Ligi Kuu soka Tanzania bara kurudi kuwa na timu 16 msimu wa 2021/22

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Afisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura amesema kuwa mfumo wa Ligi Kuu ya soka nchini kujumuisha timu 20 utatumika kwa msimu wa 2019/20 pekee

Kwa msimu wa 2020/21 timu zitapungua na kubaki 18

Msimu wa 2021/22 timu zitapungua na kubaki 16

Wambura amesema kwa msimu huu zitashuka timu nne moja kwa moja daraja la kwanza, zitakazo kuwa nafasi ya 17, 18, 19 na 20 huku timu zilizoshika nafasi ya 15 na 16 zikicheza mchujo na mbili za daraja la kwanza

Aidha, utaratibu wa kupanda Ligi Kuu kwa timu za daraja la kwanza utakuwa vile vile kwa vinara wa makundi yao mawili kupanda moja kwa moja huku watakaomaliza nafasi ya pili kwenye kila kundi wakicheza mchujo

Je, ni uthibitisho wa kuwa tumefulia?
 
ishu ni kukurupuka, kurukia timu ishirini, check scotland wana timu 12tu, South Africa timu 16 tu ligi kuu.watu wanaangalia ubora na si bora league.
 
Kila siku kanuni zinabadilika, watu makini wanatakiwa kuendesha lile shirikisho la soka
 
TANZAGIZA.
Nashangaa Hadi Sasa hivi mwakyembe na wales karia bado wapo ofisini, hii nchi hii sijui kama tutafika..
 
Shida Si uwingi wa timu au upungufu shida ni ubora na uratibu mzuri wa ligi.Hata timu zikiwa 5 kama haijapangiliwa nikazi bure
 
Yaani tuko kama mlevi hatua moja mbele hatua mbili nyuma.. sijui tutafika lini🤷🤷🤷🤷
 
Hawa wahuni walishafeli na TFF yao. Hivi hkuna watu wengine makini wakuendeshà ligi na shirikisho la mpira hawa wahunì waondolewe
 
Back
Top Bottom