Lile lililosemwa kwamba ni andiko la Rioba mbona ni kama la 'Mwajuma Ndala Ndefu' akimnanga 'Chausiku' kwa kumchukulia bwana

Lile lililosemwa kwamba ni andiko la Rioba mbona ni kama la 'Mwajuma Ndala Ndefu' akimnanga 'Chausiku' kwa kumchukulia bwana

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
2,195
Reaction score
3,309
Yaani mtu amekabidhiwa TBC, chombo cha habari kikubwa halafu kwenye kuaga baada ya kukalia kiti miaka 10 anashukuru hakutumbuliwa na anaenda mbali zaidi eti anawananga wabaya wake hivi kweli? Mtu wa level ya Ryoba!?

Kwa dhamana aliyokuwa nayo kwa Taifa na usomi wa kuitwa 'Dr' inawezekana kweli? Badala ya kuja na tathmini ya mafanikio mliyoyafikia na changamoto zinazowakabili, unakuja na mambo ya uswahilini.

Kama hawa ndio wasomi tunaowategemea kuleta mageuzi, basi nchi isahau kabisa maendeleo.
 
🤣🤣🤣 Kwani huyu mkurugenzi anaishi wapi?.

Maana ukisoma andiko lake mzee wetu ametumia lugha ya watu wa Buguruni kwa Madenge,

Huenda huyu mstaafu amekulia kwenye mitaa yetu pendwa huku Tandika Maputo aka tambuka reli😇😇
 
Wabongo hatuna tofauti mkuu, kuanzia mamaduro na mwenzie msoga hadi chini kabisa kwa wauza magenge ni mipasho tu.

Ukitaka channel ya mipasho toleo jipya, fungua Bunge line, utachoka na kujiuliza kama kuna mtu serious alibaki ndani ya sisiemu labda wasira anayeamini kufoka ndio udumembegu!
 
Bila aibu anaweza kusema lile "andiko langu la kustaafu" aibu naona mie, andiko la Doktori wa PhD sijui ni ya jalalani ile au nje, maana hata aliyepatia nje bado hana change of behavior
 
Duh
 

Attachments

  • 1774278074067.jpg
    1774278074067.jpg
    89 KB · Views: 2
Back
Top Bottom