Nafurahi kuwa rafiki yako ana misimamo mizuri. Kwanza fahamu kuwa ukimjua mwanamke kabla ya kuwa mkeo rasmi kuna mambo ya msingi ambayo baadaye hamtafurahia mtakapokuwa mmeoana... Hamtaheshimiana katika baadhi ya maeneo; Hamtakuwa na confidence ya kuwashauri wadogo zetu (wanandoa watarajiwa) kusubiri na hata kama mkiweza mtakuwa mnafanya kinafiki; Endapo mwanamke husika atapata mimba kabla ya ndoa heshima yake katika jamii itashuka; Mtoto atakayezaliwa baadaye mbeleni akifanya ufuatiliaji mdogo akafahamu mimba yake ilitungwa nje ya ndoa, atawapunguzia marks... TENDO LA NDOA NI TAKATIFU NA NI MUHIMU LIFANYWE KATIKA MPANGO WA MUNGU, nje ya hapo unapoteza baraka muhimu.. Anza na Mungu ufanikiwe kwa baraka zake.