Kwanini Wahindi Watoto huwa hawakai Boarding?

Kwanini Wahindi Watoto huwa hawakai Boarding?

MURUSI

JF-Expert Member
Joined
Jun 25, 2013
Posts
4,574
Reaction score
8,907
Ukijalibu kuchunguza hata kwa hizi International School utagundua kwamba Boarding wako watoto wa Kiafrica pekee hata na Watoto wa Wahindi na Wazungu wako Day yaani wanaenda na kurudi.

Niliwahi uliza Muhindi mmoja rafiki yangu ila hakunipa jibu la maana kwamba kwa nini wao watoto wao wako Day pekee?

Ila nilikuja baadae kuambiwa kwamba sababu kubwa wanataka kuwa monitor watoto wao hasa kimaadili na pia kimaendeleo, hii ni kwa sababu watapaswa kuwa na muda wa kupractise yale wanayo fanya wazazi wao hasa kwenye biashara na hii ndo sababu wanakuwa ni mihimu kukaa Day na pia wanataka ule umoja wa kifamilia usipotee kabisa.

Kwa sababu inasemekana moja ya sababu za ndugu kuanza kutengana ni kwa sababu waki wadogo muda wote walikuwa mshuleni Bording hivyo kupelekea mtoto kuoana kama wale rafiki zake wa shuleni ndo kama ndugu zake na pia mtoto kuanza kudevelop rabia ya kutaka kukaaa mwenyewe.

Cha ajabu sisi hadi watoto wa miaka 8 wako Bording na tunaona sawa kabisa kisa tu yuko na wakina Matron na Patron wanawalea yaani tunazaaa na tupo hai hatujafa ila jukumu la kumlea mtoto kimaadili anapewa Matron na Patron.
 
Hii ni kweli watoto wa wahindi hawakai bording hata kama shule ni ya wahindi tupu na mambo ya Boarding nchi nyingi waanza kuyapiga vita niliona hata Kenya wanataka shule zote ziwe day kwa sababu wanaona Bording watoto wana develop tabia za ajabu sana, how come shule ina watoto 500 na ina matroni mmoja au patron kwamba ndo awaleee hawa watoto? Sisi ndo tuna furahia kuona watoti hadi wadogo wako bording na huwa tunaona ni sifa mtaani na kazini
 
Suala la kukaa boarding kwa Tanzania ni suala la Kihistoria kwa sababu ya shule chache tangu miaka kabla ya Uhuru.

A. Shule chache

Mpaka mwaka 1997 hapa Dar es Salaam shule za sekondari za serikali kwa kidato cha kwanza mpaka cha nne ( O LEVEL) zilikuwa
1. Azania Boys - AZA BOY
2. Kibasila
3. Jangwani Girls
4. Forodhani pale St.Joseph
5. Kisutu Girls
6. Zanaki Girls

Tambaza ilikuwa inaanzia kidato cha tano (Advanced Level)

Hizo shule zilikuwa zinachukua wanafunzi wa kidato cha kwanza wasiozidi 2000; lakini kwa idadi ya shule za msingi Dar es Salaam wanafunzi ni wengi zaidi.

Sasa hawa wengine wanaenda katika shule zipi za Sekondari? Hapa sasa ndipo shule kama Kigonsera, Same, Tabora boys na nyingine zinakuja.

Sasa mtoto anayeishi Magomeni na wazazi wake atasafiri kwenda Tabora na kurudi kila siku. Hapo ndipo boarding ilipoanza. Uchache wa shule.

Ipo mikoa mingine katika miaka hiyo ilikuwa na shule moja ya sekondary mkoa mzima.

Kwahiyo suala la Boarding kwa kidato cha kwanza mpaka cha nne halikuwa suala la kuchagua bali suala la lazima kutokana na uwepo wa shule chache.


Baba yangu ilibidi ahamie wilaya nyingine kwa ajili ya elimu ya darasa la kwanza mpaka darasa la nne.

Ikabidi ahame tena mkoa kwa ajili ya kwenda kusoma elimu ya darasa la tano mpaka darasa la nane kwa sababu kwa wakati huo mkoa aliokuwa akiishi hakukuwa na shule ya kati (MIDDLE SCHOOL) kutoka darasa la tano mpaka darasa la nane.

