Mkuu kuna matukio mengi yanayoonyesha ni jinsi gani waisrael walivyo makini when it comes kwenye masuala ya kulinda usalama wao. Usisahau ndege 100 za kivita walizozilipua pale Cairo ambazo zilikuwa zinasubiri amri kuruka na kwenda kufuta kabisa taifa linaloitwa Israel lakini kwa mshangao ndege zote 100 zililipuliwa hapo hapo uwanjani hata kabla hazijaruka na Rais Nasser alipata ugonjwa wa moyo aliposikia hii habari, ugonjwa ambao haukumuacha mpaka ALIPOFARIKI. Usisahau pia ile Radar iliyokuwa imewekwa karibu na Suez canal kwa ajili ya kumonitor ndege za Israel na makomandoo waliokuwa wametumwa kwenda kuilipua walirudi na kutoa taarifa kwamba hakuna haja ya kuilipua, ile ni ya kwenda kuchukua tu kwani hapakuwa na ulinzi makini. Na kweli walikwenda wakawaua walinzi, wakaifungua na kuibeba kwa helikopter mpaka kwao.
Hawa jamaa ni mwisho wa maneno na ndio maana dunia inawaogopa including nchi za europe na marekani yenyewe. Huwezi kusikia marekani ikilaani kilichofanywa na muisrael.
Tiba