Countrywide
JF-Expert Member
- Mar 2, 2015
- 18,173
- 27,223
Habari wanaJF,
Leo kuna jambo nataka kulizungumzia, issue ya matokeo ninapenda kumpa pole Lissu.
Lakini kuna hili jambo lingine ambalo sijalipenda hata kidogo. Lissu kwa sasa anaishi kwenye ubalozi wa ujerumani kwa kile alichosema kutishiwa maisha yake.
Yupo sahihi kwa hilo, lakini akumbuke sisi tulikuwa tunamtegemea kiongozi wetu huyu kutuvusha na sio kukata tamaa.
Ninasema hayo kwa kuwa Lissu alisema mwenyewe kuwa yupo tayari kwa lolote na haogopi tena vitisho, iweje leo aseme ametishiwa hivyo kuamua kwenda kujihifadhi ubalozini?
Na ameenda mbali kwa kusema muda si mrefu anarudi ubelgiji kwa kuwa huku usalama wake ni mdogo.
Lissu kumbuka sisi wafuasi wako tulisema "Lissu sio Lowassa" tukimaanisha wewe sio muoga na upo tayari kwa lolote na ndio maana hata ulipofunga barabara siku ile kwenye kampeni tulishangilia sana kwa kukuona shujaa, sasa leo imekuwaje tena?
Ok, pia umekua ukisema kuwa wananchi wananyanyasika sana wengine wanakufa kwa uonevu, sasa na sisi wananchi tunaoumizwa tukimbilie wapi?? Tupe mbinu, usijiokoe mwenyewe tu.
Wote tunaonyanyasika na sisi tuje tuishi huko ubalozini?
Wanachadema bado tunakudai sana, kwa kuwa uliahidi kutuvusha.
Nawasilisha
Leo kuna jambo nataka kulizungumzia, issue ya matokeo ninapenda kumpa pole Lissu.
Lakini kuna hili jambo lingine ambalo sijalipenda hata kidogo. Lissu kwa sasa anaishi kwenye ubalozi wa ujerumani kwa kile alichosema kutishiwa maisha yake.
Yupo sahihi kwa hilo, lakini akumbuke sisi tulikuwa tunamtegemea kiongozi wetu huyu kutuvusha na sio kukata tamaa.
Ninasema hayo kwa kuwa Lissu alisema mwenyewe kuwa yupo tayari kwa lolote na haogopi tena vitisho, iweje leo aseme ametishiwa hivyo kuamua kwenda kujihifadhi ubalozini?
Na ameenda mbali kwa kusema muda si mrefu anarudi ubelgiji kwa kuwa huku usalama wake ni mdogo.
Lissu kumbuka sisi wafuasi wako tulisema "Lissu sio Lowassa" tukimaanisha wewe sio muoga na upo tayari kwa lolote na ndio maana hata ulipofunga barabara siku ile kwenye kampeni tulishangilia sana kwa kukuona shujaa, sasa leo imekuwaje tena?
Ok, pia umekua ukisema kuwa wananchi wananyanyasika sana wengine wanakufa kwa uonevu, sasa na sisi wananchi tunaoumizwa tukimbilie wapi?? Tupe mbinu, usijiokoe mwenyewe tu.
Wote tunaonyanyasika na sisi tuje tuishi huko ubalozini?
Wanachadema bado tunakudai sana, kwa kuwa uliahidi kutuvusha.
Nawasilisha