La Rojita - Spain Under 19 Champions of UEFA 2012

MAMMAMIA

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
3,811
1,603
Baada ya kaka zao La Roja kutwaa ubingwa wa EURO2012, vijana wa chini ya miaka 19 wametwaa ubingwa wa mwaka huu dhidi ya wapinzani wao Greece.
Kwa habari zaidi, bonyeza HAPA

Huu ni ushindi wa 6 kwa wadogo ndani ya miaka 11.

Wakati huo huo, timu ya Spain inayojitayarisha kwa michuano ya Olimpiki, juzi haikufua dafu katika mechi ya kirafiki dhidi ya Senegal iliyochezwa katika kisiwa cha Tenerife (Spain), ambapo wenyeji walilalazwa mabao mawili kwa yai. Kwa kweli katika mchezo huo tiu ya Spain ilielemewa sana na vijana wa Senegal.

Timu ya Spain ambayo wachezaji wake wa kikosi cha kwanza Juan Matta na Jordi Alba wamo kwenye timu ya Olimpiki, wataendeleza "ubabe wao" katika soka au ni "Upepo tu, utapita?"
 
nkupe siri ya spain na iweke akilini mwako.huwa mechi za kirafiki wanaboronga mbaya,ishu ni inapokuja mashindano ndio utakoma.fuatilia trend yao utagundua hlo
 
nkupe siri ya spain na iweke akilini mwako.huwa mechi za kirafiki wanaboronga mbaya,ishu ni inapokuja mashindano ndio utakoma.fuatilia trend yao utagundua hlo
Ni kweli yaser, kwani katika mechi za kirafiki walizocheza Latin Amerika baada ya kushinda kombe la dunia ungewaonea huruma walivyokuwa wanafungwa, na hata walipocheza na Portugal ya kirafiki walitwangwa 4-1.

Ninaifahamu La Roja tangu Olympics za Barcelona 1992 wakati timu yao ilipoibuka mabingwa, baada ya hapo walikuwa hawafanyi vizuri hadi 2008 waliposhinda UEFA2008. Sasa imebadilika sana na nina imani watamudu miaka mingi kwani subs zao zote ni nzuri (sub 15, 17,19,21) na timu ya taifa.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom