commonmwananchi
JF-Expert Member
- Mar 12, 2011
- 3,377
- 1,952
Haiwi haiwi mwisho imekuwa.
Ni nape nnauye yule katibu mwenezi wa ccm taifa.ambae amekuwa akipinga ufisadi ndani ya chama chake kila siku majukwaani, hatimae amejitokeza rasmi huko arumeru na kumtangaza rasmi Bw sioi sumari kama mgombea wa chama chake kwa nafasi ya ubunge jimboni humo.
Hatua hii ni sawa na kukubali Rasmi kupoteza mechi baina yake dhidi ya mafisadi,kwani mbali ya sioi kuwa ni mkwe wa hasimu mkuu wa Nape Bw Lowassa lakini pia mchakato mzima wa uteuzi wake ulighubikwa na ufisadi mkubwa wa rushwa na kupelekea malalamiko makubwa ndani ya chama chao.
Lakini pia imeenda mbali zaidi na kufikia hatua hata ya baadhi ya wana ccm kutiwa mbaroni kwa tuhuma za rushwa wakihusishwa na Sioi huyuhuyu.
Kitendo cha Nape kutokea na kuwa bega kwa bega na maamuzi hayo ni sawa na kusalimu amri kwa ufisadi sawa na kupoteza mechi kwa kulambwa magoli mawili kwa bila.
Ni nape nnauye yule katibu mwenezi wa ccm taifa.ambae amekuwa akipinga ufisadi ndani ya chama chake kila siku majukwaani, hatimae amejitokeza rasmi huko arumeru na kumtangaza rasmi Bw sioi sumari kama mgombea wa chama chake kwa nafasi ya ubunge jimboni humo.
Hatua hii ni sawa na kukubali Rasmi kupoteza mechi baina yake dhidi ya mafisadi,kwani mbali ya sioi kuwa ni mkwe wa hasimu mkuu wa Nape Bw Lowassa lakini pia mchakato mzima wa uteuzi wake ulighubikwa na ufisadi mkubwa wa rushwa na kupelekea malalamiko makubwa ndani ya chama chao.
Lakini pia imeenda mbali zaidi na kufikia hatua hata ya baadhi ya wana ccm kutiwa mbaroni kwa tuhuma za rushwa wakihusishwa na Sioi huyuhuyu.
Kitendo cha Nape kutokea na kuwa bega kwa bega na maamuzi hayo ni sawa na kusalimu amri kwa ufisadi sawa na kupoteza mechi kwa kulambwa magoli mawili kwa bila.