukuwA deep kwny mahabati so it means akili yngu ilikuwa normal mi nakAjua kiss ya kawaida heh kumbe kachange gear angani!!!hahahHaha mpka leo naogopa sana hyo kitu!!!
 

Nadhani atakapoamua kurudi basi abebe na kopo la rangi nyekundu kabisa maana kwa kumnyonya mwenzake kiasi akaelekea kupoteza fahamu kwa dakika hizo ni zaidi ya hatari haswaaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…