Kwani wapi nimesema inazuia kufa?Kwahiyo hiyo chanjo inazuia kufa?
Kuna vitu vya kijinga sana mkuu,hivi wazee wangapi hawavai hata barakoa huku mtaani na hawajachanjwa hizo chanjo ila hawajafa wala kuumwa hiyo corona yao?Achana na Kiranga mkuu ni agent wao,anahamasisha hivyo.
Umehusisha kifo cha mtu na kutokuchanjwa kwa hiyo chanjo ya corona kwa maana kama angechanjwa asingekufa,ndio maana nakuuliza kwani chanjo inazuia kifo?Kwani wapi nimesema inazuia kufa?
Unapotaka kuvuka barabara utaacha kuangalia magari kulia na kushoto, uvuke barabara tu bila kuangalia magari, kwa sababu kuangalia magari kulia na kushoto hakuzuii kufa?
Dawa gani Tuliochukua kule MalaysiaNdugu unaongelea hizo kitu wakati hata ile ya Malaysia ilienda kuchukuliwa kwa gharama kubwa na WHO waliipinga ila mlikunywa kwa mbwembwe, sasa sijui huu uzi wako unamlenga nani?
Kwa hiyo ndugu yangu unabisha kwamba mambo makubwa yanayotokea duniani hayakupangwa? Mbona mambo ni wazi sana.Mtu kama Bill Gates, kwa mfano huyu ndiye mvumbuzi wa Microsoft.
Kwa mlimwengu wa sasa, mtu huyu lazima awe tajiri.
Sijui maisha yake ya ndani. Lakini kwa hili la uvumbuzi wa microsoft, linaeleza huyu ni mtu mwenye uwezo wa hali ya juu ya akili.
Fahamu ndugu kwamba utajiri ni sifa. kama hauna hizo sifa huwezi kuwa tajiri. Fanya utafiti utagundua kwamba watu ambao ni matajiri wa kweli wana sifa fulani zinazofanana, popote ulimwenguni. Mazingira yanaweza kumdhoofisha au kumstawisha, lakini sifa zao zinafanana; ni zilezile.
Madai kwamba kuna kundi la watu la siri linalofanya mipango mbalimbali; ikiwemo kutengeneza magonjwa na kadhalika, kuuwa watu, kutaka kutawala dunia na kuweka utawala mmoja, huo ni uongo mtupu na madai hewa yanayoenezwa na watu fulani wakomonisti, wapagani; wafrika, waislama na wakristo waafidhina kwa maslahi yao binafsi ya ama uchumi, utawala na mamlaka au kuwadhofisha watu wasitafute ukweli.
Utasikia wakomonisti, wapagani na waafidhina wakisema; hapa wanawataja wazungu kwamba wanataka kutuangamiza waafrika au wanataka kuungamiza waislamu na kadhalika.
Lakini hao hao kwa upande mwingine wananunua silaha chungu nzima kwenye nchi zao, wanashughulikia zaidi silaha kuliko wanavyoshughulikia mambo ya elimu, afya, chakula na ustawi wa watu.
Kwao kuwadhoofisha watu, ununuzi wa silaha na dhuluma dhidi ya watu wao sio maangamizi na mauaji, sio uovu! Kwao uovu ni shughuli za kimaabara au magonjwa.
Kama kuna watu dunia hii wanafikiri kwamba wanaweza kutawala dunia kwa njia yoyote ile ambayo lengo lao ni kuuwa watu, "hao hawana akili"na hawataweza kutawala dunia.
Pia tufahamu kwamba dunia inasafiri hivyo inaenda mbele. Kama ilivyo dunia, watu nao wanaenda mbele. Hivyo kadiri muda unakwenda kila mtu anajua ukweli wa mamba na vitu.
Lakini pia ndugu duniani Serikali kuu ni moja tu ndivyo mambo yalivyo. Tusidanganye watu kama kuna Serikali huru isipokuwa Serikali inayoongoza dunia.
JOHNKEKE mkuu dah! Umeni-impress sana,you are a very well informed person.Watu wamelala sana usingizi,na naamini the NWO cabal walikuwa wanamlaani sana Magufuli kwa jinsi alivyokuwa anajaribu kuamsha the sleeping masses.Once more hongera sana.Kwa hisanadugu yangu unabisha kwamba mambo makubwa yanayotokea duniani hayakupangwa? Mbona mambo ni wazi sana.
Kwamba tuanzie ukoloni, mataifa ya Ulaya hayakukaa na kupanga kugawana makoloni na kuyatawala?
Je hawakuamua tena kupitia vikao na sheria kwamba sasa tuwape uhuru! wa bendera? Na tena hawakutengeneza mifumo ya kuendeleza unyonyaji wa kiuchumi na influence?
Unabisha kwamba mwelekeo wa dunia kupitia mikondo kama "globalization" si mipango ya wakubwa?
Hujui kwamba mifumo ya kibiashara, kijamii na kiuchumi inaamuliwa na mataifa makubwa kupitia sera sheria na propaganda zinazopelekea kuunda au kutumia vyombo vya kiutekelezaji kama UN, WTO, UNESCO nk?
Hujui mataifa makubwa G7 yanakuwaga na vikao tena vya siri kuamua wanaendelezaje maslahi yao binafsi kwanza katika dunia yote? Na cha ajabu hata wazungu wema huwa wanaandamana kupinga uovu kwa binadamu wa hii mikutano. Maandamano yamefanyika sana na yamekuwa yakitangazwa, alafu waafrika wengi ambao ni watetewa wakubwa wa hayo maandamano hatuna habari!
Kama hata hili la wazi kwamba ukimwi ulitengenezwa maabara kwa lengo la ku control population ya waafrika nalo ulijui basi ni hatari. Hiyo policy ya enzi za kina Kissinger nafikiri sasa hivi ni de-classified information, tafuta ujiridhishe. Matukio mengi upangwa kabla ya kutokea.
Ujui kwamba mataifa makubwa wana influence nani mwenye mtazamo upi wa mambo ndiyo awe kiongozi kwenye mataifa mengine? Na wasiye mtaka huu tumia mbinu mbalimbali ili atoke hata kwa kutumia njia za wazi Kama walivyofanya Haiti.
Unabisha kwamba US ili ku maintain u"super power" vile vile anatumia njia ya kuzuia mataifa mengine yasikue? Au ujui ugomvi wa kibiashara na uchumi wa China na US? Unabisha mfano kwamba ili kuendeleza maslahi yake US iko katika mataifa karibu yote duniani na kwamba vyombo Kama CIA vinatoa ripoti ya matukio na mwelekeo katika mataifa hayo na vilevile vinatekeleza kwa siri maamuzi na maelekezo ya nini kitokee kwa maslahi yao?
Ujiulizi kwa nini mataifa makubwa yanatumia fedha nyingi tena za serikali kuendesha vyombo vya habari kama VOA na BBC tena hata kwa lugha za mataifa mengine kama Kiswahili? Unashindwa kuona mwelekeo na nia ya matangazo ya vyombo hivyo. Uoni wanavyotumia ujanja, utaalamu na gharama kutucontrol culturally and psychologically?
Mambo yote makubwa na mengine madogo yanayotokea duniani upangwa. Na ni kwa manufaa ya wanao panga. Sijui kwa nini wengine wanakubali kupofushwa na propaganda kupitia vyombo vyao vya habari nk. wakati mambo ni wazi.