Lakini wazungu wanamkubali Lowassa kweli?

Lakini wazungu wanamkubali Lowassa kweli?

Radhia Sweety

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2011
Posts
4,433
Reaction score
1,772
Kwa asilimia kubwa, nchi za dunia ya tatu zinaendesha bajeti zao kwa kutegemea misaada kutoka nchi zilizoendelea, hususani Marekani na Jumuiya ya Ulaya.

Watoa misaada hao wamekuwa wakitumia udhaifu huo wa umaskini kutengeneza urafiki wa kinafiki na vyama vya siasa vinavyoongoza nchi hizi fukara.

Tanzania ni miongoni mwa nchi hizo. Tangu uhuru imekuwa ikiishi kwa misaada ya nchi za magharibi na kwa vyovyote vile nchi hizi ni wanufaika wakubwa wa rasilimali zetu. Na kwa vyovyote vile CCM imeshajitengenezea urafiki mkubwa na nchi hizi.

Mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi, ushindani mkubwa ukiwa baina ya mgombea wa CCM(John Magufuli)na yule wa Ukawa(Edward Lowassa). Hisia nyingi mtaani ni mapenzi makubwa kwa mgombea wa Ukawa.

Lakini wazungu wanamkubali Lowassa kiasi hiki kweli? Wazungu wapo tayari kuona mabadiliko kweli?Kuna sababu gani za msingi zitakazowafanya waiondoe CCM madarakani kama zipo?
 
Mods hii hoja nimeijenga kwa kutumia akili nyingi sana. Mkiifuta kizembezembe nitawafananisha sijui na kitu gani.
 
Kwa asilimia kubwa, nchi za dunia ya tatu zinaendesha bajeti zao kwa kutegemea misaada kutoka nchi zilizoendelea, hususani Marekani na Jumuiya ya Ulaya.

Watoa misaada hao wamekuwa wakitumia udhaifu huo wa umaskini kutengeneza urafiki wa kinafiki na vyama vya siasa vinavyoongoza nchi hizi fukara.

Tanzania ni miongoni mwa nchi hizo. Tangu uhuru imekuwa ikiishi kwa misaada ya nchi za magharibi na kwa vyovyote vile nchi hizi ni wanufaika wakubwa wa rasilimali zetu. Na kwa vyovyote vile CCM imeshajitengenezea urafiki mkubwa na nchi hizi.

Mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi, ushindani mkubwa ukiwa baina ya mgombea wa CCM(John Magufuli)na yule wa Ukawa(Edward Lowassa). Hisia nyingi mtaani ni mapenzi makubwa kwa mgombea wa Ukawa.

Lakini wazungu wanamkubali Lowassa kiasi hiki kweli? Wazungu wapo tayari kuona mabadiliko kweli?Kuna sababu gani za msingi zitakazowafanya waiondoe CCM madarakani kama zipo?

Nywele zake tu zinatosha kuwashawishi wampende....SWALI jingine?
 
Wapiga kura watachagua wampendae na sio anayependwa na wazungu
 
Mods hii hoja nimeijenga kwa kutumia akili nyingi sana. Mkiifuta kizembezembe nitawafananisha sijui na kitu gani.

Kama umejenga hoja kwa "akili nyingi sana", itaonekana tu huna haja ya kuomba rehema za Moderators.

Back to the topic sasa.
Unasahau ni katika kipindi hiki cha utawala mbovu wa JK Mrisho ndipo ubadhirifu mkubwa umewahi kutokea.

Tanzania inategemea misaada, na unachopaswa kutambua hata nchi zilizo katika uchumi wa kati na baadhi ya uchumi wa juu kabisa hutegemea misaada(hiyo ndiyo dunia ilivyo). Sasa tutakuwa wapumbavu, na naomba nirudie hili, Tutakuwa wapumbavu wa hali ya juu kutumia safari za Rais eti kigezo cha kuomba msaada? Tufute kazi za mabalozi sasa, if that's the case. Yaani jumla ya safari zote zinaweza kuteglngeneza bajeti ya nchi.

Pili, kwa rasilimali zilizo nchini ni kiwango kidogo sana, narudia kiwango kidogo sana cha misaada tunachotegemea.


Hatuhitaji wazungu kudetermine fate ya watanzania. Hapa ndipo tunaposema 'Liwalo na liwe', tunahitaji watanzania kumkubali mgombea not light/white skin.
 
Kama umejenga hoja kwa "akili nyingi sana", itaonekana tu huna haja ya kuomba rehema za Moderators.

Back to the topic sasa.
Unasahau ni katika kipindi hiki cha utawala mbovu wa JK Mrisho ndipo ubadhirifu mkubwa umewahi kutokea.

Tanzania inategemea misaada, na unachopaswa kutambua hata nchi zilizo katika uchumi wa kati na baadhi ya uchumi wa juu kabisa hutegemea misaada(hiyo ndiyo dunia ilivyo). Sasa tutakuwa wapumbavu, na naomba nirudie hili, Tutakuwa wapumbavu wa hali ya juu kutumia safari za Rais eti kigezo cha kuomba msaada? Tufute kazi za mabalozi sasa, if that's the case. Yaani jumla ya safari zote zinaweza kuteglngeneza bajeti ya nchi.

Pili, kwa rasilimali zilizo nchini ni kiwango kidogo sana, narudia kiwango kidogo sana cha misaada tunachotegemea.


Hatuhitaji wazungu kudetermine fate ya watanzania. Hapa ndipo tunaposema 'Liwalo na liwe', tunahitaji watanzania kumkubali mgombea not light/white skin.

Hii hoja nzito. Vilaza kaeni pembeni. Kuna tofauti kubwa ya nilichoandika na ulichopost.
 
Hivi majina ya selection za UDSM yameshatoka?
 
Fanyeni kazi kwa bidii, punguzeni magunia ya kodi yasiyo na ulazima, punguzeni matumizi ya hovyohovyo serikalini, dhibitini mianya ya kukwepa kodi, wawajibisheni viongozi wazembe pia wekezeni sana katika kilimo ili mpate malighafi za kulisha hivyo viwanda mnavyoota kuvijenga. Mkiyafanya haya hakuna haja ya kutaka mzungu amkubali rais wenu.
 
Hii hoja nzito. Vilaza kaeni pembeni. Kuna tofauti kubwa ya nilichoandika na ulichopost.

Nakushauri uje na majibu, maana nahisi unayo kabisa, haiwekani kila anayetoa analysis kwako ni kilaza njoo tufute tongotongo mkubwa
 
Hivi wazungu ndio wanatuchagulia viongozi jamani?
Au huyo Raisi anachaguliwa akawatawale wazungu?
 
innocent chacha ​ je wewe ni kijana wa ccm ? Kabla hatuja kujibu!
 
Mimi ni mvumilivu kama Lowassa. Umeona nimereact kwa kuitwa nyau?

Sasa unataka kujifananisha na Lowassa?

Yaani simply kwasabanu unatumia jina halisi na unaogopa kuonyesha hisia tukuite mvumilivu?

Uvumilivu wako haunisaidii chochote wala sihitaji kujua your threshold, nichohitaji ni wewe kujibu hoja kwa hoja, umeleta hoja nimejibu kwa hoja tuendelee from there wala si kutoa cheap comment "vilaza kaeni pembeni", Period.
 
Back
Top Bottom