Jamani, kulikuwa na mada humu zikilalamikia makato yanayofanywa na CRDB bank, mpaka wengine kutishia kuhama bank hiyo na kutafuta huduma kwenye mabenki mengine. Kwa kweli leo nimepata fresh na kesho itabidi niende kwenye tawi lao nionane na manager nipate ufafanuzi juu ya hili.
Nisiwachoshe, ilikuwa hivi, niliingiziwa shilling million sita na mteja wangu na niliangalia salio nikakuta kweli zimeingizwa, baada ya muda Kama masaa mawili nilicheki tena salio baada ya kuona Kuna mtu humu amelalamika kuhusu makato, nilivyoangalia salio tena nikakuta zimefyekwa Tshs 25000/, salio lilisoma 5,975,000/ nikaona isiwe tabu labda wamekata makato yao ya mwezi kugharamia hiyo account.
Cha ajabu mpaka nimeaamua kuandika mada hii tena ni kwamba leo jumapili nimeamua kwenda kutoa pesa kiasi cha 5,900,000/, kwa ajili ya shughuli zangu hivyo nikajua zitabaki 75,000/ lakini baada kutoa na kucheki salio nikakuta zimebaki 29,000/ tu hivyo wamefyeka tena sh. 46,000/ hivyo jumla ya makato niliyokatwa kwa sh. 6,000,000/ nilizoingiziwa na mteja wangu ni sh. 71,000/ , inawezekana vipi hii?
Maana sijawahi kuona makato makubwa namna hii, nadhani kuna kitu kinaendelea ndani ya hii bank bila sisi wateja kujulishwa, hatua itabidi zichukuliwe.
Nisiwachoshe, ilikuwa hivi, niliingiziwa shilling million sita na mteja wangu na niliangalia salio nikakuta kweli zimeingizwa, baada ya muda Kama masaa mawili nilicheki tena salio baada ya kuona Kuna mtu humu amelalamika kuhusu makato, nilivyoangalia salio tena nikakuta zimefyekwa Tshs 25000/, salio lilisoma 5,975,000/ nikaona isiwe tabu labda wamekata makato yao ya mwezi kugharamia hiyo account.
Cha ajabu mpaka nimeaamua kuandika mada hii tena ni kwamba leo jumapili nimeamua kwenda kutoa pesa kiasi cha 5,900,000/, kwa ajili ya shughuli zangu hivyo nikajua zitabaki 75,000/ lakini baada kutoa na kucheki salio nikakuta zimebaki 29,000/ tu hivyo wamefyeka tena sh. 46,000/ hivyo jumla ya makato niliyokatwa kwa sh. 6,000,000/ nilizoingiziwa na mteja wangu ni sh. 71,000/ , inawezekana vipi hii?
Maana sijawahi kuona makato makubwa namna hii, nadhani kuna kitu kinaendelea ndani ya hii bank bila sisi wateja kujulishwa, hatua itabidi zichukuliwe.