“Leo hapana mpenzi…..!”

“Leo hapana mpenzi…..!”

Mtambuzi

Platinum Member
Joined
Oct 29, 2008
Posts
8,809
Reaction score
15,439


Najua hamjaelewa ninataka kuzungumzia kitu gani. Labda nianzie mbali kidogo. Pindi mwanamke aingiapo katika uhusiano, msukumo wake wa kufanya mapenzi hupungua mno. Katika utafiti fulani uliowahi kufanywa kuhusiana na tendo la kujamiiana katika mahusiano ilibainika kwamba kwa miaka minne na nusu ya uhusiano wanawake walihitaji mapenzi mara kwa mara, na baada ya miaka ishirini, ni asilimia 20 kati yao waliohitaji kufanya mapenzi na wenzi wako kama kawaida.

Kwa wengine haifiki miaka ishirini, mara nyingi ni miaka kumi, tatizo hilo la, ‘usiku huu hapana mpenzi' huanza. Je umeelewa sasa nina maana gani? Naamini umeelewa.

Kwa upande wa wanaume hamu ya tendo la kujamiiana inabaki vie vile kwa muda wote wanapokuwa kwenye uhusiano. Watafiti wanasema msukumo wa mwanzo wa mapenzi kwa wanawake ni wa juu ili kudumisha mahusiano (Kuweka msingi). Hii inaenda kinyume na hitaji la kupendwa, ambapo asilimia 90 ya wanawake walio kwenye uhusiano kwa miaka kumi wanahitaji kupendwa wakati kwa wanaume, ni asilimia 25 tu ndio wanahitaji hilo.

Kama hujaelewa ninachosema ni kwamba, ikifika miaka kumi ya ndoa kwa mfano, mwanamke bado hitaji lake la kuona mume anamjali, anamsikiliza na kuwasiliana naye kihisia, linakuwa na nguvu ileile, wakati kwa mwanaume mahitaji hayo yanakuwa yameshuka sana, kwao siyo lazima sana………
 
Sipo kwenye ndoa but i think nikiingia ntahitaji kupendwa mpaka mwisho,,, "jamani nyie kupendwa raha acheni 2"
 
Uko sahihi na hii ki2 nahic ndo inaleta kero kubwa baadhi ndoa! Hadi vinyumba vidogo vinakuwa vingi mtaani! Kumbe ni kutofahamu mambo kama haya!!
 
Mimi naona pia Afya njema, Matunzo, lishe nzuri na stress free life, vina determine sex life style ya Partners!
 
Ngoja niache wazi hapa mkweo aone umeandika nini. Na mshua, i hope unafanya the same kwa mama ngina.
 
sasa mtambuzi nini kifanyike tuwe na hitaji linalofanana jamani, ndo mwanzo wandoa ndoano ikifikia point hiyo maana we hutamani kudo mwenzio ndo anaona mpango mzima , wewe unatamani care mwenzio anauna sio ishu mshakua watui wazima ,tutafika kweli
 
Kuna baadhi ya wanaume wanafikiri mapenzi ni kitandani tu, wanashindwa kuwaandaa wake zao kisaikolojia kabla hata ya kufika kitandani. Haijalishi mmeishi katika ndoa kwa muda gani lakini kama upendo kwa mke upo hakutakuwa na udhuru huo. Imagine umetoka kumgombeza mkeo au umemjibu vibaya then unaenda kitandani unaanza kumtomasa na unataka akubali kufanya mapenzi (NI NGUMU KWA MWANAMKE). Mwanamke anayependwa hasubiri kuanzwa na katu hutasikia "Leo hapana mpenzi" Hata neno la Mungu linasema "ENYI WAUME WAPENDENI WAKE ZENU". Hivyo mkiwapenda wake zenu mtafaidi sana tendo la ndoa.
 
I am still single I think I am not concerned with this marriage business
nc wikend
 
Naunga mkono hii hoja....but naona kama imechangiwa na nature vile, ukiifuatilia kwa umakini sana kuanzia historia za watu wa zamani,vitabu vya dini,mazingira ya watu na mitindo ya maisha utagundua hilo! kuondoa hii ni imani na maombi peke yake...though inaaminika kwamba you cant go against nature
 


Kama hujaelewa ninachosema ni kwamba, ikifika miaka kumi ya ndoa kwa mfano, mwanamke bado hitaji lake la kuona mume anamjali, anamsikiliza na kuwasiliana naye kihisia, linakuwa na nguvu ileile, wakati kwa mwanaume mahitaji hayo yanakuwa yameshuka sana, kwao siyo lazima sana………

Hii shughuli kubwa kuliko maelezo.
Qa mtaji huo nyumbandogo hazitakaa ziishe.