Nitarudi kukupa sababu ya pili.....
 
NB:
Watoto wa Kihindi ni tofauti na watoto wetu kimalezi.
Mtoto wako akiruzi shule anaenda kucheza kwa majilani zako au kwa marafiki zake .
Mtoto wa kihindi akirudi shule ndani haendi kuzurula mtaani.
Jamaa wametuacha mbali sana

Sent from my SM-J500F using JamiiForums mobile app
Wana wa controo sana watoto wao Kimaadili aisee,
 
Suala la kukaa boarding kwa Tanzania ni suala la Kihistoria kwa sababu ya shule chache tangu miaka kabla ya Uhuru.

A. Shule chache....
Hii ni sawa na Kenya ila kwa sasa wanapiga vita mno Boarding school make mtoto anaenda Bording akirudi ameisha kuwa mlevi, msagaji, Mvita sigara na hata Mwizi.
 
Kwani tabia za kishoga huwa zinaanziaga wapi si huko huko boarding school
Acha uongo..hawa mapunga waliojazana uswahilini wamesoma shule gani ya bording.

Kimsingi suala la malezi na makuzi ya mtoto ni pana sana..kuanzia famila..marafiki..mazingira...hali ya uchumi..imani n.k

#MaendeleoHayanaChama
 
NB:
Watoto wa Kihindi ni tofauti na watoto wetu kimalezi.

Mtoto wako akirudi shule anaenda kucheza kwa majilani zako au kwa marafiki zake...
Hata wahindi (watu wazima) tofauti na sisi. Mtu akianza kazi anachukua mkopo NMB anaenda Kujenga banda Malamba Mawili halafu utegemee ulee watoto vizuri.
 
Hii ni sawa na Kenya ila kwa sasa wanapiga vita mno Boarding school make mtoto anaenda Bording akirudi ameisha kuwa mlevi, msagaji, Mvita sigara na hata Mwizi.
Upo sahihi sana, umri ambao watoto wanapelekwa boarding ndio muda wa wazazi/walazi ku-enforce tabia, desturi na tabia kwa ujumla.

Akiwa boarding hana mtu wa kumuongoza, hana mtu wa kumfundisha matokeo yake anaiga na kuwa na tabia anazokuta kwa wenzake.
 
Suala la kukaa boarding kwa Tanzania ni suala la Kihistoria kwa sababu ya shule chache tangu miaka kabla ya Uhuru.

A. Shule chache

Mpaka mwaka 1997 hapa Dar es Salaam shule za sekondari za serikali kwa kidato cha kwanza mpaka cha nne ( O LEVEL) zilikuwa
1. Azania Boys - AZA BOY
2. Kibasila
3. Jangwani Girls
4. Forodhani pale St.Joseph
5. Kisutu Girls
6. Zanaki Girls

Tambaza ilikuwa inaanzia kidato cha tano (Advanced Level)

Hizo shule zilikuwa zinachukua wanafunzi wa kidato cha kwanza wasiozidi 2000; lakini kwa idadi ya shule za msingi Dar es Salaam wanafunzi ni wengi zaidi.

Sasa hawa wengine wanaenda katika shule zipi za Sekondari? Hapa sasa ndipo shule kama Kigonsera, Same, Tabora boys na nyingine zinakuja.

Sasa mtoto anayeishi Magomeni na wazazi wake atasafiri kwenda Tabora na kurudi kila siku. Hapo ndipo boarding ilipoanza. Uchache wa shule.

Ipo mikoa mingine katika miaka hiyo ilikuwa na shule moja ya sekondary mkoa mzima.

Kwahiyo suala la Boarding kwa kidato cha kwanza mpaka cha nne halikuwa suala la kuchagua bali suala la lazima kutokana na uwepo wa shule chache.


Baba yangu ilibidi ahamie wilaya nyingine kwa ajili ya elimu ya darasa la kwanza mpaka darasa la nne.

Ikabidi ahame tena mkoa kwa ajili ya kwenda kusoma elimu ya darasa la tano mpaka darasa la nane kwa sababu kwa wakati huo mkoa aliokuwa akiishi hakukuwa na shule ya kati (MIDDLE SCHOOL) kutoka darasa la tano mpaka darasa la nane.

