Head prefect
JF-Expert Member
- Apr 16, 2013
- 225
- 108
***nimeipenda hii***
Habari wana MMU:
Utafiti unaonesha kuwa kuna baadhi ya vitu vilivyofanya ndoa za babu zetu zidumu tofauti na hizi za zama hizi. Mojawapo ya vitu hivyo ni aina ya malazi waliyolalia ikiwa ni ngozi za wanyama,mikeka na vitanda vya samadari vilivyokuwa na ukubwa usiozidi futi 2.5.
Udogo huo wa vitanda uliwafanya wanandoa kuwa karibu mno na kugusana usiku kucha. Hii iliwalazimisha kuongea hata kama wamegombana maana bila kusema "sogea huko" huwezi kupata nafasi ya kulala vizuri.
Baridi ilivyokuwa inaongezeka kunapokaribia kucha iliwalazimu wasameheane hata bila kuombana msamaha maana kugusana kule kuliwapa joto lililogusa mioyo yao na kufuta makosa yote na kuanza upya siku iliyofuata.
Sasa vitanda vyetu vya 5*6 na 6*6 havitoi nafasi ya kufuta makosa ya wanandoa kwani wakikoseana kila mtu anakuwa kwenye kona yake ya 6*6 na kusikia aibu ya kumgusa mwenziwe kutokana na makosa waliyofanyiana,nani aanze kumgusa mwenziwe? Nani aanze kupandisha mguu kwenye paja la mwenziwe wakati kulikuwa na ugomvi? Ngoma inakuwa droo mpaka asubuhi na ugomvi unakuwa palepale kila mmoja akijifanya nunda kwa kutompapasa mwenziwe.
Sasa je turudishe vitanda vyetu kwa fundi seremala virekebishwe viwe 3*6 ili viweze kusuluhisha wanandoa? Au tulalie mikeka kama ileeee ya babu na bibi ili tuondoe foleni ya kwenda kwa washenga,wazazi,mashoga na baba Paroko kusuluhisha majambo yetu????
~~~KARIBUNI~~~
Habari wana MMU:
Utafiti unaonesha kuwa kuna baadhi ya vitu vilivyofanya ndoa za babu zetu zidumu tofauti na hizi za zama hizi. Mojawapo ya vitu hivyo ni aina ya malazi waliyolalia ikiwa ni ngozi za wanyama,mikeka na vitanda vya samadari vilivyokuwa na ukubwa usiozidi futi 2.5.
Udogo huo wa vitanda uliwafanya wanandoa kuwa karibu mno na kugusana usiku kucha. Hii iliwalazimisha kuongea hata kama wamegombana maana bila kusema "sogea huko" huwezi kupata nafasi ya kulala vizuri.
Baridi ilivyokuwa inaongezeka kunapokaribia kucha iliwalazimu wasameheane hata bila kuombana msamaha maana kugusana kule kuliwapa joto lililogusa mioyo yao na kufuta makosa yote na kuanza upya siku iliyofuata.
Sasa vitanda vyetu vya 5*6 na 6*6 havitoi nafasi ya kufuta makosa ya wanandoa kwani wakikoseana kila mtu anakuwa kwenye kona yake ya 6*6 na kusikia aibu ya kumgusa mwenziwe kutokana na makosa waliyofanyiana,nani aanze kumgusa mwenziwe? Nani aanze kupandisha mguu kwenye paja la mwenziwe wakati kulikuwa na ugomvi? Ngoma inakuwa droo mpaka asubuhi na ugomvi unakuwa palepale kila mmoja akijifanya nunda kwa kutompapasa mwenziwe.
Sasa je turudishe vitanda vyetu kwa fundi seremala virekebishwe viwe 3*6 ili viweze kusuluhisha wanandoa? Au tulalie mikeka kama ileeee ya babu na bibi ili tuondoe foleni ya kwenda kwa washenga,wazazi,mashoga na baba Paroko kusuluhisha majambo yetu????
~~~KARIBUNI~~~