Kwenu nyie madereva wa bodaboda

Kwenu nyie madereva wa bodaboda

Indoraptor

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2019
Posts
251
Reaction score
508
Habari wanajamvi,

Kazi ya kuendesha bodaboda imekuwa kitega uchumi kwa vijana wengi hapa nchini, lakini hivi sasa jamii inawachukulia madereva wengi wa bodaboda kama wahuni tu hii ni kutokana na mazingira waliyojiwekea wenyewe

Nitatoa mfano mmoja huenda ikawa msaada wenu pia.

Siku moja nilikutana na rafiki yangu wa kitambo akiwa kijiweni na pikipiki yake akisubiri abiria. Lakini mwonekano wake ulikuwa sio wa kuridhisha kabisa.

Niliamua kumwambia ukweli na kumshauri abadilike jambo ambalo limedilisha mwenendo wa kazi yake, mwenyewe amekiri hata kipato chake kwa siku kimeongezeka na pia sio mtu wa kutegemea kusubiri mteja kijiweni. Kwa sasa kazi zake nyingi ni za simu na za uhakika (Tayari ana vichwa kadhaa ambavyo kila siku ni lazima awape ride). Hii kutokana na abiria kumkubali jinsi anavyoifanya kazi yake

Sasa ipo hivi madereva bodaboda embu jaribuni kuzingatia haya;


1. UENDESHAJI WA CHOMBO (PIKIPIKI)
Sio lazima ukimbize ndo uonekane upo fiti kwenye bodaboda.
Endesha mwendo wa kawaida
Endesha upande unaotakiwa kuendesha
Overtake upande unaotakiwa ku-overtake

Bodaboda wengi wanapopata ajali hata kama wao ndo wapo upande wa haki wataonekana wao ndo chanzo cha ajali kutokana na uendeshaji wao


2. IFANYE PIKIPIKI YAKO IONEKANE KWELI INAFAA KWA USAFIRI
Hapa bwana mnazingua sana kucheza na hizo exhaust zinapiga kelele ambazo hata watu hatuzipendi.

Arusha naona kuna mtindo mpya umeanza wa kung'oa taa ya mbele na kuweka taa ndogo mithili ya 'sportlight' ndo itumike kama taa kubwa(head light)

Embu jaribu kuweka chombo chako vizuri hata abiria asiwe na wasiwasi wa kupanda akidhani ni mbovu.

Weka pikipiki yako safi mda wote.

3. DEREVA MWENYEWE JIWEKE 'SMART'
Hata kama unashinda kijiweni isiwe sababu ya kupauka uso mda wote.
Jaribu kuwa na Hair style inayoeleweka
Sawa tunajua pikipiki inahitaji nguo nzito kwa ajili ya upepo basi ziwe safi na sio oversize
Achana na kunywa pombe mida ya kazi

Hayo ni kwa uchache tu, jaribuni kuzingatia hayo mtajenga uaminifu hata kwa abiria awe na moyo wa kukutafuta anapohitaji usafiri wa pikipiki.

Pendeni kazi yenu, itababili pia jamii inavyowachukulia kwa sasa

NIMEMALIZA
 
Mkuu kwa kikubwa namba 1 hapo ndio muhimu mno kuliko yote mana ukiwa rafu barabarani itakugharimu maisha, kovu na pengine pia kilema!

Boda boda wana haraka mno sijui ndio kukimbizana na hesabu ya boss!

