Uchaguzi 2020 Lissu, je wananchi wa vijijini watazitumia hizo reli unazotaka kuzijenga Dar?

Kunatakiwa kuwe na BALANCE kati ya maendeleo ya watu na maendeleo ya vitu.

Pia maendeleo ya vitu yazingatie mahitaji ya watu, na yawe shirikishi.

Kwa mfano, huwezi kuwajengea wananchi wa Chato uwanja wa ndege wa kimataifa wakati hitaji lao ni maji, zahanati, madawati,na pembejeo.

Huwezi kuleta maendeleo ya vitu huku ukinyima wananchi / walipakodi haki zao za msingi kwa mfano, kutowapandisha watumishi wa umma mishahara, kuwadhulumu wakulima korosho zao, kuwatoza wanawake wanaojifungua ada ya kujifungua, kuwalazimisha wamachinga kununua vitambulisho, na dhuluma nyingine nyingi.

Zaidi kuna umuhimu wa kuwapa wananchi mamlaka makubwa zaidi ya waliyonayo sasa hivi ktk kuamua mambo yao ya kimaendeleo. Utaratibu uliopo umempa Raisi madaraka makubwa kupita kiasi na kuwafanya wananchi wawe ombaomba kwa Raisi.
Nakubaliana na wewe kuwa maendeleo ya vitu yaendane na mahitaji ya watu kwa maendeleo yao.

Sikubaliani na wewe ya hiyo mifano uliyotoa kwa kuwa yanakisi mtazamo wako kisiasa zaidi kuliko kiuchumi/maendeleo.

Miradi yote iliyotekelezwa au inaendelea kutekelezwa na Serikali iko kwenye Ilani ya Uchaguzi Mkuu, 2015 ya CCM. Ni Ilani iliyokipa chama ridhaa ya kuunda Serikali. Ni imani kuwa Ilani hiyo, ilivyoboreshwa kwenye Ilani ya Uchaguxi Mkuu, 2020 itakipa CCM ushindi mnono ukilinganisha na Ilani ya CHADEMA ya Uhuru, Haki na Maendeleo ya Watu.
 
Kila sehemu inamahitaji yake muhimu Kama dar hitaji lake ni hilo linatakiwa lifanywe wakati na wananchi wanapewa welfare hata mfanyabiashara akiwa anainua uchumi wa biashara yake hatakiwa asiwajali wafanyakazi wake, na huko kijijini pia Kuna mahitaji yao muhimu yafanywe huku wanakijiji nawatengewa maeneo ya kilimo na kufuga, maji, umeme, na mahitaji ya muhimu ya eneo husika ili wafurahi na kula mema ya nchi hayo ndo maendeleo ya watu, yaani Kuna kazi za serikali ambazo ni lazima huku unaangalia watu Kama wanamudu kupata pato lililowekwa kimataifa.
Mnaongelea maendeleo ya watu kinadharia tu. Km hali ya mkulima kimapato itabadilika bila kuwa na soko? Je, soko ni majirani zake tu? Hivyo basi, huyu mkulima aondokane na umaskini wa kipato lazima kuwepo na miundombinu imara na bora ya hifadhi ya mazao na usafirishaji (reli, barabara, majini na angani) mazao yaweze kuwafikia walaji kwa wakati na ubora uleule.
 
Ukiniambia T. Lissu baada ya kulipata hili ataeleza nitakuelewa.

Lakini hapo awali hakuthubutu kabisa kulizungumzia hili kwa Mlengo huu.

1.Kuhusu Ujenzi wa miundo mbinu T.Lissu bado yupo gizani.

CHADEMA tusubiri atakae kuja Labda atatufaa ila sio huyu.

..tatizo la ccm ni kupotosha.

..sasa wewe ni victim wa upotoshaji wa ccm.

..miundombinu anayoipinga TL ni ile ambayo ina harufu ya ufisadi, na isiyowagusa wananchi.

..kwa mfano, airport ya Chato, wananchi wa Chato waliulizwa kama wanahitaji uwanja wa ndege wakasema hapana.

..lingine ni ununuzi wa ndege na kuifufua atcl. Ukweli ni kwamba mradi huo ni wa hasara. Pia tayari kulikuwa na mashirika ya ndege yanayoleta watalii toka nje, na mengine yanayosafirisha abiria wa ndani.

..Trillions of shillings zilizotumika kununua ndege na nyingine kuingia ktk mifuko ya wakubwa zingeweza kuanzisha miradi inayogusa wananchi wengi zaidi hapa nchini.

..Again, lazima kuwe na balance kati ya maendeleo ya vitu na maendeleo ya watu. Maendeleo ya vitu lazima yawalenge na yawanufaishe WATU.
 
Leo Mh Tundu Lissu kawaambia Watanzania na waandish wa Habar kua Serikali yake yeye italipanua jiji la Dar na kuakikisha Anaongeza usafiri wa Reli za umeme kwani Kujenga Mabara Bara tu Haitosh pia Anaongeza Mabas ya Mwendokas na kuupanua Mkoa wa Dar

Pia kasema Daresalam nzima Haina sehem Ambayo watu Wanaweza kwenda kupumzika na kusema kua serikal yake lazima itafanya ayo

Tundu Lissu amekuwa akipiga kelele juu ya Miundombinu inayo jengwa Dar na kusema kua vitu ivyo havimfaidish mtu Wa kijijin na kusema kua je Watu watakula Madaraja? Au watakula ndege. Na mimi pia ningependa kumuuliza izo Treni atazo jenga zitamsaidia Nini mtu alie kijijin??

