Uongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro unapenda kuufahamisha umma kuwa
haumtambui ndugu Lembruce Mchome kama Mwenyekiti wa Jimbo la Mwanga, kinyume na jinsi anavyojitambulisha katika shughuli mbalimbali.
Aidha, uongozi unapenda kuutaarifu Umma kuwa
Mwenyekiti halali anayekaimu nafasi hiyo kwa sasa ni Mhe. Kirua Hassani Msangi, ambaye ndiye mwenye mamlaka ya kutekeleza majukumu ya uongozi wa Jimbo la Mwanga kwa mujibu wa taratibu na maamuzi halali ya uongozi husika.
Hivyo, wananchi, wanachama na wadau wote wanashauriwa kupuuza taarifa, matamko au utambulisho wowote unaotolewa na ndugu Lembruce Mchome kwa kujinasibisha na nafasi hiyo, kwani hautambuliwi na uongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro.
View attachment 3623933