Live on TBC: Sherehe za kuwasha mwenge

Live on TBC: Sherehe za kuwasha mwenge

Tunaitaji mabadilko, matumizi kama hayo yasiyoyaleta tija lazima yapungue
 
watoto.jpg The Govt prioties is Sherehe na Siyo Matatizo ya Msingi! jk_torch.jpg
 
Hivi nyie ndo mnagundua sasa hivi kuwa mbio za mwenge ni chaneli za watu kutafuna pesa za walalahoi..!?
Mi tangu nasoma miaka hiyo tulikuwa tunalazimishwa shuleni kupeleka "mchango wa mafuta ya mwenge" sh. 50. Yaani nikipewa hiyo sh. 50 nyumbani ilikuwa ni bora niitumie kula mihogo ya kuchemsha na kachumbari wakati wa mapumziko. Sikuwahi kuchangia mwenge tangu nizaliwe. Na nilikuwa naingia kwenye mgogoro mkubwa sana na walimu kuhusu mchango wa mwenge.
 
Enzi za mwl.mwenge ulikuwa unamaaana sana,kwa sababu baada ya mwenge kupita ripoti ya kila wilaya ilikuwa inaandikwa na kukabidhiwa kwa rais baada ya hapo watu watendaji wabovu wanatimuliwa kazi na wengine kushushwa vyeo,lakini siku hizi ni kuwasha torch na kuzima na kiongozi wa mwenge kupata deal la kutoka kimaisha hakuna issue siku hizi ni upuuzi mtupu!!!!!!!!!!!!!!
 
Watoto wetu wanaosoma St.Kayumba hawajui umuhimu wa shule ndio maana muda huu wa masomo wako uwanjani kupigwa na jua kuwasha mwenge, ila watoto wao wanaosoma St. english medium wao ndio wanajua umuhimu wa shule. Hii ni moja ya sera za chama kuwatoa watoto madarasani kipindi cha masomo na kuwapeleka uwanjani ama kuwapanga barabarani kushangilia mwenge, mikutano ya hadhara nk nk nk nk nk....

"SOON VERY SOON VUA GAMBA VAA GWANDA ITAELEWEKA"
 
Ipo siku nitalivizia hilo likibatari nilimwagie maji,huu ni ujinga kuendekeza mambo yanayoigharimu nchi,yani msururu wa magari karibu mia mafuta wanapata wapi?na bado maambukizi ya VVU yanayotokana na shughuli za mwenge ni makubwa mno huu ni mwendelezo wa fikra za kizee za ccm,hakuna utaifa hapo ni mbinu za kujenga chama zilizopitwa na wakati
 
Huko watu wanaenda kuongeza maambukizi ya vvu tu!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom