Lema ataka Kambi ya Upinzani Bungeni ivunjwe kutokana na maoni yao kutosikilizwa, michango kuchujwa

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,885
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema(CHADEMA), amelitaka Bunge kuvunja Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kutokana na maoni ya kambi hiyo kutosikilizwa.

Aidha, lema amedai kuna kuchujwa kwa maneno yanayochangiwa na wabunge wa kambi hiyo katika mijadala katika kumbukumbu za Bunge(Hansard) alikodai kunafanywa na wafanyakazi wa Studio ya Bunge.

Aliyasema hayo bungeni mjini Dodoma jana asunuhi aliposimama na kuomba mwongozo wa Kiti cha Spika akidai kuwa michango ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imekuwa ikihaririwa na baadhi ya maneno yamekuwa yakiondolewa na hivyo kutorushwa kwenye studio hiyo na hata kwenye taarifa wanazopewa waandishi wa habari wa redio na televisheni.

Hata hivyo, katika mwongozo wake kuhusu suala hilo muda mfupi kabla ya kuahirisha shughuli za Bunge jana mchana, Mwenyekiti wa Bunge, Najma Murtaza Giga, aliyekuwa akiongoza kikao cha jana alisema Studio ya Bunge haina utaratibu wa kuchuja michango ya wapinzani isipokuwa kwa maelekezo ya Kiti cha Spika.

Katika hoja yake, lema alisema ni bora Bunge lingetoa mwongozo wa kuivunja Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni na lisipokee tena maoni yoyote kutoka kwao kutokana na maoni yao kutosikilizwa.

"Mheshimiwa Mwenyekiti mimi nimechangia Wizara ya Mambo ya Nje na (Ushirikiano wa) Afrika Mashariki, nikaenda nikaambiwa nijaze fomu, nimejaza kutaka kumbukumbu ya mchango wangu, mchango ambao haukuwa hata na mwongozo, haukuwa na taarifa wala utaratibu(bungeni)"

" Nimekwenda mambo yote yanayohusu mambo ya Acacia na Diplomasia ya Uchumi yametolewa, wamenibakizia pale panaposema tu mtu yeyote anayepinga rasilimali ni mwendawazimu na kipande hicho ndiyo kinazungushwa"

Akijibu hoja hiyo, Mwenyekiti Giga alijibu kama ifuatavyo

"Kilichotokea kwa mchango wa Lema ni kosa la kiufundi na linafanyiwa kazi na likitatuliwa anaweza kuomba kupewa mchango wake wote"

Giga aliongeza kuwa mbunge yeyote atakayekumbana na changamoto kama iliyompata Lema awasilishe malalamiko yake kwenye Ofisi ya Katibu wa Bunge.

Chanzo: Nipashe
 
Ikiwezekana ruzuku kwa vyama ifutwe kabisa...hatuwezi kutumia kodi kuwapa watu wanaotetea ukwepaji kodi.
 
Kwa nini anasubiri ivunjwe wakati kisheria wana uwezo wa kujiuzuru ubunge na kufanya hivyo watakuwa wameivunja kambi ya upinzani.

Lema analeta siasa za kinadharia wakati ukimnyima tu hata sitting allowance anapiga kelele achilia mbali kumwambia aache ubunge.
 
Kwa nini anasubiri ivunjwe wakati kisheria wana uwezo wa kujiuzuru ubunge na kufanya hivyo watakuwa wameivunja kambi ya upinzani.

Lema analeta siasa za kinadharia wakati ukimnyima tu hata sitting allowance anapiga kelele.
Ni kwa nini umnyime haki yake? Ni kwa nini ccm inang'ang'ania posho ya kukalia kiti?

Siku ikifutwa hii posho Uvccm msivyo na hata chembe ya aibu mtajifanya na nyinyi mnampongeza Magufuli.
 
Ikiwezekana ruzuku kwa vyama ifutwe kabisa...hatuwezi kutumia kodi kuwapa watu wanaotetea ukwepaji kodi.
Ccm wajinga si ndo walisaini mikataba na kupitisha sheria.
Ni nani anayekwepa kodi?
Si mnalipwa asilimia 3% ktk madini ninyi!!

Tume huru idaiwe mapema ccm itoke vinginevyo watanzania mtapata tabu sana.
 
Ironic language from Lema.. Not necessarily watz kueleweza now wataelewa baadae na kusafisha makosa kwa uchungu
 
Kwa nini anasubiri ivunjwe wakati kisheria wana uwezo wa kujiuzuru ubunge na kufanya hivyo watakuwa wameivunja kambi ya upinzani.

Lema analeta siasa za kinadharia wakati ukimnyima tu hata sitting allowance anapiga kelele achilia mbali kumwambia aache ubunge.

Ndio rahisi hivyo? Kambi rasmi ya upinzani inatambulika bungeni kikanuni hata ingekuwa na mbunge mmoja nadhani. kwa hiyo ubunge ni kitu kimoja na kambi rasmi ya upinzani ni kitu kingine
 
Ccm wajinga si ndo walisaini mikataba na kupitisha sheria.
Ni nani anayekwepa kodi?
Si mnalipwa asilimia 3% ktk madini ninyi!!

Ninyi ni wakina Mangungo,jinga kabisa.

Tume huru idaiwe mapema ccm itoke vinginevyo watanzania mtapata tabu sana.
Hapana so asilimia 3 ni 4%
 
Kweli mkuu...ruzuku inatakiwa wapewe tu wale wabunge wanaopitishaga sheria zinazo wa favour wakwepa kodi
Unaelewa maana ya ruzuku?
Pamoja na Ruzuku mnashindwa hata kuwa na ofisi ...kuna haja gani ya kuendelea kupewa?
Ruzuku mnatumia kwenye kesi za kutetea wanaorukana n.k
 
Kwa nini anasubiri ivunjwe wakati kisheria wana uwezo wa kujiuzuru ubunge na kufanya hivyo watakuwa wameivunja kambi ya upinzani.

Lema analeta siasa za kinadharia wakati ukimnyima tu hata sitting allowance anapiga kelele achilia mbali kumwambia aache ubunge.
kwanini mkate maneno na nyie, ujinga mtupu huu
 
Unaelewa maana ya ruzuku?
Pamoja na Ruzuku mnashindwa hata kuwa na ofisi ...kuna haja gani ya kuendelea kupewa?
Ruzuku mnatumia kwenye kesi za kutetea wanaorukana n.k
Kweli mkuu mimi mwenyewe sipo tofauti na mawazo yako..Mimi nataka kuliko chadema kupewa ruzuku bora tu ruzuku yote wapewe ccm waendelee kupitisha mikataba kama ule wa madini na huu wa gesi uliopitishwa kwa hati ya dharula juzijuzi
 
kwa kweli kwa bunge hili lililojaza wagonga meza tusitarajie maendeleo yoyote. cheki bajeti jinsi zinavyopita kimteremko utadhani hatuna wabunge.
 
Back
Top Bottom