Bazazi katika ufuatiliaji wa Kadhia.
 
...Nature is perfect.
I believe males were made to mate multiple females, across species. And that will keep on revealing itself now and then.
 
lakin Mtambuzi kuna sababu ambazo tunaweza kusema zinachangia. ila kabla sijaendelea naomba ninukuu moja ya misemo maarufu sna LIFE STARTS AT 40.

haya tuendelee,

wanaume wengi sana katika kipindi cha kuoana hadi mnamaliza kuzaa huwa anakuwa na hamu ya mwenzie kweli na mara nyingi sana ukaribu huwepo na hata kama anakidumu but family issues kwao bado huwa kubwa sababu kubwa ni ipi??
kwa mtazamao wangu huona sababu ni:-
a) ndio wakati ambao wao kama waanzilish wa familia wanakuwa bize na mambo ya uzazi na ulezi wa watoto wadogo
b)ndio wakati ambao wanaume hupenda zaid kushirikiana na mkewe kwaajili ya maendeleo ya familia hasa mambo ya ujenzi nk hivyo hujikuta akilazimika kuwa karibu na mkewe.
c) ndio wakati ambao mume humuona mkewe kama mrembo na mzuri zaid kwani mwanamke anakuwa bado hajazeeka kiumbo, ngozi, nywele nk
d)wanakuwa wanashare most of their interest like wanapanga matumizi pamoja, watatoka kwenda site pamoja, kununua mapambo ya nyumba pamoja na hata kuanzisha miradi ya maendeleo pamoja.
e) ndio wakati ambao wanakuwa wanajikuta wanapata nafasi za kusimamia ndoa za marafiki zao hivyo most of the times hujikuta wakikumbushiana walikotoka na hata kusukumwa kurekebisha ndoa zao.

baada ya miaka 10 kwenye ndoa hapo ndipo yale niliyonukuu mwanzoni hujitokeza, kwani unakuta sasa maisha yameshawakolea.

baba akiangalia maisha yamemkubali, watoto wanasoma na namna ya kupata ada zao anajua, wamesha zeeka mialiko ya kusimamia ndoa sasa haipo tena ama hawaitaki tena, mwanamke ameshaanza kupata makunyanzi kwani ngozi huanza kuvutika, mwili nao kama ni mbaya huanza maradhi mara mgongo, mara kiuno, mara miguu etc, urembo wa mwanamke huanza kupungua, aina za nguo anazovaa huanza kubadilika etc.

hapa sasa baba unakuta mahitaj yake ya vitu vzr yapo juu zaid kwani kama kawaida wanaume hudanganywa na macho yao, ndipo ishu za nyumba ndogo huanza na kadhia kama hizo.

nini kifanyike??

mwanamke mwenzangu uliyeko ndoani usilemae, fanya kazi, maintain your looks kwa mazoez na aina za vyakula usikubali kuwa mzee kimwonekano. zeeka kiumri ila kimwonekano uwe kijana.jaribu na jitahd sana umvutie mumeo kwa mwonekano ili akuone mrembo kila iitwapo leo.ukiweza kuyahadaa macho ya mumeo huko nje hataona sababu ya kwenda. penda mazingira ya nyumba yako na kila baada ya muda buni kitu kipya mabacho utamshirikisha mumeo hasa kifedha na kiushauri kusudi upate muda wa kuwa nae mara kwa mara lol!

huwaga namsifu saa shoga yangu cacico yeye kama anaona hali inataka kuleta mushkheri utamsikia hubby naona tupake nyumba yetu rangi nyingine. halafu nimeskia kuna rangi nzuri kweli imetoka ukuta hautapata fungus wala kuloana inauzwa kias kadhaa hapo sasa mumewe huweka mikono kichwan ilasasa bi mkubwa ndo kaamua inabidi tu ajikute anaingia kwenye laini wanaanza tena tripu za madukani kusaka materials. umeona akili ya kaike inavyotumika hapa??
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom