Leseni za udereva - Kanuni ya mafunzo wakati wa kuhuisha (Renew) itatekelezeka?

Asamwa

JF-Expert Member
Apr 13, 2012
3,709
2,458
Jana nilisikia kupitia Radio one kuwa Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani linaangalia uwezekano wa kutumia kanuni inayotaka kila mwenye leseni ya udereva kufanya mafunzo ya siku 5 hadi 7 ili kujikumbusha sheria za usalama barabarani wakati anapokwenda kuhuisha (Renew) leseni yake.

Hili linaweza kuwa wazo zuri; lakini utekelezaji wake unawezekana bila kuleta kero kwa wahusika?

Haya mafunzo yataendeshwa na kikosi cha usalama barabarani au shule na vyuo vya udereva? Kutakuwa na gharama au hakutakuwa na gharama?

Najiuliza kuhusu mafanikio ya huu utaratibu kwa kuwa hata ukaguzi wa magari wiki ya Nenda kwa usalama haufanyiki kikamilifu; Kinachoonekana kutiliwa mkazo ni uuzaji wa stika za kubandika kwenye magari!
 
Kwani leseni ni cheti hadi wakati Wa ku-renew mtu akumbushwe? Hawatambui kwamba mwenye leseni anakuwa ana experience zaidi!
Ningewaona Wa maana wangeandaa dodoso la maswali halafu wakikukamata njiani una leseni unaulizwa maswali yoote usipoyajibu unapokonywa leseni palepale. Hadi ukasome
 
Mikwara tu penye uzia penyeza rupia wanatengeneza mazingira ya kupiga pesa za madereva ukifika hapo unaambiwa kama una haraka njoo tuongee huku unaambiwa toa kiasi fulani nikujazie uende
 
Jana nilisikia kupitia Radio one kuwa Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani linaangalia uwezekano wa kutumia kanuni inayotaka kila mwenye leseni ya udereva kufanya mafunzo ya siku 5 hadi 7 ili kujikumbusha sheria za usalama barabarani wakati anapokwenda kuhuisha (Renew) leseni yake.

Hili linaweza kuwa wazo zuri; lakini utekelezaji wake unawezekana bila kuleta kero kwa wahusika?

Haya mafunzo yataendeshwa na kikosi cha usalama barabarani au shule na vyuo vya udereva? Kutakuwa na gharama au hakutakuwa na gharama?

Najiuliza kuhusu mafanikio ya huu utaratibu kwa kuwa hata ukaguzi wa magari wiki ya Nenda kwa usalama haufanyiki kikamilifu; Kinachoonekana kutiliwa mkazo ni uuzaji wa stika za kubandika kwenye magari!
Kila siku naongea hapa kuwa Jeshi la Polisi lijitahidi kuendesha mambo yake kwa kutumia tafiti zinazojibu nini kiini cha ajali. Sio kweli kuwa chanzo kikuu cha ajali ni kutojua sheria, moja ya vyanzo vibaya vya ajali ni kupuuza utii wa sheria, hilo tatizo ni kubwa na halitibiwi kwa kufundishwa au kukumbushwa maana hilo litategemea burasa na hekima ya mtu ambavyo hiyo sidhani kama jeshi la polisi linauwezo wa kuwabadilisha watu wenye tatizo la ukosefu wa hekima na burasa wanapoendesha magari. Ni sawa na hizi imani za dini, kufanya dhambi ni matokeo ya kutokutii mafundisho ya Mungu na wengi hufahamu amri na sheria lakini kutii ndiyo tatizo. Hata umfanyie mtu semina na warsha za namna gani kama hajaamua kubadilika na kuacha dharau na kupuuza mambo ya msingi tatizo litaendelea kuwepo. Fikiria daktari mbobezi ambaye hutumia sigara wakati anajua kuwa ni kitu hatari, huyu mtu wa namna hii unaweza ukampa semina elekezi juu ya madhara ya sigara utegemee ataacha?
 
Mikwara tu penye uzia penyeza rupia wanatengeneza mazingira ya kupiga pesa za madereva ukifika hapo unaambiwa kama una haraka njoo tuongee huku unaambiwa toa kiasi fulani nikujazie uende

Ni kweli unavyosema.
Inawezekana pia wanataka kubuni chanzo kipya cha mapato. Wakiweka kiwango kikazoeleka, wanajumuisha kwenye ada ya ku-renew leseni kama walivyojumuisha ada ya "fire" kwenye road license.
 
Back
Top Bottom