Bandiko kutoka X
LA PADRI KITIMA LINATEGUA KITENDAWILI CHA MUDA MREFU
Walianza kuwamwagia tindi kali kina Sheikh Soraga kwa lengo la kufitinisha na kuwagawa Wazanzibari. Wakamuua Padri Mushi Zanzibar, wakachoma moto Makanisa ya Zanzibar ili wafitinishe baina ya Watanganyika na Wazanzibari lakini kwa umuhimu mkubwa fitna baina ya Waislamu na Wakristo. Kusudi kuzima madai ya Wazanzibari kuhusu Muungano.
Ni watu wale wale ndio walio vamia kwenye Misikiti ya Zanzibar kuwakamata na kuwabambikia kesi za uwongo (kesi za ugaidi) ambazo zilisababisha wawawekwe kizuizini kwa uonevu, kinyume na sheria viongozi wa UAMSHO kwa karibu miaka 10 bila ya kuwakuta na hatia.
Hawa ni watu wale wale waliompiga risasi Sheikh Ponda, ndio wale wale waliompiga risasi Tundu Lissu. Ni watu wale wale walio wateka na kuwapoteza kina Ben Saanane na kina Soka na wengine.
Mwandishi Sammy Awami anawaeleza kuwa ni watu wenye ujasiri mkubwa. Naam ni kweli kwa sababu wao hufanya matukio kisha hujichunguza na baada ya hapo hakuna ripoti ya maana inayokuja huendelea kufanya ukatili wao.
Wala usidhani wanakereka na #NoReformsNoElection tu? Bali wanakereka zaidi na ile sauti ya wale wanaosema huu ni wakati wa kudai Tanganyika yao. Hili la muungano linawakereketa rohoni.
Alhamdulillah! Namshukuru Allah kuwa mambo haya sasa ameanza kuyabainisha hadharani ndugu zetu wa Tanganyika wameanza kuisikia na kuiona sura halisi ya ADUI yetu nyoka wa kijani. Inshaallah tutafika.
LA PADRI KITIMA LINATEGUA KITENDAWILI CHA MUDA MREFU
Walianza kuwamwagia tindi kali kina Sheikh Soraga kwa lengo la kufitinisha na kuwagawa Wazanzibari. Wakamuua Padri Mushi Zanzibar, wakachoma moto Makanisa ya Zanzibar ili wafitinishe baina ya Watanganyika na Wazanzibari lakini kwa umuhimu mkubwa fitna baina ya Waislamu na Wakristo. Kusudi kuzima madai ya Wazanzibari kuhusu Muungano.
Ni watu wale wale ndio walio vamia kwenye Misikiti ya Zanzibar kuwakamata na kuwabambikia kesi za uwongo (kesi za ugaidi) ambazo zilisababisha wawawekwe kizuizini kwa uonevu, kinyume na sheria viongozi wa UAMSHO kwa karibu miaka 10 bila ya kuwakuta na hatia.
Hawa ni watu wale wale waliompiga risasi Sheikh Ponda, ndio wale wale waliompiga risasi Tundu Lissu. Ni watu wale wale walio wateka na kuwapoteza kina Ben Saanane na kina Soka na wengine.
Mwandishi Sammy Awami anawaeleza kuwa ni watu wenye ujasiri mkubwa. Naam ni kweli kwa sababu wao hufanya matukio kisha hujichunguza na baada ya hapo hakuna ripoti ya maana inayokuja huendelea kufanya ukatili wao.
Wala usidhani wanakereka na #NoReformsNoElection tu? Bali wanakereka zaidi na ile sauti ya wale wanaosema huu ni wakati wa kudai Tanganyika yao. Hili la muungano linawakereketa rohoni.
Alhamdulillah! Namshukuru Allah kuwa mambo haya sasa ameanza kuyabainisha hadharani ndugu zetu wa Tanganyika wameanza kuisikia na kuiona sura halisi ya ADUI yetu nyoka wa kijani. Inshaallah tutafika.