Emc2
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 16,808
- 16,951
Nawasalimia wana bodi.
Nimefuarahi sana vyama vya upinzani kuungana. Ni hatua moja ya maendeleo kisiasa.
Lakini pamoja na kuungana inapaswa kila kitu kuwekwa wazi ili kieleweke ni nini makubaliano halisi. Maana kunaugomvi mwingi umewahi kutoka hapo nyuma. Mfano mwaka jana 2013 kumekuwa na ugomvi baina ya CUF na CHADEMA:-
Kwa kweli inayaka moyo sana.
Ila pointi yangu ni kwamba je huu muungano wa vyama hivi ni wa kudumu au wa mda? kama ni wa kudumu kwa nini kila kitu kisiwekwe hadharani ili kila mmoja akaelewa.
Je lengo la hivi vya ni kung'oa CCM au kuleta maendeleo kwa wananchi?
Kama ni kimoja ni jinsi gani sasa watafikia lengo lao wakati bodo kuna watu wanavidonda vinauma havijapona na hatujaona wakisameheana?
Kukubaliana viongozi haitoshi maana huku mitaani wanachama wa CUF na CHADEMA hawapendani bado hawajaaelezwa ule utofauti uliojitokeza umeishaje? Maswali ni mengi sana.
Hivi chukulia wewe ni mwanachama wa CUF halafu wenje ndiye mgombea na unalazimishwa umchague wakati alikuita shogha!!! inakuja akilini kweli?
Mimi ninataka kujua huu umoja ni wa namna gani?
Halafu ikumbukwe mwaka 2010 baada ya kuunda kambi ya upinzani Mbowe alikataa kuwahusisha wenzake kwenye kambi ya upinzani na akataka yeye tu ndiye mpakwa mafuta. Na ikumbukwe kuwa CHADEMA sasa inapumulia oxygen kwa hiyo inatafuta kick kupitia kwa wazoefu wa siasa kama akina Lipumba na Mbatia watu waliozoea kugalaganzwa vibaya ili kujificchia aibu.
Na wana JF wekeni alini huu umoja baada ya 2015 kila mmoja ataanza kumlaumu mwenzake ndiye aliye sababisha kushindwa vibaya. Na ndio itakuwa mwisho wa CDM, CUF na NCCR.
MOU haijakaa vizuri kwani haijaeleza toauti zinamalizwaje? imejikita katika madaraka tu. Haina sera yoyote zaidi ya kujikita kwenye madaraka.
Lipumba hataki uongozi mdogo anataka mkubwa ndio mnataka agombee uraisi? Itakuwa ngumi mbaya ya usoni. Slaa je? itakuwaje. Hapa patachimbika Lipumba hatakubali hata siku moja.
Wapinzani siwaelewi kabisa lengo lenu, maana vuguvugu la utofauti ni kubwa mno.
Nimefuarahi sana vyama vya upinzani kuungana. Ni hatua moja ya maendeleo kisiasa.
Lakini pamoja na kuungana inapaswa kila kitu kuwekwa wazi ili kieleweke ni nini makubaliano halisi. Maana kunaugomvi mwingi umewahi kutoka hapo nyuma. Mfano mwaka jana 2013 kumekuwa na ugomvi baina ya CUF na CHADEMA:-
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa chama cha CUF, kutokana na itikadi zake za mrengo wa Kiliberali ambazo miongoni mwa misingi yake mikuu ni pamoja na "kupigania haki za ndoa ya jinsia moja, usagaji na ushoga". Hii ni kwa mujibu wa tangazo lao kwenye mtandao wao wa umoja wa maliberali ulimwenguni, likiungwa mkono na Waziri wa Haki na Usawa wa Uingereza, Lynn Featherstone kutoka chama cha Liberal Democrats wakati chama hicho kilipokuwa kinapitisha azimio la kuruhusu ndoa za jinsia moja kama haki ya mtu mmoja mmoja, wanashirikiana na vyama kama vile LPC ya Canada, Det Radikale Venstre cha Norway, FDP cha Ujerumani, Israel Liberal Group cha Israel,PDS cha Senegal na Liberal Democrats cha Uingereza.
Kutokana na umoja huo, CUF wamekuwa wakipata msaada wa kifedha na nyenzo nyingine mbalimbali kutoka kwa vyama hivyo vya mrengo wa Kiliberali na msaada wa mwisho ni hivi majuzi mwezi Machi 2013 waliposaini makubaliano na chama cha Kiliberali kutoka Norway.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa CHADEMA, wapo kwenye Umoja wa Vyama vya Kidemokrasia Ulimwenguni (International Democratic Union - IDU). Huu ni umoja wa vyama ambavyo vipo kwenye mrengo wa kati na ambavyo msingi wake mkuu ni pamoja na kuwa na familia, kama taasisi muhimu katika jamii, ikimaanisha kwamba: "tunapinga vitendo vyote vya ushoga na usagaji". Tunatetea demokrasia, haki za binadamu na kupambana na ufisadi katika serikali. Vyama wanachama wa umoja huu ni pamoja na Conservative Party cha UK, CPP cha Norway, Republican cha Marekani na vingine vinavyofuata mrengo huo.
Kwa kweli inayaka moyo sana.
Ila pointi yangu ni kwamba je huu muungano wa vyama hivi ni wa kudumu au wa mda? kama ni wa kudumu kwa nini kila kitu kisiwekwe hadharani ili kila mmoja akaelewa.
Je lengo la hivi vya ni kung'oa CCM au kuleta maendeleo kwa wananchi?
Kama ni kimoja ni jinsi gani sasa watafikia lengo lao wakati bodo kuna watu wanavidonda vinauma havijapona na hatujaona wakisameheana?
Kukubaliana viongozi haitoshi maana huku mitaani wanachama wa CUF na CHADEMA hawapendani bado hawajaaelezwa ule utofauti uliojitokeza umeishaje? Maswali ni mengi sana.
Hivi chukulia wewe ni mwanachama wa CUF halafu wenje ndiye mgombea na unalazimishwa umchague wakati alikuita shogha!!! inakuja akilini kweli?
Mimi ninataka kujua huu umoja ni wa namna gani?
Halafu ikumbukwe mwaka 2010 baada ya kuunda kambi ya upinzani Mbowe alikataa kuwahusisha wenzake kwenye kambi ya upinzani na akataka yeye tu ndiye mpakwa mafuta. Na ikumbukwe kuwa CHADEMA sasa inapumulia oxygen kwa hiyo inatafuta kick kupitia kwa wazoefu wa siasa kama akina Lipumba na Mbatia watu waliozoea kugalaganzwa vibaya ili kujificchia aibu.
Na wana JF wekeni alini huu umoja baada ya 2015 kila mmoja ataanza kumlaumu mwenzake ndiye aliye sababisha kushindwa vibaya. Na ndio itakuwa mwisho wa CDM, CUF na NCCR.
MOU haijakaa vizuri kwani haijaeleza toauti zinamalizwaje? imejikita katika madaraka tu. Haina sera yoyote zaidi ya kujikita kwenye madaraka.
Lipumba hataki uongozi mdogo anataka mkubwa ndio mnataka agombee uraisi? Itakuwa ngumi mbaya ya usoni. Slaa je? itakuwaje. Hapa patachimbika Lipumba hatakubali hata siku moja.
Wapinzani siwaelewi kabisa lengo lenu, maana vuguvugu la utofauti ni kubwa mno.