Linux (Ubuntu, kubuntu, Debian, fedora, linux mint, kali linux, android etc) special thread

mwaminifuhalisi

JF-Expert Member
Feb 26, 2017
329
412
Katika thread hii tutaelimishana changamoto, faida, misaada na mambo mbalimbali yanayohusiana mifumo endeshi ya kompyuta na vifaa vingine vinavyotumia linux.
Tux.svg.png

Utangulizi
Linux ni mfumo endeshi wa kompyuta ulio na asili ya ule uliokuwa unaitwa UNIX, kwa mara ya kwanza Linux iliundwa na mwanafunzi aliyekuwa ametoka kumaliza masomo ya kompyuta sayansi mwanzoni mwa miaka ya tisini aitwae Linus Torvalds.
Linus_Torvalds.jpeg.jpeg

linus torvalds​

Mwanzoni Linux haikuanza kama OS bali ilikuwa ni kernel(drivers zinazoweza kufanya mawasiliano ya moja kwa moja na hardware ya kifaa chochote). Lakini kwa kuwa Linus aliifanya kernel yake kuwa ni open source(mifumo huria) ndipo kukatokea na watu wengine waliotumia maarifa yao na kuifanya linux kuwa kwa ajili hata ya kompyuta tena ikiwa na mtindo wa GUI (graphical user interface).

Mmoja wa watu hao ni marehemu Ian Murdock ambaye ni mwanzilishi wa OS kongwe ya linux ambayo ni GUI, Ian Murdock aliunda DEBIAN OS wakati akiwa ni mwanafunzi wa chuo kikuu akichukua shahada ya kwanza ya kompyuta sayansi kwa kushirikiana na wataalamu mbalimbali na kuiachia mwaka 1993, kwa bahati mbaya Ian Murdock alijiua kwa kujinyonga mwaka 2015.
250px-Ian_Murdock_interview_at_Holiday_Club_hotel_2008_(2).jpg

ian murdock​

Linux ni moja ya mradi uliofanikiwa sana kwa ushirikiano wa wataalamu mbalimbali wa kompyuta kutoka sehemu mbalimbali duniani kwani hivi leo asilimia kubwa ya seva duniani wanatumia linux, uwepo wa Android unafanya linux kuwa na watumiaji wengi sana kuliko mfumo mwingine wowote.

Hakika kama wanaIT tanzania tunataka kufanikisha vitu vingi vikubwa ni lazima tushirikiane na kushare maarifa huwezi fanya kila kitu ukiwa peke yako.

Tutaendelea kupeana maujuzi mbalimbali ya kwenye linux kwa kutumia Debian based OS kama vile Ubuntu ,Linux mint na Debian yenyewe.
 
Pande hii tumeshindwana kwenye softwares, otherwise ubuntu 16 ni nzuri sana. Zamani nilikuwa natumia wine kuziweka lakini haiwezi kufanya kazi kwa software kubwa.
 
Kwa Wanaotaka kudownload na kuweka kwenye kompyuta zao.
Kumbuka OS za linux zipo nyingi sana kiasi cha kwamba hatuwezi kuzieleza zote kwa ujumla, ila ambazo ni maarufu sana moja wapo ni Ubuntu, ambayo unaweza kuipata kwenye hii link ifuatayo.
Code:
http://mirror.aptus.co.tz/pub/ubuntu/16.04.2/ubuntu-16.04.2-desktop-amd64.iso

kama hutopendezewa na ubuntu kuna nyingine ambayo ina muonekano flani hivi unaoendana na windows, link yake ni hii hapa,
Code:
http://mirrors.evowise.com/linuxmint/stable/18.1/linuxmint-18.1-cinnamon-64bit.iso

Linux inaweza ikawekwa kwa pamoja na windows OS na data zako zikabaki kama zilivyo na hivyo kuwa na option mbili na kuchagua mojawapo.
 
Mbona zipo tu nyingi za kudownload bure muhimu ni kujua ipi itakufaa. Ambayo ipo popular sana ni Ubuntu ni very simple kuinstall na kutumia.
 
Nam nafurahi sana kwa kuanzishwa huu uzi kwan nina imani nitajifunza mengi sana hasa kwa kuwa leo nilishakua na kazi ya kubadilisha password ya admin kwenye server ya Edubuntu....basi hapa naona ndio mahala kwake... wale wataalamu wa commands za sudo.....nautilus huu ndio uwanja wao nadhani.. haya njooni mtupe maujuzi hapa
kubadilisha password fuata hatua hizi, ingia kwenye terminal
Code:
sudo -i
passwd jinaunalotaka
 
mi natumia Ubuntu.....mwaka wa 5 sasa.......sijawahi waza kutumia windows....... nipo na Gmac OS baada ya kutomia sana pear Linux .
 
Kwa wale watu wa graphic, zipo software kadhaa ambazo unaweza kufanya mambo mengi tu, baadhi ya hizo ni
1. Blender
2. Gimp

Jinsi ya kuinstall, bonyeza ALT+T, kufungua terminal halafu andika codes zifuatazo
Gimp, kwanza update
Code:
sudo apt-get update
sudo apt-get install gimp

Blender
Code:
sudo apt-get install blender
 
WEB developers, namna ya kuinstall Apache, PHP na Mysql katika linux ubuntu

1. Unatakiwa ku-update system yako kwa kuandika code ifuatayo
Code:
sudo apt-get update

2. Anza kuweka seva ya Apache
Code:
sudo apt-get install apache2

3. Anza kuinstall Mysql
Code:
sudo apt-get install mysql-server libapache2-mod-auth-mysql php5-mysql
Hapo utaona kuna line nyingine zimeongezeka hizo ni modules ambazo zinaunganisha mysql na php pamoja na apache2 server.

4. Anza kuweka php kwenye kompyuta yako
Code:
sudo apt-get install php5 libapache2-mod-php5 php5-mcrypt

pia haitakuwa mbaya kama ukiongeza file ambalo linaelezea php katika forder (directory index)
Kwenye Terminal andika code zifuatazo
Code:
sudo gedit /etc/apache2/mods-enabled/dir.conf

kwenye sehemu ambayo imeandikwa DirectoryIndex, ongeza neno index.php

Hapo tayari webserver inafanya kazi kabisa.

Kumbuka kwenye LAMP forder inayokaa mafile *.html na mafile mengine ya kwa ajili ya tovuti ni folder liloandikwa "www/html", ambayo adrsess yake ni /var/www/html, mfano unataka kuandika file .php andika code ifuatayo kwenye terminal
Code:
sudo gedit /var/www/htm/info.php

kisha itafunguka text editor ambayo utaongeza code ifuatayo
Code:
<?php
phpinfo();
?>

Kisha kwenye browser indiza adress ya localhost/info.php, kisha ikifunguka jua kila kitu kipo sawa.
 
KUJILINDA KWENYE MTANDAO NA MATEKNIKI MENGINE
Kwa wale ambao hawapendi kufuatiliwa ama kuweka kila kitu feki ikiwemo IP adress, basi kwenye linux tunaweza kutumia openvpn, hii ni vpn ambayo ianafanya kompyuta yako na IP address ya nchi nyingine na hivyo kompyuta yako kuonekana ikiwa nchi nyingine, faida zake utaweza kutembelea website ambazo zimezuiliwa nchini mwako, kuinstall andika code ifuatayo kwenye terminal
Code:
sudo apt-get install openvpn
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom