GE2025 Lazaro Nyalandu: Tuwakumbushe vijana wetu, waumini wetu, kwamba hakuna tunu muhimu katika Taifa zaidi ya amani

GE2025 Lazaro Nyalandu: Tuwakumbushe vijana wetu, waumini wetu, kwamba hakuna tunu muhimu katika Taifa zaidi ya amani

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
844
Reaction score
1,604

Jamii hasa vijana, wamekumbushwa kutambua kwamba tunu ya pekee katika taifa ni amani, upendo na mshikamano hasa katika kipindi hiki kuelekea zoezi la kupiga kura na kwamba ni jukumu la kila mmoja kulinda na kuhakikisha uwepo wa amani hiyo. Hayo yamebainishwa leo Oktoba 20, 2025, na aliyewahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii hapa nchini, Lazaro Nyalandu, alipokuwa akizungumza katika kongamano la amani la viongozi wa dini mbalimbali linalofanyika mkoani Mwanza.

“Tuwakumbushe vijana wetu, waumini wetu, kwamba hakuna tunu muhimu katika Taifa zaidi ya amani, upendo na mshikamano. Tunapofanya zoezi hilo la kupiga kura, tunapowasisitiza watoke, basi tuhakikishe kila mtu anailinda hiyo amani, anashiriki katika upendo wa watanzania na anafanya zoezi la haki yake ya kupiga kura” amesema Nyalandu.

Amesema ipo haja ya Tanzania kuendelea kulea imani zote za dini, ambapo nchi pamoja na mamlaka husika zinajipambanua kukosa udini, badala yake kuruhusu amani na uhuru kwa watu wote pamoja na kuendelea kuishi kwa amani. Kongamano hilo limeandaliwa na Kamati ya amani ya viongozi wa dini mbalimbali mkoa wa Mwanza, wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Said Mtanda, likiwa na mada isemayo “Uchaguzi ni Muda wa Maamuzi, Tushiriki Sote. Tudumishe Amani na Mshikamano kwa Maendeleo ya Taifa”
 
Watu wamechafukwa na mahibiri ya amani.. Hapa ndio vijana wamefika
Screenshot_20251020-162802.png
 
Jamii hasa vijana, wamekumbushwa kutambua kwamba tunu ya pekee katika taifa ni amani, upendo na mshikamano hasa katika kipindi hiki kuelekea zoezi la kupiga kura na kwamba ni jukumu la kila mmoja kulinda na kuhakikisha uwepo wa amani hiyo. Hayo yamebainishwa leo Oktoba 20, 2025, na aliyewahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii hapa nchini, Lazaro Nyalandu, alipokuwa akizungumza katika kongamano la amani la viongozi wa dini mbalimbali linalofanyika mkoani Mwanza.

“Tuwakumbushe vijana wetu, waumini wetu, kwamba hakuna tunu muhimu katika Taifa zaidi ya amani, upendo na mshikamano. Tunapofanya zoezi hilo la kupiga kura, tunapowasisitiza watoke, basi tuhakikishe kila mtu anailinda hiyo amani, anashiriki katika upendo wa watanzania na anafanya zoezi la haki yake ya kupiga kura” amesema Nyalandu.

Amesema ipo haja ya Tanzania kuendelea kulea imani zote za dini, ambapo nchi pamoja na mamlaka husika zinajipambanua kukosa udini, badala yake kuruhusu amani na uhuru kwa watu wote pamoja na kuendelea kuishi kwa amani. Kongamano hilo limeandaliwa na Kamati ya amani ya viongozi wa dini mbalimbali mkoa wa Mwanza, wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Said Mtanda, likiwa na mada isemayo “Uchaguzi ni Muda wa Maamuzi, Tushiriki Sote. Tudumishe Amani na Mshikamano kwa Maendeleo ya Taifa”
Huyu ana kesi ya kubaka mtoto mdogo. Anaogopa nchi ikipata utawala wa sheria atapelekwa mahakamani.
 
Anayeichezea ni nani ? Huenda nasaa hii tukawapa watawala ambao wamesahau wahenga walivyowaambia (Ukila na Kipofu Usimshike Mkono) wao sio tu kuwashika bali kuwatemea mate....
 
Hakuna nchi yenye amani hapa, unyumbu wa kuhubiliwa amani umeshapitwa na wakati.
 
Atulize kij***io tarehe 29 inakaribia
 
Back
Top Bottom