Kwetu sote: "Asiyekubali kushindwa si mshindani"

Kwetu sote: "Asiyekubali kushindwa si mshindani"

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
34,775
Reaction score
46,058
Mabibi na mabwana heshima kwenu na moja kwa moja kwenye mada.

CCM, CDM, ACT,CUF, NCCR nk, mnaotupa karata zenu kuomba ridhaa kuongoza katika nyadhifa zozote zilizopo na sisi wapiga kura, uzi huu unatuhusu, sote kabisa.

Kama ilivyo katika mashindano, hatima ya ushindi au kushindwa kwenye uchaguzi wowote iko mikononi mwa wapiga kura ambao kwao jukumu hilo ni siri sirini - mioyoni mwao.

Viachwe vyama, wagombea na wapiga kura kwa starehe zao kutimiza majukumu yao.

Vitisho, hadaa, janja janja, laghai na vitendo vyovyote vya kutumia nguvu vinapaswa kukemewa na kupigiwa kelele na waungwana wote, kote ndani na hata nje ya nchi.

Haijalishi ni nani anataka kulitumbukiza taifa hili kwenye machafuko. Tusilazimishane. Uchaguzi wa mpiga kura ni uamuzi binafsi.

Wenye wajibu wa kulinda usalama na wafanye kazi yao bila kuwaathiri watia nia, vyama, mashabiki wala wapiga kura.

Tume ya uchaguzi itambue kuwa kazi yake iko kwenye idadi ya kura kama zilivyo pigwa na si vinginevyo.

Asiye kubali kushindwa si mshindani. Hatumhitaji yeye wala matokeo yake ya mfukoni au ya kulazimisha.
 
Ni yeye 2020 liwake jua inyeshe mvua kura yangu term hii inaenda kwake.
 
Ni yeye 2020 liwake jua inyeshe mvua kura yangu term hii inaenda kwake

Mawazo mgando kama kama ya mrugaruga huyu hapa chini:

IMG_20200814_185545_518.jpg


yanapaswa kukemewa vilivyo na kila mtanzania na hasa aliye mzalendo:

Tanzania ni kuu mno kwa yeyote kudhani yu ana hati miliki ya namna yoyote kwenye lolote na dhidi ya yeyote:

Wito: Chonde chonde, Tanzania ni zaidi mno ya yeyote
 
Wewe bro, CCM wanajua free na fair election wanakabidhi nchi...hawawezi kukubali hata kidogo!!
Ndiyo maana mataifa yote ya nje yapo mguu sawa!! Wanajua njama zote na wanajua TZ si salama tena.

Timbwili lazima liwepo tu!! Wananchi waandaliwe kisaikologia. Hupewi dola ukiwa umekaa...hilo la Arusha ni beep tu makubwa tena ya hatari yaja...

Ukiwa muoga achana na siasa!!
 
Wewe bro, CCM wanajua free na fair election wanakabidhi nchi...hawawezi kukubali hata kidogo!!
Ndiyo maana mataifa yote ya nje yapo mguu sawa!! Wanajua njama zote na wanajua TZ si salama tena.

Timbwili lazima liwepo tu!! Wananchi waandaliwe kisaikologia. Hupewi dola ukiwa umekaa...hilo la Arusha ni beep tu makubwa tena ya hatari yaja...

Ukiwa muoga achana na siasa!!

Asiyekubali kushindwa si mshindani - na kila mtu including jiwe anapaswa kujua au kujulishwa hivyo bayana.

Anayetaka kutuharibia ustaarabu wetu wenye kutambua kushinda na kushindwa na aambiwe hivyo wazi wazi bila ya kuangalia makunyanzi, hata kama huyo ni jiwe mwenyewe.

Vitimbi vyovyote kwa chama, mgombea, wagombea, mpiga kura, wapiga kura, au mashabiki havikubaliki!

Hivi sasa "basi" ni kwa maneno. Kwa kasi sana tunaelekea kwenye "makabiliano."

Tunayo nafasi ya kutokufika huko na huo ndiyo ulio msingi wa hoja.
 
Ajabu na kweli pana watu kwa kusikia "asiyekubali kushindwa si mshindani" wamefura kwa hasira mithili ya vifutu!

Kama kukubali matokeo hamtaki kwa nini mnapanga mtanange hali mkipanga kulazimisha matokeo? Kwanini kuwabugudhi wagombea na hata kupanga kuwaengua wengine mezani kwa sababu zenu za kubumba bumba kama kweli nyie siyo washari?

Kwa hakika atakaye kubali kushindwa huyo ndiye jembe letu wala si huyu ambaye anapambana kinyume cha utaratibu kutulazimisha kuwa tunampenda!
 
Anaekubali kushindwa ni loser!

Hiyo ni methali ya kwa manyani tokea katika "rules of the jungle."

Nyani na arejee kwa manyani wenziwe. Hana nafasi katika jamii ya watu waliostaarabika!
 
Ccm mnamuona mhutu wenu anakoipeleka nchi ?Si mlionywa kabla hamkusikia mkajifanya mnajua kuliko mama yake mzazi ,sass mwaka huu kwa dalili hizi si damu inaenda kumwagika sababu ya lihutu.
 
Tunakoelekea ni muda wa kuanza kumsaka mwenye kuweza kumfunga paka kengele tayari inasemekana pana maisha yamepotea huko Hai. Katu, huu siyo utanzania.

Watanzania siku zote tumejipambanua kama watu wenye kuweza kurumbana na kupambana kweli kweli lakini kwa hoja. Siyo kwa mawe wala risasi!
 
Back
Top Bottom