Lahaja za kiswahili

Lahaja za kiswahili

Averos

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2010
Posts
994
Reaction score
703
Ni ipo lahaja ya kiswahili iliyo sahihi kuliko zote?
 
Lahaja za kiswahili zipo kama 15-20 na zote ni sahihi ( kuanzia kibarawa -somalia mapaka kikomoro)
Lahaja ilofanywa kuwa rasmi ni kiunguja mjini na ndio hii tunayosomeshwa na inayotumika kwenye vyombo vya habari......
Sifikirii kama ni sahihi kusema lahaja nyengine sio sahihi.........
 
mara nyingine lahaja ni kama lugha, na tukiangalia sifa mojawapo ya lugha ni UBORA, kwa maana ya kuwa hakuna lugha bora kuliko nyingine.

Hivyo lahaja zote ni sahihi, na zipo sababu zilizofanya kiunguja kichukuliwe kama lahaja ya usanifishaji.
 
kila mahali kuna lahaja yake na watu wake wanaiona sahihi...ukienda kenya watakuambia lahaja ya kimvita ilistahili zaidi kusanifishwa kuliko lahaja ya kiunguja.
 
Kweli sijui kiswahili...... Lahaja ni nini?
 
Back
Top Bottom