Kwanini wakatoliki wanashambuliwa na madhehebu mengine?

Kwanini wakatoliki wanashambuliwa na madhehebu mengine?

mdesi

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2013
Posts
1,373
Reaction score
2,251
Habarini wanajamii..

Mimi ni mkristo wa moja ya madhebu ya kikristo, huwa napenda kuheshimu kila imani ya mtu, hata kama haamini vile namini. Kilichonifanya kuja hapa; ni mashambulizi ya kihasira ya mda mrefu ambayo madhehebu mengine yanafanya dhidi ya hili dhehebu la kakatoliki au RC kama wanavyoita wengine.

Vitendo hivyo vilinifanya nianze kulifuatilia kwanini linashambuliwa tena wakati mwingine kwa matusi, na kwanini watu wanazingatia na kuudhiwa na imani ya mtu mwingine?

Katika kudadisi nikagundua SDA ndo wako mstari wa mbele wakifuatiwa na madhehebu mengine, ugomvi mkubwa ni kusali siku ya jumapili badala ya juma mosi, yaani wanaosali jumamosi ni kama hawajiamini hivyo kutumia nguvu kubwa kuwainesha wengine kuwa wako sahihi.

Zaidi ni wanalituhumu kuwa wana abudu sanamu, zaidi wanawapinga kuwa na sikukuu zao mbali mbali km vile Ijumaa kuu, Pasaka, Noel, etc. Cha ajabu hao wa RC ktk kuchangamana nao sijawahi ona wakidharau au kutukana madhebu mengine, hilo lilinifikirisha sana.

Nikafuatilia ibada zao including zile za juma pili na hizi za Alhamis na Ijumaa kuu, nimeona ni ibada ziko very calm, deep and very well organized, tofauti na nitokako (sina dhamira ya kuhama dhehebu langu).
Jambo lingine ambalo nime gundua madhebu mengi (including mine) kwa namna fulani yamefuata wakatoliki wanavyofanya nitatoa mifano michache:

I. Sikukuu za kidini:
Hapo kale dhehebu langu lilikuwa kama halijali hizo sikukuu, ila sikuhizi lime adopt ingawa hakuna miongozo ya nini hasa siku hiyo kinatakiwa kufanyika. Mfano kuna jumatano ya majivu ila hatupaki, kuna alhamisi na ijumaa kuu, usiku wa pasaka na pasaka. Niliwahi kusali RC pasaka mojawapo ya usiku, niliona wana mambo ambayo yako organised mahususi kwa siku hiyo and is like everywhere they do the same.

II. Kusali siku ya jumapili:
Na sisi tunasali siku ya jumapili kama RC ila hatushambuliwi hata kidogo na SDA kama wanavyoaashambulia RC, hapo sijauja ni kwa nini...

III. Kuwa na jumuiya mitaani:
Hapo awali hatukuwa na utaratibu huo, ila baadae ukaanzishwa km wafanyavyo RC.

IV. Mavazi ya wachungaji na maaskofu.
Wa kwetu wanavaa ya mfanano na RC hata askofu anavaa kofia ina pembe mbili na miraba miwili nyuma ila ile inavaliwa na maaskofu wa RC inasemwa kuwa ni alama ya 666 ila ya kwetu haisemwi hivyo kabisa.

V. Mazishi ya wafu:
Utafauti ni kuwa wa RC mtu akifariki huwa wawazi kabisa kuwa kwa imani yao wanaamini kuwa mtu akifariki hawezi fanya lolote tena, ila wana amini wanaobaki kwa maombi yao yanasikilizwa na Mungu hivyo kumuombea marehem, Mungu wa rehema anaweza msamehe makosa wakati wa hukumu kwa aliyetangulia.

Huku kwangu haiko wazi mtu akifariki tunasema habari yake imeishia hapo na hatuna utaratibu wa kuombea ila huwa tunafanya ibada kanaisani ingawa haiko specific.

Haya machache na mengine mengi dizain km tuna follow what RC has been doing.

My take ni kuwa ifike pahala tuache kushambulia imani ya mtu mwingine, ambaye haamni km unavyo amini wewe. Kunahaja gani ya kutoa lugha chafu za hasira kwa kitu ambacho hakikuhusu na haki athiri unacho kiamini wewe?

Matokeo yake madhebu ya kikristo yamekuwa ni mengi mno na makanisa binafsi yanazidi kujitokeza kila leo. Ila hawa wenzetu wakuwa watulivu hawabishani wala kuwatukana wenye mtazamo tofauti. Hakuna mwenye hati miliki ya Mungu. Mungu ni wetu sote ila namna ya kuwasiliana nae kila madhebu yana namna yao ila tusitake namna yako iwe yangu. Nawapenda sana!!
 
Kwanini mti wenye matunda au kigori huwindwa na kila Mtu?

Ubinadamu ni kazi/The humanity is work.
 
Habarini wanajamii..

Mimi ni mkristo wa moja ya madhebu ya kikristo, huwa napenda kuheshimu kila imani ya mtu, hata kama haamini vile namini. Kilichonifanya kuja hapa; ni mashambulizi ya kihasira ya mda mrefu ambayo madhehebu mengine yanafanya dhidi ya hili dhehebu la kakatoliki au RC kama wanavyoita wengine.

