ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,650
Tukiwa ndani ya gari (daladala-naomba msinizodoe jamani) kutoka nkuhungu kuja jamatini mjini dodoma, ghafla tukaona njemba inamshushia kipondo mpenzi wake. Ilibidi tusimame tukihofia huenda jambazi linampora mdada au huenda ndo suala zima la ubakaji. Baada ya kuwaamua, mwanamke akaamua kupanda gari kurudi zake ipagala-nadhani hamu ya sex ilimuishia baada ya kupata kile kipondo.
Mwanaume kwanza alimzuia asipande gari kutoka four ways, lakini mdada akakomaa kwa kusaidiwa nasi abiria, akapanda gari kuja jamatini. Kuona vile ile njemba nayo ikatinga garini. Kasheshe ilianza wakati wa kulipa nauli. Kumbe njemba ilikuwa inamtegeme mpenzi wake eti ndo amlipie nauli, na mwanamke alipogoma kumlipia kasheshe ikawa kati ya konda na njemba. Mwanamke kuona hivyo akashuka zake njiani kabla ya kufika mwisho wa safari.
Ile mwanaume anataka kushuka konda akamkwida shati na kumtaka alipe nauli. Kwa kuwa mwanaume hakuwa na hela, akataka kuleta ubabe, abiria wote tukamchenjia ndipo konda alipomshushia kipondo cha haja hadi jamaa akalegea huku nundu zikianza kumtoka kichwani. Kwa kujua kuwa tukimshusha pale aliposhuka mpenziwe angeweza kwenda kumaliza hasira kwa mpenziwe, konda akaenda kumshushia mbele zaidi kama umbali wa kilomita moja hivi toka aliposhuka mpenzi wake.
My take: Jamani vidume tusiwe tunajifanya 'vibesi' kwa mademu hasa kama unajua akibonyeza kitufe chekundu, we unakuwa kwishney! Na mapenzi ni zaidi ya huo ubabe wako ndani ya nyumba
Mwanaume kwanza alimzuia asipande gari kutoka four ways, lakini mdada akakomaa kwa kusaidiwa nasi abiria, akapanda gari kuja jamatini. Kuona vile ile njemba nayo ikatinga garini. Kasheshe ilianza wakati wa kulipa nauli. Kumbe njemba ilikuwa inamtegeme mpenzi wake eti ndo amlipie nauli, na mwanamke alipogoma kumlipia kasheshe ikawa kati ya konda na njemba. Mwanamke kuona hivyo akashuka zake njiani kabla ya kufika mwisho wa safari.
Ile mwanaume anataka kushuka konda akamkwida shati na kumtaka alipe nauli. Kwa kuwa mwanaume hakuwa na hela, akataka kuleta ubabe, abiria wote tukamchenjia ndipo konda alipomshushia kipondo cha haja hadi jamaa akalegea huku nundu zikianza kumtoka kichwani. Kwa kujua kuwa tukimshusha pale aliposhuka mpenziwe angeweza kwenda kumaliza hasira kwa mpenziwe, konda akaenda kumshushia mbele zaidi kama umbali wa kilomita moja hivi toka aliposhuka mpenzi wake.
My take: Jamani vidume tusiwe tunajifanya 'vibesi' kwa mademu hasa kama unajua akibonyeza kitufe chekundu, we unakuwa kwishney! Na mapenzi ni zaidi ya huo ubabe wako ndani ya nyumba