Lifahamu jiwe la Moabu

Lifahamu jiwe la Moabu

Jackwillpower

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2017
Posts
2,539
Reaction score
3,860
Jiwe la Moabu

katika mwaka wa 1868 kule Diboni, Yordani kulipatikana jiwe lifaamikalo kama Moabite Stone, lililogunduliwa na mwana Akiolojia na Mmishionari wa Ujerumani Klein. Jiwe hili linathibitisha vita ya wa Moabu dhidi ya Israeli kama ilivyoandikwa katika 2Fal 2 na 3.

Kati ya shuhuda za kiakiolojia za kabila hili la wa Moabu ni Jiwe la Mesha, linaloeleza ushindi wao dhidi ya mwana wa Mfalme Omri wa Israeli.

Jiwe hili lilikutwa limeandikwa maneno haya;

“Mimi ni Mesha […] Mfalme wa Moabub […] Omri alikuwa Mfalme wa Israeli, na akawatesa Moabu Moabu […]Nilichukua kutoka humo vyombo vya Yehova […] ilihali nyumba ya Daudi ilimiliki Horonaimu."

Jiwe la Moabu ni maelezo ya matukio yanayofanana na 2 Wafalme sura ya 3. Watu kadhaa wa Biblia na mahali hutajwa:
Jiwe la Moabu lilikuwa na umri unaokaribia miaka 3,000. Ni kipande cha jiwe la basalti jeusi lililosuguliwa likiwa na upande wa juu ulioviringishwa vizuri, lilikuwa na kimo cha karibu mita 1.2 likipita kidogo tu upana wa meta 0.6, na likiwa na unene unaokaribia meta 0.6.
images%20(7).jpg
1420583621.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jiwe la Moabu

katika mwaka wa 1868 kule Diboni, Yordani kulipatikana jiwe lifaamikalo kama Moabite Stone, lililogunduliwa na mwana Akiolojia na Mmishionari wa Ujerumani Klein. Jiwe hili linathibitisha vita ya wa Moabu dhidi ya Israeli kama ilivyoandikwa katika 2Fal 2 na 3.

Kati ya shuhuda za kiakiolojia za kabila hili la wa Moabu ni Jiwe la Mesha, linaloeleza ushindi wao dhidi ya mwana wa Mfalme Omri wa Israeli.

Jiwe hili lilikutwa limeandikwa maneno haya;

“Mimi ni Mesha […] Mfalme wa Moabub […] Omri alikuwa Mfalme wa Israeli, na akawatesa Moabu Moabu […]Nilichukua kutoka humo vyombo vya Yehova […] ilihali nyumba ya Daudi ilimiliki Horonaimu."

Jiwe la Moabu ni maelezo ya matukio yanayofanana na 2 Wafalme sura ya 3. Watu kadhaa wa Biblia na mahali hutajwa:
Jiwe la Moabu lilikuwa na umri unaokaribia miaka 3,000. Ni kipande cha jiwe la basalti jeusi lililosuguliwa likiwa na upande wa juu ulioviringishwa vizuri, lilikuwa na kimo cha karibu mita 1.2 likipita kidogo tu upana wa meta 0.6, na likiwa na unene unaokaribia meta 0.6. View attachment 2604230View attachment 2604231

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwanini mnapenda kuondoa "h" katika uandishi wenu. Sasa neno lifaamikalo ndio kitu gani? Mnakera mno kwa kuharibu lugha yetu adhimu ya kiswahili.
 
Onesha wapi nimeondoa "h"

Sent using Jamii Forums mobile app
Soma habari yote uliyoandika. Kuna sehemu umeandika lifaamikalo badala ya lifahamikalo. Kama ni typo error ni sawa. Nimeamua kukemea kwa kuwa imekuwa ni trend kwa wengi siku hizi kuondoa herufi h kwa makusudi. Kumekuwa na maneno Kama ali badala ya hali, maindi badala ya mahindi, aimbi badala ya haimbi, amsini badala ya hamsini, n.k. Tushirikiane kukemea huu upuuzi.
 
Back
Top Bottom