Habarini! Nilipokuwa JKT sehemu fulani, siku moja msichana mlokole na anayesema anamjua Mungu alikuwa akipiga stori na mwenzake.
Katika stori akasema kwa kujisifia kuwa ameshawahi kuumiza vibaya moyo wa mwanaume wake aliyekuwa akimpenda sana, akasema kuwa mpaka mama wa mwanaume alikuwa akifahamu uhusiano wao.
Ilipelekea mpaka yule mwanaume kutaka kujiua ila binti anasema hakujali wala nini, na sababu kuu ya kumuacha na kuuvunja moyo wake ni kuwa, jamaa alimuomba demu sex, demu akakataa. Hapa naamini ni kweli alikuwa akijitunza na ndio maana akakataa kusex.
Pia anakiri kuwa huyu mwanaume wake alikuwa akimuhudumia kadri ya uwezo wake, vocha ameshamtumia sana na mambo mengine.
Binti huyu mlokole najiuliza ni kwa nini alikuwa katili hivi? Yaani anaongea huku anacheka bila hata chembe ya huruma kwa mwenzake!
Yaani unapataje raha ya kucheka na wenzio huku umemuumiza vibaya mtu, na yupo kwenye mateso? Kumbe hatutakiwi kuwaonea huruma na ninyi mkitendwa sio?
Kwa sababu huwa mnajiliza sana mkitendwa, yaani unamjeruhi mtu hivyo na hujali?