Pia maendeleo sio vitu ni Watu kua na hela so izo Treni ni Nini?

Tundu Lissu anasema Dar hakuna sehem ya kupumzikia je ni kweli?

Au Tundulisu ni Mtu anae taka kuiongoza nchi asio ijua?

Mpo vijana mbona hampendi kufikirisha hizo akili kila saa mnawaza mgando tu

Sent from my BLL-L22 using JamiiForums mobile app
 
Leo Mh Tundu Lissu kawaambia Watanzania na waandish wa Habar kua Serikali yake yeye italipanua jiji la Dar na kuakikisha Anaongeza usafiri wa Reli za umeme kwani Kujenga Mabara Bara tu Haitosh pia Anaongeza Mabas ya Mwendokas na kuupanua Mkoa wa Dar

Pia kasema Daresalam nzima Haina sehem Ambayo watu Wanaweza kwenda kupumzika na kusema kua serikal yake lazima itafanya ayo

Tundu Lissu amekuwa akipiga kelele juu ya Miundombinu inayo jengwa Dar na kusema kua vitu ivyo havimfaidish mtu Wa kijijin na kusema kua je Watu watakula Madaraja? Au watakula ndege. Na mimi pia ningependa kumuuliza izo Treni atazo jenga zitamsaidia Nini mtu alie kijijin??

Pia maendeleo sio vitu ni Watu kua na hela so izo Treni ni Nini?

Tundu Lissu anasema Dar hakuna sehem ya kupumzikia je ni kweli?

Au Tundulisu ni Mtu anae taka kuiongoza nchi asio ijua?


Hii Awamu ya Tano imeleta watu wajinga kila mahali mpaka wasomi wenye akili na uwezo hawaeleweki na wanapoleta maoni yao yenye tija wanachukuliwa na vilaza wasaka teuzi kama huyu kuwa ni wapinga Miradi ya viongozi walio madarakani. Tundu Lissu ana akili, ujuzi na uwezo kuliko wagombea wote wa Urais na anachosema kuhusu usafiri Dar ni kweli kabisa kunahitajika mwingine zaidi ya Mabasi ya Mwendo Kasi ambayo ni Mabasi ya kawaida tu. Mabasi haya yanaitwa ya Kasi kwa sababu yanapita kwenye barabara ambako vyombo vingine vya usafiri haviruhusiwi kupita. Waliobuni Mradi wa Mabasi hayo walikuwa na akili kama za Lissu ambazo kwa bahati mbaya viongozi wa sasa, ikiwa labda ni pamoja na wasimamizi wa Mradi, hawana na wanapongezana kwa ufanisi. Hizo barabara za hayo Mabasi zilipanuliwa sana ili Mabasi ya kwenda upande mmoja yaende bila bugdha na yale ya upande wa pili nayo vivyo hivyo yaende bila shida na katikati ya njia mbili za Mabasi ilianchwa nafasi pana sana njia nzima wavuka kwa miguu wana madaraja yao ili wasigongwe. Sisi wa bara tunashangaa kuwa vilaza wanaachwa wawasemee viongozi wetu wote wa nchi hii walioko Dar mpaka waonekane hawajui kwa nini hizo barabara za Mabasi Kasi ni pana hivyo na wakazi wa Jiji hawaruhusiwi kutumia maeneo ambayo Mabasi hayapiti. Nafasi katikati ya barabara za Mabasi ilianchwa ili wakati ukifika na fedha ikipatikana zijengwe reli za treni (trams) mbili moja ya kwenda upande mmoja na ya pili upande wa pili bila kukutana. Baada ya barabara ya kwanza ya mabasi kufunguliwa mkandarasi wa reli angeanza kutandika reli na mpaka leo labda line moja ingekuwa imekamilika tayari kuanza kutumika. Treni hizo ndizo Lissu anazungumzia na zitakuwa zinapakia watu wengi zaidi kuliko Mabasi kwa gharama ndogo za uendeshaji maana zitatumia umeme na zitapita kwenye njia zao bila kuingiliwa na vyombo vingine vya usafiri. Wengi wa Dar wanakumbuka zile treni za Mwakyembe ambazo zilikuwa za TRC za safari ndefu na uzito mkubwa kwa hiyo gharama kubwa za uendeshaji
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Leo Mh Tundu Lissu kawaambia watanzania na waandish wa Habari kuwa Serikali yake yeye italipanua jiji la Dar na kuhakikisha anaongeza usafiri wa Reli za umeme kwani Kujenga mabarabara tu haitoshi pia anaongeza mabas ya Mwendokasi na kuupanua Mkoa wa Dar

Pia kasema Dar es salaam nzima haina sehemu ambayo watu wanaweza kwenda kupumzika na kusema kua serikal yake lazima itafanya ayo

Tundu Lissu amekuwa akipiga kelele juu ya Miundombinu inayo jengwa Dar na kusema kua vitu ivyo havimfaidishi mtu wa kijijini na kusema kua je Watu watakula Madaraja? Au watakula ndege. Na mimi pia ningependa kumuuliza izo Treni atazo jenga zitamsaidia nini mtu alie kijijini??

Pia maendeleo sio vitu ni watu kua na hela so izo Treni ni nini?

Tundu Lissu anasema Dar hakuna sehemu ya kupumzikia je ni kweli?

Au Tundulisu ni Mtu anae taka kuiongoza nchi asio ijua?


Selikari za majimbo kila Jimbo litaamua kushughulika na priorities,

Jimbo la dar litakenga brbr na reli Kama njia ya kurahisisha usafiri
 
Back
Top Bottom