Kweli CCM imedhamiria kuleta Vurugu Arumeru, Soma hii ya leo jioni...

yplus

Senior Member
Mar 20, 2012
153
69
Leo jioni mida ya saa 12 wakati wana CDM wakiwa Ngomeni kwao Elephant Logde wakiusubiri Msafara wa Mgombea ubunge wao toka Maji ya Chai, Alipita Binti mmoja akiwa amejifunga Scurf ya CCM na kuelekea Elephant Logde bila uoga wowote kwani hapo Palikuwa na wakereketwa wa CDM tu.

Kilichotokea hapo huyo Bint alivuliwa hiyo scurf yake na kuulizwa anataka nini, akajibu anataka kukaa hapo Elephant Bar, Scurf yake ilichukuliwa na kuchomwa moto na huyo Bint kuombwa aondoke kwani atawasababishia wamfanyie ukatili. Huwezi amini huyo Bint aligoma kuondoka, Vijana hao waligundua kuwa katumwa kuja kuchukoza wamtandike then iwe kesi Polisi na stori kwenye Kampeni kesho, aliachwa na alipoona hakuna mtu mwenye time nae akaamua kuondoka Mwenyewe.

Nawasihi CCM acheni kuwatumawatu kuchokoza wana CDM kwani mtasababisha vurugu zisizo na msingi...

Nawasilisha...
 
Enyi MAFISADI wote pamoja na chama CCM eleweni hili vema na kwa uwazi wake wote, ukweli wote ni kwamba;

... WaTanzania sote TUMESHAAMUA kwamba mambo yote ya ukombozi wa MTANZANIA kuondokana na MAFISADI ni kwa CHADEMA.

Je ni nani tena wa kutuzuia???
 
amebanwakila upande,mwangalie Mwiguliu michembe anaropoka tu ,kwani nani kamwambia kuwa uchaguzi huu ni wa kubadilisha utawala?think tank ya CCM iko wapi siku hizi au ndo kusema mwalimu alishikilia akili za wana CCM wote na kifo chake kimeondoka na CCM origional na kubaki CCM artificial.Kwanini hawanadi sera ila wanajibu kejeli zinazo fanywa na wananchi walio wachoka.Alichozungumza mzee Sendeka kinadhihirisha jinsi chama kilivyokosa matumaini na kubaki na blabla tu.Leo unasimama na kuzungumzia picha za mgombeawenu kupakwa lipstick na kuchorwa amevaa hereni kuna saidia nini wakati mwananchi wanahangaika na ukosefu wa maji ndani ya miaka hamsini.Ardhi imekuwa kikwazo wana wa Arumeru wamegeuka manamba ndani ya nchi yao,kuna tofauti gani na ukoloni wakati ardhi yao imebinafsishwa na kutumiwa kulima maua wakati hakuna chakula cha kutosha.

Arumeru wanahitaji elimu bora,huduma bora za afya,hawahitaji porojo,wanataka mapinduzi ya kifikra zaidi katika kujikomboa na udhalimu na dhuluma iliyosababishwa na uroho wa kujilimbikizia mali na kujaza matumbo ya wachache.Mapinduzi ya kweli ya kifikra yanategemea dhamira ya dhati ya wenye kuomba dhamana ya kuwapigania na kuwakomboa wana wa Arumeru.Dhana potofu inayojaribu kujengwa na wachovu wachache aidha kwa ulevi wa madaraka na kuvimbiwa matumbo yao kutokana na moto wa dhuluma ya mali ya umma unavyotukutia ndani ya matumbo yao.

Ukombozi wa wanaarumeru unategemea ushindi dhidi ya madhalimu wachache walioamua kula mpaka kukomba mboga.Ushindi huo ni bakora mujarabu kwa serikali na chama tawala kuwa wananchi wamechoshwa na maneno yasiyo na maana.Siku zote mwenye shibe hamkumbuki aliye na njaa.Kama kweli wanakubalika kuna haja gani ya kutumia nguvu kubwa na kugeuza utawala wa nchi kuwa ni royal family.Ni kweli Arumeru hakuna aliye na uwezo wa kuwaongoza na kuwawakilisha zaidi ya familia ya marehemu Sumari,kama kigezo ni utanzania na kupinga ubaguzi wa rangi basi Makongoro Nyerere ndiye alyestahili kuchukua viatu vya baba yake na si Mwinyi.Hatushangai naitakuwa shame on them kuona Ridhiwani,Fredrick,Hussein na wote mnao wajua watatawadhwa kuwa viongozi wa taifa hili.
 
therefore cdm you need to be careful for these tricks which are done by ccm if its true anyway!
 
Vijana msitumiwe na CCM, mtakufa bule na magamba mtayaacha, huyo binti alitaka kununua kifo kisicho chake. Kifo hiki ni cha CCM na magamba yao hivyo vijana msijiingize kichwakichwa mtafia huko maana watanzania wamekusudia baada ya miaka 3 ijayo CCM haitakuwepo Tz kama huamini kauli hii omba uzima uwepo.
 
katika mambo ya njama huyo binti anaweza kutengenezwa na chadema kwa ajili ya kukoleza au kuongeza chumvi kwamba CCM ni chama cha wakorofi
 
Kamanda si hilo tu siamini kama kweli mbunge wa mtera ana watoto nyumbani kwake, maana matusi aliyokuwa ayaporomosha wakati anamnadi mgombea wa ccm utadhani ndio kungwi.

Si hilo tu nadhani alikumbuka kazi yake ya zamani ya umc maana alijisahau kabisa pale stejini, ama ametumwa kuvuruga uchaguzi maana hawa jamaa wa magamba hawaaminiki mchana wapo pamoja usiku wanatengana
 
Afadhali CDM wamegundua mbinu chafu za CCM. Ukishamjua shetani wako hakupi shida
 
ccmwanajidanganya , labda kwa kuiba kura kwa sera zile ambazo hazitekelezeki , sijuiii labda itokee miujiza, ama waibe kura kama kawaida yao
 
Back
Top Bottom