Mimi pia nashauli serikali iwabane kwenye utoaji wa leseni zao itasaidia kupata madereva sahihi
 
Ka
Nimeweka ngao kwenye Gari Yangu kwa ajili ya Boda boda .
Yani boda jiingize tu napita na ww...Leo Asubuhi Kuna mmoja alikua mbele Yangu anaendesha ovyo nikamlenga ajibonyeze mwenyewe akawa amekwepa akatema mate yakarukia kioo nisingekua na haraka ningedeal nae.
Kaka acha ukatili utamaliza vijana ukiwaua
 
Boda akili zao wanazijua wenyewe
Kuna dogo mmoja boda namjuwa aliingiaga msafara wa rais,
Alikamatwa kupelekwa obay.
Bila kumfatilia,police kumchunguza
Angekaa sana ndani..
Boda boda wengi wana wenge wakiwa barabarani

Ova
 
..... boda boda anaweza akawa amempakiza wakili msomii, mfanyakazi wa taasisi nzuri, hata mfanyabiashara mwenye uwezo wa kuchukua tax ... akiwa anaendesha anahisi amepakiza boda boda mwenzieee --- mbio ka zote

*NB ni muhimu hata abiria kumwelekeza mwendesha boda boda mwendo autakao --- kufika salama
 
Habari wanajamvi,

Kazi ya kuendesha bodaboda imekuwa kitega uchumi kwa vijana wengi hapa nchini, lakini hivi sasa jamii inawachukulia madereva wengi wa bodaboda kama wahuni tu hii ni kutokana na mazingira waliyojiwekea wenyewe

Nitatoa mfano mmoja huenda ikawa msaada wenu pia.

Siku moja nilikutana na rafiki yangu wa kitambo akiwa kijiweni na pikipiki yake akisubiri abiria. Lakini mwonekano wake ulikuwa sio wa kuridhisha kabisa.

Niliamua kumwambia ukweli na kumshauri abadilike jambo ambalo limedilisha mwenendo wa kazi yake, mwenyewe amekiri hata kipato chake kwa siku kimeongezeka na pia sio mtu wa kutegemea kusubiri mteja kijiweni. Kwa sasa kazi zake nyingi ni za simu na za uhakika (Tayari ana vichwa kadhaa ambavyo kila siku ni lazima awape ride). Hii kutokana na abiria kumkubali jinsi anavyoifanya kazi yake

Sasa ipo hivi madereva bodaboda embu jaribuni kuzingatia haya;


1. UENDESHAJI WA CHOMBO (PIKIPIKI)
Sio lazima ukimbize ndo uonekane upo fiti kwenye bodaboda.
Endesha mwendo wa kawaida
Endesha upande unaotakiwa kuendesha
Overtake upande unaotakiwa ku-overtake

Bodaboda wengi wanapopata ajali hata kama wao ndo wapo upande wa haki wataonekana wao ndo chanzo cha ajali kutokana na uendeshaji wao


2. IFANYE PIKIPIKI YAKO IONEKANE KWELI INAFAA KWA USAFIRI
Hapa bwana mnazingua sana kucheza na hizo exhaust zinapiga kelele ambazo hata watu hatuzipendi.

Arusha naona kuna mtindo mpya umeanza wa kung'oa taa ya mbele na kuweka taa ndogo mithili ya 'sportlight' ndo itumike kama taa kubwa(head light)

Embu jaribu kuweka chombo chako vizuri hata abiria asiwe na wasiwasi wa kupanda akidhani ni mbovu.

Weka pikipiki yako safi mda wote.

3. DEREVA MWENYEWE JIWEKE 'SMART'
Hata kama unashinda kijiweni isiwe sababu ya kupauka uso mda wote.
Jaribu kuwa na Hair style inayoeleweka
Sawa tunajua pikipiki inahitaji nguo nzito kwa ajili ya upepo basi ziwe safi na sio oversize
Achana na kunywa pombe mida ya kazi

Hayo ni kwa uchache tu, jaribuni kuzingatia hayo mtajenga uaminifu hata kwa abiria awe na moyo wa kukutafuta anapohitaji usafiri wa pikipiki.

Pendeni kazi yenu, itababili pia jamii inavyowachukulia kwa sasa

NIMEMALIZA
natoka nje ya mada kidogo.

ila hawa jamaa wa bodaboda wanajua siri nyingi sana za wake za watu
 
Back
Top Bottom