Nitarudi kukupa sababu ya pili.....
hawa tambaza, aza boy, kibasila na nyinezo ilikuwa fujo fujo kweli... shule zilijaza wahuni walio jielewa na wafata mkumbo...

boarding skuls ni nyingi kwa kipindi hicho hasa kulingana na mazingira ya wakati huo kulingana na hatua iliyopo kimaendeleo hasa miundombinu ya usafirishaji, njia za usafiri, na ikumbukwe ilikuwa jambo la kawaida mtu kufaulu toka rukwa kwenda pugu, au galanos tanga, ilbol arusha au ruvu, kilosa, minaki etc...

hivyo shule za bodi kwa wakati huo zilikuwa muhimu mno...
 
Na hawa watoto wa wahindi ni kazi sana kuwakuta na foleni interview tunazopambania sie pangu pakavu...
 
Kwani tabia za kishoga huwa zinaanziaga wapi si huko huko boarding school
Acha kukurupuka, ushoga mbona upo hadi mitaani,
Sema boarding huwa rahisi kugundulika kwasababu wale wavutiwao na watu wa jinsia moja huwa sasa wapo wanaishi kila siku na wenzao wa jinsia moja hivyo zile hisia zao lazima zitadhihirika

Yani ni kama boarding zenye wasichana na wavulana lazima kuna mahusiano yataonekana maana hisia lazima zitadhihirika
 
Ukijalibu kuchunguza hata kwa hizi International School utagundua kwamba Boarding wako watoto wa Kiafrica pekee hata na Watoto wa Wahindi na Wazungu wako Day yaani wanaenda na kurudi.

Niliwahi uliza Muhindi mmoja rafiki yangu ila hakunipa jibu la maana kwamba kwa nini wao watoto wao wako Day pekee?

Ila nilikuja baadae kuambiwa kwamba sababu kubwa wanataka kuwa monitor watoto wao hasa kimaadili na pia kimaendeleo, hii ni kwa sababu watapaswa kuwa na muda wa kupractise yale wanayo fanya wazazi wao hasa kwenye biashara na hii ndo sababu wanakuwa ni mihimu kukaa Day na pia wanataka ule umoja wa kifamilia usipotee kabisa.

Kwa sababu inasemekana moja ya sababu za ndugu kuanza kutengana ni kwa sababu waki wadogo muda wote walikuwa mshuleni Bording hivyo kupelekea mtoto kuoana kama wale rafiki zake wa shuleni ndo kama ndugu zake na pia mtoto kuanza kudevelop rabia ya kutaka kukaaa mwenyewe.

Cha ajabu sisi hadi watoto wa miaka 8 wako Bording na tunaona sawa kabisa kisa tu yuko na wakina Matron na Patron wanawalea yaani tunazaaa na tupo hai hatujafa ila jukumu la kumlea mtoto kimaadili anapewa Matron na Patron.
Kabla hujahoji kwanini hawasomi bweni na akina masawe na mkude, ushawahi jiuliza kwanini hakuna wahindi wanaoishi Goba, Kimara, ama Tabata!!!??!!
 
Pointi ni kuwa kutokana na uchache wao, hao wahindi hupendelea kuishi karibu na wahindi wenzao, kwa familia ya kihindi kumpeleka mtoto wao shule ya bweni ambayo mtoto ni minority kila kona hakuna wahindi wezie wao wanaona ni sawa na kumtelekeza mtoto.

Hivi hata wewe mtu mweusi utajiskiaje umpelekee mwanao shule ambayo wapo wahindi watupu yeye ahesabike jinsi alivyotofauti??

Lazima utahisi kuna kitu hakiko sawa, lazima at some point uhisi kuwa ni rahisi sana kwake kuonewa

Ndio maana hata mitaa wanayoishi, wahindi hupenda kuishi na wenzao, ndio maana wanaishi posta ama kariakoo, na Msione wana raha sana, kodi za huko posta ni kubwa sana kulipa, ila wanajitutumua kuishi huko, mradi tu wasiende kuishi maeneo ya mbali sana kama tunaoishi sisi waafrika ambako wao wakija kuishi watakuwa ni minority
 
Back
Top Bottom