Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Leo katika mkutano wa kampeni za lala salama za CUF mgombea ubunge wa chama hicho Lepold Mahona alizipiga kavukavu kavu kavu dhidi ya polisi na baadhi ya wanavijiji na ailzuiwa kuendelea na askari wa FFU waliokuwapo.
Kisa ni kwamba CUF waliingilia eneo la shule ya Msingi Nandekwa kutaka kufanya mkutano, huku eneo hilo lilikuwa limepangiwa CDM kufuatana na ratiba. Katika mabishano makali polisi iwalisisitiza CUF waliachilie eneo, ndipo Mahona akaja juu akidai alitukanwa vibaya na wafuasi wa CDM.
Alianza kurusha makonde kwa kila mtu aliyekuwa mbele yake lakini baadaye alidhibitiwa na FFU kama saba wenye virungu pamoja na viongozi wa chama hicho hadi ndani ya helikopta iliyokuwa ikiwasubiri.
View attachment 38183
Kipindi hiki cha lala salama huyu mgombea hakutakiwa kuonyesha upande wake mwingine. Huyu akiingua bungeni ataweza kung'uta hata microphone as long as iko mbele yake kwa hasira tu.