Lissu: Samia Suluhu Hassan has finally revealed her true colors

Samia kadondoshea tone la petrol kwenye majivu ya moto - akae tayari tayari!

Akiwasikiliza wahafidhina ndani ya chama chake, anaweza kuwa na wakati mgumu sana wa kuendesha nchi kwani atahujumiwa na makundi yanayousaka urais 2025 ndani ya chama chake, atapigwa pressure na upinzani na wanaharakati watampatisha taabu sana.
 
La nakusikitikia kiongozi Kama bado unayaamini wanayotamka wanna siasa.
 
Kila mtu anampima kutoka kwenye angle yako na atatoa maoni yake, tatizo nini? Wanasiasa wanata mikutano, wamekataliwa ulitaka wamsifu kwa kumtema Chalamila? Au ulitaka wamsufu kwa kumuondoa Jeri James kutoka UVCCM?
Nadhani Lissu akikuamuru kufa utakufa
 
Let's join hands, feet, bodies, and brains in fighting for the constitutional reform. We shouldn't retreat or surrender. "Ninapayuka tena: KATIBA MPYA!!!?"
 
Kila mtu anampima kutoka kwenye angle yako na atatoa maoni yake, tatizo nini? Wanasiasa wanata mikutano, wamekataliwa ulitaka wamsifu kwa kumtema Chalamila? Au ulitaka wamsufu kwa kumuondoa Jeri James kutoka UVCCM?

Shida ya wana siasa wanalazimisha sana wote tuwafuate nyuma kwenye hoja zao za kutaka dola. Wananchi walio wengi wanataka maendeleo. Wanataka maisha yenye amani na uhakika wa kupata riziki zao.
Wanataka kulipwa milion 12 kwa mwezi kama wabunge. Sio kukimbizana na polisi kama wezi wa mifukoni
 
ficha upuuzi wako basi kidogo
 
hahahahaha mwambieni TL, Mama hawezi kuongoza kwa kumsikiliza Lissu anataka nini.. Mama ni Rais wa watanzania wote sio CDM wala CCM au Chauma...anaongoza kwa maslahi ya wengi..

Mwambieni Lissu tulimuonea sana huruma alivyotandikwa risasi pale dodoma kiukweli haikuwa sawa na wahusika wanapaswa kukamatwa kwa maana ya uchunguzi huru ufanyike....lakini kuwa muhanga wa serikali iliyopita hakutufanyi tumkubalie kila kitu bado tutapima mawazo na fikra zake kama zinatufaa watanzania..

Katiba kila mtu anaitaka kwa maslahi ya Taifa sio vyama vya siasa na wanasiasa ...wakati ukifika wananchi wote tutaongea lugha moja na kuidai hiyo katiba sio wakati huu wa wanasiasa kwa maslahi yao ya kurahisishiwa njia ya ikulu
 
Kueka matumaini kwa mtu binafsi ni kama vile kucheza kamari. Nadhani wapinzani wajipange kupigania katiba au mabadiliko ya sheria kwa uwezo wao wote. Hii sio kupiga soga tuu kwenye vyombo vya habari nadhani waanzie vijijini kwa wananchi wa kawaida wafahamu umuhimu wake kwanza.

Watanzania wengi bado wanafikiria mabadiliko ya sheria ni kwa ajili ya uchaguzi au ni tatizo la kisiasa pekee. Nataka nitofautiane na hili, mabadiliko haya ni ya kitaifa na siasa ni moja ya sehemu ya mabadiliko hayo.

Sheria zetu ni mbovu kupita kiasi zinahitaji upgrade ya hali ya juu, pengine sio upgrade ni complete new install ili taifa lisonge mbele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…