Vitendo hivyo vilinifanya nianze kulifuatilia kwanini linashambuliwa tena wakati mwingine kwa matusi, na kwanini watu wanazingatia na kuudhiwa na imani ya mtu mwingine?

Katika kudadisi nikagundua SDA ndo wako mstari wa mbele wakifuatiwa na madhehebu mengine, ugomvi mkubwa ni kusali siku ya jumapili badala ya juma mosi, yaani wanaosali jumamosi ni kama hawajiamini hivyo kutumia nguvu kubwa kuwainesha wengine kuwa wako sahihi.

Zaidi ni wanalituhumu kuwa wana abudu sanamu, zaidi wanawapinga kuwa na sikukuu zao mbali mbali km vile Ijumaa kuu, Pasaka, Noel, etc. Cha ajabu hao wa RC ktk kuchangamana nao sijawahi ona wakidharau au kutukana madhebu mengine, hilo lilinifikirisha sana.

Nikafuatilia ibada zao including zile za juma pili na hizi za Alhamis na Ijumaa kuu, nimeona ni ibada ziko very calm, deep and very well organized, tofauti na nitokako (sina dhamira ya kuhama dhehebu langu).
Jambo lingine ambalo nime gundua madhebu mengi (including mine) kwa namna fulani yamefuata wakatoliki wanavyofanya nitatoa mifano michache:

I. Sikukuu za kidini:
Hapo kale dhehebu langu lilikuwa kama halijali hizo sikukuu, ila sikuhizi lime adopt ingawa hakuna miongozo ya nini hasa siku hiyo kinatakiwa kufanyika. Mfano kuna jumatano ya majivu ila hatupaki, kuna alhamisi na ijumaa kuu, usiku wa pasaka na pasaka. Niliwahi kusali RC pasaka mojawapo ya usiku, niliona wana mambo ambayo yako organised mahususi kwa siku hiyo and is like everywhere they do the same.

II. Kusali siku ya jumapili:
Na sisi tunasali siku ya jumapili kama RC ila hatushambuliwi hata kidogo na SDA kama wanavyoaashambulia RC, hapo sijauja ni kwa nini...

III. Kuwa na jumuiya mitaani:
Hapo awali hatukuwa na utaratibu huo, ila baadae ukaanzishwa km wafanyavyo RC.

IV. Mavazi ya wachungaji na maaskofu.
Wa kwetu wanavaa ya mfanano na RC hata askofu anavaa kofia ina pembe mbili na miraba miwili nyuma ila ile inavaliwa na maaskofu wa RC inasemwa kuwa ni alama ya 666 ila ya kwetu haisemwi hivyo kabisa.

V. Mazishi ya wafu:
Utafauti ni kuwa wa RC mtu akifariki huwa wawazi kabisa kuwa kwa imani yao wanaamini kuwa mtu akifariki hawezi fanya lolote tena, ila wana amini wanaobaki kwa maombi yao yanasikilizwa na Mungu hivyo kumuombea marehem, Mungu wa rehema anaweza msamehe makosa wakati wa hukumu kwa aliyetangulia.

Huku kwangu haiko wazi mtu akifariki tunasema habari yake imeishia hapo na hatuna utaratibu wa kuombea ila huwa tunafanya ibada kanaisani ingawa haiko specific.

Haya machache na mengine mengi dizain km tuna follow what RC has been doing.

My take ni kuwa ifike pahala tuache kushambulia imani ya mtu mwingine, ambaye haamni km unavyo amini wewe. Kunahaja gani ya kutoa lugha chafu za hasira kwa kitu ambacho hakikuhusu na haki athiri unacho kiamini wewe?

Matokeo yake madhebu ya kikristo yamekuwa ni mengi mno na makanisa binafsi yanazidi kujitokeza kila leo. Ila hawa wenzetu wakuwa watulivu hawabishani wala kuwatukana wenye mtazamo tofauti. Hakuna mwenye hati miliki ya Mungu. Mungu ni wetu sote ila namna ya kuwasiliana nae kila madhebu yana namna yao ila tusitake namna yako iwe yangu. Nawapenda sana!!
If I were not a Catholic, and were looking for the true Church in the world today, I would look for the one Church which did not get along well with the world; in other words, I would look for the Church which the world hates. My reason for doing this would be, that if Christ is in any one of the churches of the world today, He must still be hated as He was when He was on earth in the flesh. If you would find Christ today, then find the Church that does not get along with the world. Look for the Church that is hated by the world, as Christ was hated by the world. Look for the Church which is accused of being behind the times, as Our Lord was accused of being ignorant and never having learned. Look for the Church which men sneer at as socially inferior, as they sneered at Our Lord because He came from Nazareth. Look for the Church which is accused of having a devil, as Our Lord was accused of being possessed by Beelzebub, the Prince of Devils. Look for the Church which theworld rejects because it claims it is infallible, as Pilate rejected Christ because he called Himself the Truth. Look for the Church which amid the confusion of conflicting opinions, its members love as they love Christ, and respect its voice as the very voice of its Founder, and the suspicion will grow, that if the Church is unpopular with the spirit of the world, then it is unworldly, and if it is unworldly, it is other-worldly. Since it is other-worldly, it is infinitely loved and infinitely hated as was Christ Himself. ... the Catholic Church is the only Church existing today which goes back to the time of Christ. History is so very clear on this point, it is curious how many miss its obviousness...BISHOP FULTON SHEEN.
 
Back
Top Bottom