Francis12
JF-Expert Member
- Sep 30, 2016
- 7,533
- 22,281
Anaandika Comred Malisa Godlisten
Leo January 05, 2017 Ben amefikisha siku 50 tangu simu yake ya mkononi ilipotumika mara ya mwisho maeneo ya Mburahati jijini Dar, na zimetimia siku 48 tangu taarifa za kupotea kwake zianze kutajwa.
Benard Focus Rabiu Saanane, Baba wa mtoto mmoja, mwanafunzi wa shahada ya uzamivu (PhD) chuo kikuu cha Maastrich nchini Uholanzi, mwanaharakati wa masuala ya demokrasia na utawala bora, na mtumishi wa CHADEMA Makao makuu hajulikani alipo kwa siku 50 sasa.
Pengine kuna watu wachache wanaojua alipo (waliomshikilia). Au pengine yeye mwenyewe ndiye anayejua alipo. Kuna nadharia nyingi zinazotolewa na watu mbalimbali kuhusu Ben. Wengine wakisema amekufa/kuuawa, wengine wakisema anashikiliwa na vyombo vya usalama kutokana na harakati zake (detention), wengine wakisema amefichwa na chama chake (mkakati wa kisiasa) na wengine wakisema amejificha yeye mwenyewe (kwa sababu anazozijua yeye).
Pengine moja kati ya nadharia hizi inaweza kuwa kweli. Lakini mimi na wewe hatujui ipi ni ya kweli, japo naamini siku moja tutajua ipi ni kweli.
Baada ya siku 50 za kuandika na kutoa taarifa mbalimbali kuhusu Ben, leo January 05, 2017 nasitisha utoaji wa taarifa yoyote kuhusu Ben, hadi itakapohitajika vinginevyo. Hii haimaanishi kuwa juhudi za kumtafuta zimekoma, hasha.! Nitaendelea kumtafuta Ben mimi binafsi na kupitia taasisi ya UTG ambayo inaendelea kufanya hivyo.
Tayari UTG ina mipango mingi inayoitekeleza kumtafuta Ben kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, Taasisi za serikali, na baadhi ya mashirika ya kiraia. Kwahiyo juhudi za kumtafuta zinaendelea na kwa sasa ni kubwa zaidi kuliko awali. UTG kama taasisi inaweza kutoa taarifa juu ya juhudi hizo, lakini mimi binafsi sitaandika tena jambo lolote kuhusu Ben, though namuombea usiku na mchana apatikane akiwa hai.
Japo kupatikana kwake akiwa hai au maiti ni majaliwa ya Mwenyezi Mungu. Naamini Mungu achunguzaye nafsi na mioyo siku moja atatuonesha Ben alipo, whether akiwa hai au akiwa maiti na tutajua yote yaliyotokea hadi kupotea kwake. Tuendelee kumuombea. [HASHTAG]#BringBackBenAlive[/HASHTAG].!
Malisa Godlisten
Leo January 05, 2017 Ben amefikisha siku 50 tangu simu yake ya mkononi ilipotumika mara ya mwisho maeneo ya Mburahati jijini Dar, na zimetimia siku 48 tangu taarifa za kupotea kwake zianze kutajwa.
Benard Focus Rabiu Saanane, Baba wa mtoto mmoja, mwanafunzi wa shahada ya uzamivu (PhD) chuo kikuu cha Maastrich nchini Uholanzi, mwanaharakati wa masuala ya demokrasia na utawala bora, na mtumishi wa CHADEMA Makao makuu hajulikani alipo kwa siku 50 sasa.
Pengine kuna watu wachache wanaojua alipo (waliomshikilia). Au pengine yeye mwenyewe ndiye anayejua alipo. Kuna nadharia nyingi zinazotolewa na watu mbalimbali kuhusu Ben. Wengine wakisema amekufa/kuuawa, wengine wakisema anashikiliwa na vyombo vya usalama kutokana na harakati zake (detention), wengine wakisema amefichwa na chama chake (mkakati wa kisiasa) na wengine wakisema amejificha yeye mwenyewe (kwa sababu anazozijua yeye).
Pengine moja kati ya nadharia hizi inaweza kuwa kweli. Lakini mimi na wewe hatujui ipi ni ya kweli, japo naamini siku moja tutajua ipi ni kweli.
Baada ya siku 50 za kuandika na kutoa taarifa mbalimbali kuhusu Ben, leo January 05, 2017 nasitisha utoaji wa taarifa yoyote kuhusu Ben, hadi itakapohitajika vinginevyo. Hii haimaanishi kuwa juhudi za kumtafuta zimekoma, hasha.! Nitaendelea kumtafuta Ben mimi binafsi na kupitia taasisi ya UTG ambayo inaendelea kufanya hivyo.
Tayari UTG ina mipango mingi inayoitekeleza kumtafuta Ben kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, Taasisi za serikali, na baadhi ya mashirika ya kiraia. Kwahiyo juhudi za kumtafuta zinaendelea na kwa sasa ni kubwa zaidi kuliko awali. UTG kama taasisi inaweza kutoa taarifa juu ya juhudi hizo, lakini mimi binafsi sitaandika tena jambo lolote kuhusu Ben, though namuombea usiku na mchana apatikane akiwa hai.
Japo kupatikana kwake akiwa hai au maiti ni majaliwa ya Mwenyezi Mungu. Naamini Mungu achunguzaye nafsi na mioyo siku moja atatuonesha Ben alipo, whether akiwa hai au akiwa maiti na tutajua yote yaliyotokea hadi kupotea kwake. Tuendelee kumuombea. [HASHTAG]#BringBackBenAlive[/HASHTAG].!
Malisa Godlisten