Leo tumemzika mpendwa Edward Magige kijijini Butiama

Poppy Hatonn

JF-Expert Member
Apr 9, 2021
2,102
2,718
Maziko yamekwisha kwa amani tunashukuru.

Kwanza tulikuwa Shinyanga tukamwita paroko kufanya ibada. Paroko hakuongea chochote zaidi ya kumgombeza maiti kwa tabia yake ya kutopenda kwenda kanisani alipokuwa hai.

Tukaenda Butiama ikafanyika misa, lakini hotuba ya paroko ilikuwa inaonyesha ulikuwepo mgogoro na kwamba ile misa kidogo isifanyike.

Hata hivyo, tumefanya misa na tumezika. Baada ya hapo mtu akatoa tangazo wanaukoo tukutane baada ya watu kutawanyika.

Tukafanya mkutano wa ukoo. Mtu akatoa hoja pale:"Mwalimu Nyerere amekufa, hakutuachia hela. Lakini, alikuwa anaheshimika, na yeye hayupo sasa, kwa hiyo ile heshima yake, yote ni yetu. Lakini watu wengine hapa wanafanya mambo ya ovyo. Kwa hiyo wachapwe viboko."

Baada ya mabishano ya muda mrefu, watu pale wamechapwa viboko.
 
First Born wa taifa ushazeeka sasa mwandiko wako inakua ngumu kukuelewa
Ngumu kuelewa,you are quite right. You are very right.
Lakini leo tulikuwa na primitive justice hapa.
Hawa watu walikuwa wanajirekodi hizi habari probably zipo Facebook sasa hivi.
In fact,mambo yaliyokuwa yanaleta mtafaruku ni mambo waliyobishana walipokuwa Facebook.
 
Maziko yamekwisha kwa amani tunashukuru.
Kwanza tulikuwa Shinyanga tukamwita paroko kufanya ibada. Paroko hakuongea chochote zaidi ya kumgombeza maiti kwa tabia yake ya kutopenda kwenda kanisani alipokuwa hai.
Tukaenda Butiama ikafanyika misa,lakini khutba ya paroko ilikuwa inaonyesha ulikuwepo mgogoro na kwamba Ile misa kidogo isifanyike.
Hata hivyo,tumefanya misa na tumezika. Baada ya hapo mtu akatoa tangazo wanaukoo tukutane baada ya watu kutawanyika.
Tukafanya mkutano wa ukoo. Mtu akatoa hoja pale:"Mwalimu Nyerere amekufa,hakutuachia hela. Lakini,alikuwa anaheshimika,na yeye hayupo sasa,kwa hiyo ile heshima yake,yote ni yetu. Lakini watu wengine hapa wanafanya mambo ya ovyo. Kwa hiyo wachapwe viboko."
Baada ya mabishano ya muda mrefu,watu pale wamechapwa viboko.
Ulibadili id?

Haunaga unafiki mzee.

Poleni mzee
 
Back
Top Bottom