Lembrus Mchome atimuliwa Chadema

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,891
Reaction score
6,416
Uongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro unapenda kuufahamisha umma kuwa haumtambui ndugu Lembruce Mchome kama Mwenyekiti wa Jimbo la Mwanga, kinyume na jinsi anavyojitambulisha katika shughuli mbalimbali.

Aidha, uongozi unapenda kuutaarifu Umma kuwa Mwenyekiti halali anayekaimu nafasi hiyo kwa sasa ni Mhe. Kirua Hassani Msangi, ambaye ndiye mwenye mamlaka ya kutekeleza majukumu ya uongozi wa Jimbo la Mwanga kwa mujibu wa taratibu na maamuzi halali ya uongozi husika.

Soma Pia: Chadema yamlima barua Mchome, yamtaka ajieleze ndani ya siku 14

Hivyo, wananchi, wanachama na wadau wote wanashauriwa kupuuza taarifa, matamko au utambulisho wowote unaotolewa na ndugu Lembruce Mchome kwa kujinasibisha na nafasi hiyo, kwani hautambuliwi na uongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro.

 
chadema bana 🤣
 
Kikatiba bado Lembris ni kiongozi wa CHADEMA. Hao waliomlima barua wakasome tena katiba ya CHADEMA inavyosema.
 
WAngesema aliondolewa kwenye hicho cheo lini na kupitia kikao gani. Na huyo anaye kaimu alikaimishwa kupitia kikao gani.

Amandla...
 
Chadema wanapaswa kuwa na template ya barua ya kumsimamisha na kumfukuza mwanachama ambazo zitatumika na matawi yao. Naamini viongozi wengi katika matawi yao hawana uzoefu wa kuandika barua rasmi. Matumizi ya hizo template yatawalinda endapo mtu atapinga uamuzi wa tawi lao.

Amandla...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…